Mafia Island Boy
Member
- Apr 1, 2017
- 16
- 25
Picha: Akili Mnemba
Sheria ya Mafuta Na. 21 ya mwaka 2015 inaipa nguvu EWURA, kusimamia shughuli za mkondo wa kati na mkondo wa chini wa sekta ya mafuta ya petroli. Kifungu cha 126 (1) cha sheria hiyo kinamtaka mtu yoyote anayetaka kujenga miundombinu ya mafuta kuomba kibali cha ujenzi kutoka EWURA.
Aidha, Kifungu cha 131 (1) cha sheria hiyo kinawataka wote wanaojihusisha na sekta tajwa kuwa na leseni iliyotolewa na EWURA.
Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA), imekuwa mara kwa mara ikisisitiza kanuni namba 27 ya usimamizi wa biashara za vituo vya mafuta ya mwaka 2022 kama ilivyochapishwa kwenye gazeti la serikali Na. 150.
Kanuni za mipango miji na Sheria ya Usimamizi wa Mazingira, 2004 inakataza vituo vya mafuta kuwa karibu na makazi ya watu.
Kwa mujibu wa utaratibu wa mipango miji, umbali wa kituo hadi kituo ni mita 200.
Hata hivyo, kumekuwa na ujenzi holela wa vituo vya mafuta tena karibu na makazi hali inayohatarisha usalama wa wananchi endapo moto utalipuka.
Ujenzi huo holela umeonekana katikabarabara ya Tandale/ Sinza, kuanzia Tandale SweetyKona utaanza na kituo cha mafuta cha ATN, upande wa kushoto ukiwa unatoka Sinza kuelekea Magomeni, mbele kidogo hatua upande wa kulia utakutana na kituo cha Victori (ushahidi upo kwenye video chini).
Ukisogea mbele Tandale kwa Mtogole eneo la Chama utakutana na kituo cha mafuta cha Olympic upande wa kulia hata chache mbele upande wa kushoto utakutana na kituo cha KSK Oil, ukisogea mbele mita 30 karibu na Tandale Kwa Tumbo upande wa kulia kuna kituo cha kujaza gesi asilia upande wa kushoto kituo cha OilCom, barabara hiyo hiyo eneo la Magomeni kwa Bibi Nyau utakutana na kituo cha Total Energy.
Umbali kutoka Magombeni Kanisani mpaka kufikia Sinza Madukani ni Kilometa nne, lakini kuna vituo vitano vya mafuta.
Kanuni hiyo inawataka wamiliki wote kuhakikisha wanachukua tahadhari juu usalama wa afya, mali na mazingira ili kuepusha milipuko.
Mwandishi wa habari alizungumza na baadhi ya wakazi wa maeneo ya, amesema kuwa licha ya kuwa biashara imechangia ukuaji wa eneo lao lakini wanawasiwasi wa usalama wao eneo ikitokea mlipuko wa moto.
Mkazi mmoja wa Tandale Chama aliyezungumza kwa sharti ya kutotajwa jina lake, alisema, “hebu fikiria duka langu lipo karibu na hiki kituo cha mafuta siku ikitokea la kutokea tunalipuka sote sio mimi hata makazi ya wananchi yapo karibu kabisa.
“Hivi vituo wakati vinajengwa wananchi hatujashirikishwa sisi tumeona tu ujenzi hatimaye kituo na isitoshe hivi vituo vimetufuata sisi,” alisema.
Ali Kipulizo mkazi wa Mtongani, wilayani Temeke, alisema anastaajabishwa kuona kila uchao vituo vya mafuta vinajengwa kwa wingi katika eneo moja.
“Najiuliza mimi kwanini wajenge kwa mlundikano ikwa kuna sehemu huko mikoani wanahitaji huduma hizi kwanini wanatufanya tuishi kwa hofu,” alisema.
Oktoba 2012 Policy Forum na Chama cha wanasheria wa Mazingira (LEAT) walipendekeza wakati taifa likielekea kwenye katiba mpya kipekee yaingize ibara zitakazosisitiza suala la mazingira wananchi kuingi kwenye mazingira salama kuwa moja ya haki ya msingi kwenye katiba.
PrayGod Sallema, Mwanasheria pia mwanaharakati wa mazingira amemwambia Mwandishi wa habari kuwa uholela wa ujenzi wa vituo vya mafuta ni bomu ambalo likilikupuka hatutakuwa na wa kumlaumu.
“Tazama hii njia ya Tandale humalizi hata nusu kiwanja pale chama kuelekea kwa Tumbo unakutana na takribani vituo vitano vya mafuta kwa pamoja lakini ajabu makazi ya watu yapo karibu yaani nyumba za watu na vituo vya mafuta zipo karibukaribu kiasi ambacho moto ukiwaka kwanza vile vituo vya mafuta vinne pale vitakuwa vikipokezana kisha kwenye makazi ya watu yaani kutawaka moto ambao hata fire watashindwa kujua waanzie wapi kuzima,” alisema Sallema.
Alisema kuwa mambo kama hayo hayatokie bila rushwa.
“Hapa ni wazi kuna mashaka kwamba kuna mazingira ya rushwa isingekuwa rushwa hakuna mtu angekubali kutoa vibali hivyo au kama sio rushwa basi ni uzembe watafakari upya.”