'Ujinga' wa Ikulu unarudi kwa kasi

'Ujinga' wa Ikulu unarudi kwa kasi

Pole kijana . Mimi ningependa zifutwe kabisa . Maswala ya elimu na afya yalitakiwa yawe chini ya Serikali tuu. Sasa hivi kumekuwa na vilaza wengi maofisini kwasababu ya mashule na vyuo vya kijinga vilivyojazana mitaani .
 
Huyu jamaa inaelekea alikuwa mwizi wa mali za umma, haiwezekani kuona watu wakidhalilika kwa sababu kiwango cha elimu, hivi tunajenga taifa gani, dhulma sasa bc huwezi kufata taratibu za kiserikali na maelekezo yake funga shule yako.
 
Ada hazina uhusiano na ujamaa kwa jinsi unavyotaka kutuaminisha. Uingereza na Marekani ambao ni mabepari wakubwa hawapangi ada lakini wanayo namna ya kuthibiti ili iwe affordable kufuatana na huduma inayotolewa na taasisi za elimu
 
Ada hazina uhusiano na ujamaa kwa jinsi unavyotaka kutuaminisha. Uingereza na Marekani ambao ni mabepari wakubwa hawapangi ada lakini wanayo namna ya kuthibiti ili iwe affordable kufuatana na huduma inayotolewa na taasisi za elimu
Mfumo wao wa soko umekomaa na utawala wa sheria pia umekomaa kuzuia upuuzi huu tunaouona hapa kwetu. Soko linadhibiti mtu hasijipangie tu bei anayotaka, hatapata wateja; lakini utawala wa sheria ni komavu unazuia uonevu usio na msingi. Tunavyo vyombo vya udhibiti, badala ya kutekeleza majukumu yake wankimbikia kupanga bei badala ya kuweka mifumo thabiti! Upangaji wa bei isiyo lingana na matakwa ya soko haitadumu, sana sana itaua huduma hiyo.
 
Hii tabia ya serikali kuanza kuirudisha nchi kwenye mfumo wa ujamaa, ambao ulithibitika kwa vitendo kuwa mfumo wa kijinga, usiotekelezeka, unaogandisha mawazo na unaowafanya viongozi kuwa watawala pekee na siyo viongozi kweli; ni upotofu na udikteta wa hali ya juu. Serikali yoyote inayopanga bei ni serikali ya wajinga, wenye mawazo mgando na madikteta!

Hivi karibuni serikali ya ccm na magufuli wametangaza kuzuia shule binafsi kupandisha ada eti wangoje kile ambacho ikulu walikiita "ada elekezi".

Nasema huu ni ujinga kwa sababu kinachopaswa kuihusu serikali katika shule binafsi ni kuhakikisha wanafuata mtaala wa nchi tu. Tofauti na hapo hakuna kingine. Kumbukeni hakuna kodi yoyote ya mtu iliyotumika kujenga ama kugharamia chochote kwenye hizi shule!

Sasa kwa nini waingiliwe?! Hivi serikali haitupi ujumbe kwamba kwenye shule binafsi ndiko kuliko na elimu bora na kwa hiyo haki ya kupata elimu bora maana yake ni haki ya kusoma kwa bei ndogo kwenye shule binasi?!

Boresheni shule za walipa kodi. Porojo hatutaki!
Hata huko kwa mabepari serikali zipo na Ndio wahusika.
Kinachotakiwa waanze kulipa kodi tu na sio kujipandishia ada holela kwa kisingizio cha kutoa huduma huku faida mlima.
 
Kimsing unapoamua kuweka ada elekezi (ceiling price) ni lazima vigezo ving vizingatowe, aidha katika mfumo wa kibepari bei huachiwa soko liamuwe serikal jukumu lake kubwa ni kuangalia kinachotolewa kama huduma kwa wananchi kiwe kimekidhi vigezo na taratibu zilizowekwa na serikali. Hivyo kwa upande mmojai naona mtoa mada yuko sahihi..
 
Hii ni shule ya sekondari ya Marekani.

Inaitwa Salisbury School.
Shule binafsi.

