Clever505
JF-Expert Member
- Jul 27, 2020
- 2,023
- 3,037
Unaposema Yohana kazaliwa na dini, unamaanisha roho mtakatifu ndo dini?Wewe uwezo wako wa kuelewa ni mdogo sana lakini kwakuwa nimeamua nikufundishe acha tu niendelee kufundisha
Hilo andiko la Luka nilikuonyesha Baada ya wewe kusema binadamu hatuzaliwi na dini Yani ukipinga andiko la Quran kuwa watu wote wanazaliwa wakiwa waislam
Hilo andiko la Luka linasema Yohana alijazwa roho mtakatifu tokea akiwa tumboni Kwa mama yake kwahiyo Yahona anazaliwa akiwa na roho mtakatifu
Nikakwambia hili andiko linathibisha kuwa Yohana amezaliwa akiwa na dini maana haiwezekani Yohana azaliwe huku roho mtakatifu akiwa ndani yake alafu awe mpagani
Swali likabaki Yohana amezaliwa akiwa na dini JE hiyo dini ni ipi ?
Mimi nikakwambia hiyo Dini ni uislam ila wewe kama unabisha weka ushahidi wako kuwa Yohana alikuwa mkristo kama wewe
Huo ushahidi haujaweka na sio wewe tu wakusanyike wachungaji wote Duniani hawawezi kuwa na ushahidi kuwa dini ya Yohana ni ukristo
Labda utajiuliza kwanini nimetoa andiko la Luka?
Nimetoa hilo andiko Kwa sababu lipo katika kitabu ambacho wewe unakiamini na hiyo story hapo ya Zakaria na mwanawe Yohana haijachakachuliwa sana inafanana na iliyopo ndani ya Quran
Ndani ya Quran Yohana anaitwa Yahaya
Quran 3:38
Pale pale Zakariya akamwomba Mola wake Mlezi, akasema: Mola wangu Mlezi! Nipe kutoka kwako uzao mwema. Wewe ndiye unaye sikia maombi.
Quran 3:39
Alipo kuwa kasimama chumbani akisali, Malaika kamnadia: Hakika Mwenyezi Mungu anakubashiria Yahya, ataye kuwa mwenye kusadikisha neno litokalo kwa Mwenyezi Mungu, na ni bwana na mt'awa na Nabii kwa watu wema.
Nabii Yohana pamoja na baba yake nabii Zakaria wote walikuwa waislam
Kama wewe unao ushahidi kuwa walikuwa wagalatia kama wewe weka hapa tuuone
Kitu ambacho unaharibu ni kuunganisha Aya za Biblia takatifu na Quran. Achana na hiyo kitu.
Swali langu ni kwamba roho mtakatifu ndo dini?
Waislam mnasema watu wote wanazaliwa na dini, hilo fundisho halipo kwenye Biblia. Unajaribu kuonyesha hiyo aya inayomuhusu Yohana kujazwa roho mtakatifu ikuunge mkono kwenye imani yako ya watu kuzaliwa na dini. Mkuu hebu acha Imani za ajabu, mtu anazaliwaje na dini? Roho mtakatifu sio dini. Kama ni dini hebu nionyeshe ambapo kwenye Biblia panaonyesha kila mmoja anazaliwa akiwa amejazwa roho mtakatifu....
Ifike hatua usilazimishe Imani yako ithibitishwe na Aya za Biblia. Ikiwa dini yako inafundisha mnazaliwa mkiwa waislam usitake iwe lazima na sisi wakristo tuamini hilo.