Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 22,606
- 29,754
Unapoelekea Mbagala kupitia barabara ya Kilwa utaona ujenzi unavyoendelea kwa kujenga pia njia ya mwendokasi, kuna daraja la juu pale Uhasibu na kwa kweli inapendeza haswaa.
Mkandarasi anajitahidi kukimbizana na deadline ya kazi. Lakini kuna tatizo kubwa la vumbi litokanalo na kifusi kitumikacho kwenye ujenzi huo
Masaa yote kumekuwa na foleni kibwa lakini vumbi kama tupo jangwani. Watu wengi wameanza kuugua vifua na mafua ambapo inawezekana wengi wakafa kwa hofu wakidhani wameambukizwa CORONA.
Mshauri mwelekezi anapaswa kukagua kama vigezo kuhusu afya na usalama wa wanaoitumia sasa na wanaoishi pembezoni umezingatiwa.
Kuhusu foleni nawasihi wahusika wafungue njia mbadala zitakazopunguza adha za foleni kwa wanatumiaji.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke tusaidie kwenye hili
Mkandarasi anajitahidi kukimbizana na deadline ya kazi. Lakini kuna tatizo kubwa la vumbi litokanalo na kifusi kitumikacho kwenye ujenzi huo
Masaa yote kumekuwa na foleni kibwa lakini vumbi kama tupo jangwani. Watu wengi wameanza kuugua vifua na mafua ambapo inawezekana wengi wakafa kwa hofu wakidhani wameambukizwa CORONA.
Mshauri mwelekezi anapaswa kukagua kama vigezo kuhusu afya na usalama wa wanaoitumia sasa na wanaoishi pembezoni umezingatiwa.
Kuhusu foleni nawasihi wahusika wafungue njia mbadala zitakazopunguza adha za foleni kwa wanatumiaji.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke tusaidie kwenye hili