Ada:

2017 Tuition and Fees

Boarding Day
Tuition $58,100.00. $47,500.00

Hawa wanatoa msaada (Financial Aid), lakini mwisho wa siku ni wafanyabiashara. Wazazi wenye uwezo ndio wanaosomesha hapa. Kama mzazi hana uwezo, anaenda shule za serikali au shule nyingine binafsi zenye ada nafuu zaidi.

source:salusburyschool.org

Hii nyingine ni private school inaitwa Charterhouse ya Uiingereza. Imeanzishwa mwaka 1611 na kuhamia Surrey mwaka 1872. Ada ni Poundi 35500 au $50,000 kwa mwaka.

source:charterhouse.org.uk

All animals are equal, but some animals are born equal than others.
- George Orwell
 
Umeguswa wewe kwenye ilo ndo maana unakuwa mkali kasome masharti ya uanzishwaji wa shule ndo urudi apa.Policy ipo watu walikuwa wakiiby pass.
Kila sector ina bei elekeZi mbona hulalamiki mafuta kupewa bei elekeZi au bse hauko uko?
Basi acha na wenye mafuta wajipangir bei watakavyo tuone kama patakalika apa
Anamaslahi na hizo shule huyo
 
Ubepari ni unyama kwa hiyo ni lazima uwe controlled. price control ni njia mojawapo ya kudhibiti ubepari inayotumiwa na serikali.
 
SI haki kutumia zama za soko huria vibaya watu wafanye wanachotaka kupanga wenyewe kana kwamba hakuna serikali.
 
Porojo hatutaki!

Mwenzetu naona taratibu za serikali hujazikamata, lazima kuwe na taratibu za shule binafsi kuanzishwa na kuendeshwa, huwezi jipangia tu fees kama hakuna sheria, ni utoto na ulimbukeni, naona mzee wa msoga aliwadekeza wengi! Maana mpaka wakina mnukulu wanadai wao wana hela sana 80m/- sio kitu, wengine wanadai 10m/- ni hela ya mboga, nyoka mwenye makengeza kudai bilioni ni visenti tu, wengine kugawa mamilioni ya escrow kama njugu, nchi ilikuwa inaendeshwa kama ngoma za kikwere, wengine mishahara ya kubeba na mikokoteni sababu tu wameombwa kurudi bongo, wengine kuomba kusafiri kwenda nchi za nje zaidi ya mara tano! Kisa posho! #HAPAKAZITU..
 
Hii ni shule ya sekondari ya Marekani. Inaitwa Salisbury School.
Shule binafsi.

Wazazi wanaowasomesha hizo shule ndio wakwepa kodi #panamapapers imetupanua macho, kukimbiza hela kule ili wasilipe kodi eti wawasomesha watoto kwenye hizi overpriced schools! Watu duniani wamewastukia wezi, wakwepa kodi na wala rushwa, mtasoma tu shule za kata popote zilizopo nchini kwenu...
 
Hii ada isipowekewa udhibiti watadai pia wawe na mitaala yao inayoendana na shule hizo,kujitofautisha na shule za umma na itakuwa ni haki yao wakisema wanatoa elimu bora.
 
Madhara ya ugumu wa Maisha uliopo sasa utaanza kuona kwenye term ya Pili mwaka huu Na January mwakani watu wataanza kukimbizia watoto wao shule Za serikali
 
Mwenzetu naona taratibu za serikali hujazikamata, lazima kuwe na taratibu za shule binafsi kuanzishwa na kuendeshwa, huwezi jipangia tu fees kama hakuna sheria, ni utoto na ulimbukeni, naona mzee wa msoga aliwadekeza wengi! Maana mpaka wakina mnukulu wanadai wao wana hela sana 80m/- sio kitu, wengine wanadai 10m/- ni hela ya mboga, nyoka mwenye makengeza kudai bilioni ni visenti tu, wengine kugawa mamilioni ya escrow kama njugu, nchi ilikuwa inaendeshwa kama ngoma za kikwere, wengine mishahara ya kubeba na mikokoteni sababu tu wameombwa kurudi bongo, wengine kuomba kusafiri kwenda nchi za nje zaidi ya mara tano! Kisa posho! #HAPAKAZITU..
KUMBUKA KUNA SHULE ZA BURE! MPELEKE HUKO! OKOA MAPENE!!!
 
Wazazi wanaowasomesha hizo shule ndio wakwepa kodi #panamapapers imetupanua macho, kukimbiza hela kule ili wasilipe kodi eti wawasomesha watoto kwenye hizi overpriced schools! Watu duniani wamewastukia wezi, wakwepa kodi na wala rushwa, mtasoma tu shule za kata popote zilizopo nchini kwenu...

Endelea kuota Ujamaa.

Wenye uwezo watasomesha shule binafsi nchi jirani kama zamani.

Wewe unaona "overpriced", wengine wanaona kawaida tu, wala hawastuki.

Kama huna uwezo, usishindane na wenye uwezo. Hutashinda daima.
 
Back
Top Bottom