Ujinga ni kuamini mambo haya

Ujinga ni kuamini mambo haya

Mk54

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2016
Posts
1,996
Reaction score
3,961
Ujinga ni kuamini kwamba CCM ndio watu sahihi wa kuongoza Taifa la Tanzania; Kwamba, WAPINZANI wataharibu nchi ikiwa watapewa Ridhaa ya kuongoza.

Ujinga ni Kuamini kwamba, yeyote anaejaribu kuonesha nguvu za kuitoa CCM madarakani kwa mujibu wa kisheria na kikatiba kwa kutumia kura za wananchi huyo NI MPINZANI na anahatarisha AMANI YA NCHI.

Ujinga ni kuamini kwamba AMANI ya nchi inaletwa kwa uwepo wa CCM madarakani

Ujinga ni kuamini kwamba Ukiwa MPINZANI mwenye maono tofauti na UTAWALA, wewe ni MSALITI/ BEBERU, UNATUMIKA, MCHOCHEZI, MVUNJIFU AMANI

UJINGA ni kuhubiria AMANI huku haki za MSINGI za wapinzani zikiminywa na Kubakwa

Ujinga ni kuamini kwamba TANZANIA kuna AMANI huku mitandao ya kijamii ikizimwa na kuwa deactivated.

Ujinga ni kuamini kwamba TUNDU anatumwa na MABEBERU kuja kutuharibia AMANI ya nchi; huku, watu 9 wakiuliwa huko ZANZIBAR na vyombo vyetu vya ulinzi na Usalama kwa kuhakikisha wanamchagua Rais wa matakwa yao.

Ujinga ni kuficha Uovu nyuma ya neno AMANI.
Ujinga ni kutokujua kwamba KAZI ya Tanzania Intelligence Security Services ni kuilinda Serikali iliyopo madarakani dhidi ya kupinduliwa au kuondolewa MADARAKANI kinyume na Utaratibu uliowekwa KIKATIBA kama vile Upigaji kura ( TISS ACT, 1996); Halikadhalika, Ujinga ni kuamini kwamba KAZI ya TISS ni kuitetea serikali iliyopo madarakani kuendelea kuwepo madarakani hata wakati wa upigaji kura kikatiba na kisheria

Ujinga ni kuamini kwamba CHADEMA IKISHINDA basi nchi itakuwa na UKABILA WA KIKANDA; Ikama kuna chuki fulani dhidi ya KASKAZINI huku asilimia 75 ya teuzi za awamu ya 5 ni Kanda ya Ziwa.

Ujinga ni watumishi wa UMMA , wanafunzi na wafanyabiashara kushindwa kujua sehemu sahihi ya kuelekeza kura zao ili Kufanya mabadiliko ya kweli na kuleta maslahi mapana ya TAIFA

UJINGA ni kukubali kutatuliwa shida zenu kwenye MIKUTANO ya kampeni kama vile ukosefu wa Nguzo za Umme BABATI hali ya kuwa malipo yalishafanywa takribani mwaka mzima. Inamaana hili lilikuwa halijuiikani? Ujinga ni kushidwa kujua kuwa hawa watu hawapo SERIOUS.

Tumia nafasi ya kubadili karatasi ya kupiga kura kubadili maamuzi yako. Toa Maamuzi sahihi kwa maslahi mapana ya Taifa.
 
Ujinga ni kumuamini Mwanasiasa

Ujinga ni kuamini kuletewa maendeleo ila wewe mwenyewe hujitambui

Ujinga ni kuamini, CCM ikiondoka ndio tutapata haki plus amani ya kweli

Ujinga ni kuamini kuwa chadema ni watu wema na Lisu ametumwa na Mungu

Ujinga ni kuamini Demokrasia ndio mkombozi wetu

Ujinga ni kuamini maandamano na vurugu ndio njia sahihi

Ujinga ni kuamini, bila Wazungu, hatuna maisha


Acha ujinga wako chalii
Tafuta ugali kisha tulia na familia yako
 
Ujinga ni kumuamini Mwanasiasa

Ujinga ni kuamini kuletewa maendeleo ila ww mwenyewe hujitambui...

