Ujinga ni kuamini mambo haya

Ujinga ni kuamini mambo haya

Hili ni ndilo tatizo la msingi na linatokana na na umasikini na mfumo wa elimu usiowaandaa vijana ku-reason kwa ufasaha. Wengi wao ni waoga, hawajiamini na wamejaa hofu kubwa. Suluhisho litapatikana pale itakapoongezeka idadi ya walioelimika kwa ufasaha, kuongezeka kwa tabaka lenye kujimudu kiuchumi na waliojiajiri na wenye exposure.

Umasikini na elimu duni ndiyo chanzo kikuu cha hali hii. Kote duniani watawala upenda kukandamiza na kutumia hila na nguvu kuendelea kutawala. Kwa hiyo km watawaliwa hawatabaini na kusimamia maamuzi yao kwa kuchagua watu ambao walau wata-balance maslahi ya pande zote 2, jamii hiyo itaendelea kuteseka.

Sent from my SM-J530F using JamiiForums mobile app

Ujinga ni wapinzani kuendelea kukubali kushiriki Uchaguzi kwa tume ya NEC na ZEC.
 
Ujinga ni kumuamini Mwanasiasa

Ujinga ni kuamini kuletewa maendeleo ila wewe mwenyewe hujitambui

Ujinga ni kuamini, CCM ikiondoka ndio tutapata haki plus amani ya kweli

Ujinga ni kuamini kuwa chadema ni watu wema na Lisu ametumwa na Mungu

Ujinga ni kuamini Demokrasia ndio mkombozi wetu

Ujinga ni kuamini maandamano na vurugu ndio njia sahihi

Ujinga ni kuamini, bila Wazungu, hatuna maisha


Acha ujinga wako chalii
Tafuta ugali kisha tulia na familia yako
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
 
Nchi zote duniani, Ma DG wa taasisi za usalama wanateuliwa na Rais, kwa nchi zenye demokrasia makink hawana ujinga wa kama wa bongo.

Ninachokiona tatizo ni Kitengo cha ulinzi wa Rais kuwa chini ya TISS.

Ilitakiwa hiki kitengo kiwe kinajitegemea kama secret service na TISS inakua kama MI6.

Kwa mfumo huu, ni ngumu ccm kuondoka madarakani.

Na upinzani inabidi waje na mbinu nyingine nje ya uchaguzi

Kwa kura za Masanduku na kura za Kusomeana kwa makaratasi. Bashiri kuwa CCM itatawala FOREVER, swali la msingi ni how long does forever last ?
 
Back
Top Bottom