Chaos Master
JF-Expert Member
- Jul 7, 2021
- 636
- 1,304
''Kuna watu inawezekana tumejuana kwa kutuona kwa mitandao humu na ndio maana wakati mwingine wanatutukana! Muungwana anapokea kila aina ya matusi na anamshtakia Mungu tu! Safari yetu wengine ilikuwa ndefu sana kwenye tasnia hii. Tumetembea sana kwa miguu, tumekula sana mihogo ya kukaanga barabarani na hii yote katika kusaka habari na kuwahabarisha watu.
Mungu aiweke roho ya marehemu Efrahim Kibonde mahala panapostahili, lakini angekuwa leo yeye angeweza kusema kitu! Ila wale wanaotuona leo mitadaoni tunasafiri huku na kule wanadhani tumeamka tu asubuhi na kukurupuka! Safari ilikuwa ndefu sana na hakuna aliye jua kesho yake.
Mungu mkubwa baada ya miaka 20 tunaendelea kupambana! Tumesota sana, tumesaga lami sana yote kwa kupambana kufika mbele. Mafanikio hayaji kwa kuamka tu asubuhi yanahangaikiwa usiku na mchana! Tupambane. Jioni njema wana wa insta tuliojuana humu.'' @maulidkitenge
Mungu aiweke roho ya marehemu Efrahim Kibonde mahala panapostahili, lakini angekuwa leo yeye angeweza kusema kitu! Ila wale wanaotuona leo mitadaoni tunasafiri huku na kule wanadhani tumeamka tu asubuhi na kukurupuka! Safari ilikuwa ndefu sana na hakuna aliye jua kesho yake.
Mungu mkubwa baada ya miaka 20 tunaendelea kupambana! Tumesota sana, tumesaga lami sana yote kwa kupambana kufika mbele. Mafanikio hayaji kwa kuamka tu asubuhi yanahangaikiwa usiku na mchana! Tupambane. Jioni njema wana wa insta tuliojuana humu.'' @maulidkitenge