Utaratibu wa ada elekezi ulikuwepo hata katika serikali za awamu zilizopita kwa makubaliano ya kwamba hata shule za binafsi zipatiwe ruzuku toka serikalini kufidia pengo.
Tatizo lililokuja kujitokeza ni serikali kutotimiza sera na mpango yake yenyewe kwa kuzipatia ruzuku shule binafsi ili ziweze kujiendesha. Ni lazima tutambue kuwa elimu ndiyo kila kitu na ndiyo msingi wa maendeleo. Na ewekezaji ktk elimu hatuna namna ya kuukwepa kwa gharama yoyote ile. Na kuna usemi huu, kwamba, kama tunadhani elimu ni gharama, basi tujaribu ujinga kwani gharama yake ni kubwa zaidi !!
Na hii iko hata ktk shule za serikali yenyewe kwa maana ya kushindwa kuzihudumia ipasavyo kwa kuzipatia vifaa na fedha za kujiendesha kwa mfumo wa ruzuku.
Serikali yenyewe inachokifanya eti ni kuhakikisha tu walimu wanapata mishahara yao kiduchu, baaasi na kujiona imetekeleza jukumu lake ktk eneo hili. Mengine ni matatizo matupu. Hakuna vitabu, hakuna nyumba za walimu, wazabuni (kwa shule za bweni hawalipwi na mpaka sasa kuna wengine wameishtaki serikali), hakuna maabara na hii mbaya zaidi hasa ktk shule zilizojengwa kati ya mwaka 2005 - 2015 chini ya uongozi wa Kikwete maarufu kama shule za kata. Zingine hata hazina hadhi ya kuitwa shule ni kana kwamba ni mabanda ya kufugia kuku au nguruwe!!
Kwa mtazamo wangu tatizo linaloikabili sekta ya elimu hapa nchini si ada elekezi kwa shule binafsi au "bure" kwa zile za umma. Bali tatizo kubwa ni sera na utashi mbaya wa utekelezaji wa sera na mipango ya serikali. Hapa mchawi ni serikali yenyewe!!
Inawezekana kabisa tukawa na mipango mizuri ktk kutekeleza hili na kusiwe na misigano yoyote kati ya serikali na wamiliki wa shule binafsi ili kuhakikisha kuwa utoaji wa huduma hii hautetereki. Mbona katika sekta ya afya imewezekana na kwa nini katika sekta ya elimu isiwezekane?
Kinachoweza kufanyika ku harmonize hii situation ni kwa serikali kwa mfano kuamua kuwa yenyewe itabeba jukumu la kulipa mishahara ya walimu wote ktk shule za umma na binafsi na pia kila mwaka kuzipatia shule za binafsi sehemu ya fedha za maendeleo kama ruzuku ili wanunue vifaa vya kufundishia na kujifunzia na pia kuongeza miundo mbinu ya majengo, madarasa, nyumba za walimu nk.
Ni kwa njia hii utakuta gharama za elimu za shule binafsi au za mashirika ya dini na asasi za kiraia zinaji - regulate zenyewe na hapa lengo la serikali la utoaji huduma za kijamii kwa wananchi wake kwa usawa linaweza kutimilika pasipo mikwaruzano.
Swali kubwa ni hili, kwamba ni kwa vipi hili litawezekana iwapo hili limeshindikana kwa shule za serikali tu yenyewe kwa miaka nenda miaka rudi na hasa hasa katika uongozi wa serikali ya Jakaya Kikwete ambapo ndipo tuliposhuhudia kuvurugika kwa kiwango kikubwa kwa mfumo wa elimu yetu!?
Na mwisho kwa ushauri tu kwa serikali ya JPM ya awamu ya tano ambayo imeonesha matumaini ya kurekebisha mambo mengi, ni kwamba, usimamizi wa elimu hasa elimu ya juu, vyuo, ufundi na sekondari urejeshwe katika wizara moja mama i.e Wizara ya Elimu na Mafunzo ya ufundi kwa kila kitu kama ilivyokuwa zamani kabla ya Utawala wa Kikwete!!
Hapa ndipo tulipoichaga njia kuu kwani wizara iligawanywa gawanywa kwa lengo tu la kuwapatia nafasi za uongozi watu flani flani kitu ambacho kiliongeza matumizi ya serikali.
Mfano haiwezekani ukawa na waziri anayehusika na elimu TAMISEMI na idara zingine nyingi huko zinazoshughulikia mambo ya elimu wakati tayari tuna wizara husika ya elimu inayojitegemea i.e Wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi yenye taasisi na idara zake zote zinazoshghulikia mambo yale yale!!
Hali hii ilisababisha mgongano wa utekelezaji wa majukumu mengi kati ya Wizara ya Elimu na TAMISEMI na hata mambo mengi kukwama kutekelezeka kwa ukamilifu na ufanisi.
Kwa hiyo Rais wetu Dr John J.P. Magufuli anzia hapa kama tunataka kuirejesha elimu yetu ktk mstari wake. Angalia tulipoangukia na wala sioni sababu yeyote ya kugombana na wawekezaji binafsi katika sekta hii. Tatizo lilikuwa ni serikali yenyewe kwa kutosimama ktk maamuzi yake!!