Ujinga ni kukataa MABADILIKO

Ujinga ni kuwakataa wazungu huku kupeleka maombi ya mikopo na misaada

Ujinga ni kushindwa kufahamu maana ya Demokrasia

Ujinga ni kutokujua kuwa wewe ni MJINGA
UJINGA NI KUSHINDWA KUSOMA NA KUELEWA Mada

Ujinga ni kutatua matatizo ya wananchi kipindi cha kampeni, huku kipindi chote cha utawala wa 5 years hukuweza kuzitatua.

Ujinga ni kuwa MJINGA
 
Ujinga ni kutokujua mazingira halisi ya Mwafrika na Afrika

Ujinga ni kujiona wewe mjuaji ilihali ni Mjinga

Ujinga ni kutokuwa na Shukrani hata ndogo juu ya Utawala

Ujinga ni kuona matusi kwa Kiongozi ndio njia sahihi

Ujinga ni kutofunzwa adabu juu ya wakubwa zako

Ujinga ni kutojua thamani ya damu zinazomwagika kwa ajili ya ujinga wako

Ujinga ni kupambana na mwenye nguvu, ilihali wewe ni kimbao mbao

Ujinga ni kuendelea na ujinga wako, ilihali sisi tunakushangaa
Ujinga ni kukataa MABADILIKO

Ujinga ni kuwakataa wazungu huku kupeleka maombi ya mikopo na misaada..
 
Ujinga ni kumuamini Mwanasiasa

Ujinga ni kuamini kuletewa maendeleo ila ww mwenyewe hujitambui..

Ujinga ni kumuita CHALII mtu usiyemjua

Ujinga ni kuamini tumekuja kutafuta ugali na kutulia na familia mpaka KUFA, huku binadamu wachache wakijilimbikizia mali na binadamu wachache wakitaabika kwa umaskini.

Ujinga ni kushindwa kujua lengo lako la kuwepo duniani. Ujinga ni kujiwekea Limitation za kuishi na kufikiri pasipo kuwaza vizazi vingine

Ujinga ni kuwa MBINAFSI
 
Ujinga ni kutokuja mazingira halisi ya Mwafrika na Afrika

Ujinga ni kujiona ww mjuaji ilihali ni Mjinga...

Ujinga ni kushindwa kuelewa kuwa hakuna Mwenye nguvu juu ya MGONGO WA ARDHI isipokuwa MUUMBA

UJINGA ni kushindwa kuelewa kuwa hata huyo unaemuita ana nguvu ni MAVUMBI NA CHAKULA CHA MCHWA

UJINGA ni kushindwa kuamka kutoka USINGIZI WA AKILI
 
Ujinga ni kufahamu sisi soote tumeumbwa kuwa Viongozi au Matajiri

Ujinga ni kuamini usiku na mchana vinafanana

Ujinga ni kuamini kuwa sisi tumeumbwa ili tumpe fulani ulaji

Ujinga ni kuamini, kila kinachotoka mdomo mwa mtu usiemjua chimbuko lake kisha ukaamini maneno yake

Ujinga ni kutothamini mawazo chanya na kukumbatia mawazo hasi

Ujinga ni kuona yote yaliyofanywa na Chama Tawala ni makosa, ila yatayofanywa na hao ..... ndio sahihi

Ujinga ni kukumbatia ndoto, ukatukana uhalisia

Ujinga ni kuendelea na Ujinga wako, huku ukiwa na ndoto za kuokota hela bila kufanya kazi kwa bidiii

Ujinga ni kusahau asili ya Wazungu na maono yao dhidi ya Waafrika

Ujinga ni kuendelea kuandika Ujinga wako

Ujinga ni kupoteza muda na mjinga wewe

Samahani
Mimi sitaki kuwa Mjinga Chief
Mjinga hubaki na ujinga wake, naomba ubaki hivyohivyo

Mpuuzi mmoja wewe
Ujinga ni kumuita CHALII mtu usiyemjua

Ujinga ni kuamini tumekuja kutafuta ugali na kutulia na familia mpaka KUFA, huku binadamu wachache wakijilimbikizia mali na binadamu wachache wakitaabika kwa umaskini.

Ujinga ni kushindwa kujua lengo lako la kuwepo duniani. Ujinga ni kujiwekea Limitation za kuishi na kufikiri pasipo kuwaza vizazi vingine

Ujinga ni kuwa MBINAFSI
 
Back
Top Bottom