Uingereza yahalalisha ndoa za jinsia moja

Uingereza yahalalisha ndoa za jinsia moja

Status
Not open for further replies.

EMT

Platinum Member
Joined
Jan 13, 2010
Posts
14,477
Reaction score
15,347
Uingereza imehalalisha kisheria ndoa za jinsia moja baada ya mswada uliopitishwa na bunge lao jana kuwa sheria kusainiwa na Malkia leo Jumatano saa tisa na dakika sita mchana kwa saa za Uingereza.

Sheria hiyo inajulikana kama Marriage (Same Sex Couples) Act 2013. Ndoa za jinsia moja zitaanza kufungishwa rasmi kuanzia katikati ya mwaka 2014.

Sheria hiyo mpya inaungwa mkono na viongozi wa vyama vyote vya siasa nchini humo akiwemo Waziri Mkuu wa sasa David Cameron. Cameron alipata upinzani mkali kutoka kwa baadhi ya wabunge wa chama chake cha Conservative.

Hata hivyo, mswada huo ulipitishwa kiulaini kabisa na kuwa sheria baada ya kuungwa mkono na wabunge wengi wa vyama vya Labour na Liberal Democrats.

Sheria hiyo inaruhusu mpaka ndoa za kidini za jinsia moja, lakini hailazimishi madhehebu ya dini kufungisha ndoa hizo ndani ya madhabahu yao. Pia makanisa, misikiti, nk hayatashtakiwa mahakamani kwa kukataa kuwafungisha ndoa watu wanaotaka kufunga ndoa ya kidini.

Church of England ni moja ya makundi ya kidini yaliyopinga ndoa za jinsia moja.
 
Good for them.

Kama watu wazima wa jinsia moja wanapendana na wanataka kufunga pingu za maisha, rukhsa. Ni maisha yao.
 
Utashi wa mwanadamu unazidi kusonga mbele..! Naona ni uamuzi wa busara, tuwache wanacuf waishi wapendavyo ingawa sikubaliani na sheria hii kulazimisha mistikiti na makanisa kufungisha ndo hizi..!
 
Hii ni dalili kuwa huenda miaka hamsini ijayo ikawa imesambaa duniani kote. Balaa...
 
Utashi wa mwanadamu unazidi kusonga mbele..! Naona ni uamuzi wa busara, tuwache wanacuf waishi wapendavyo ingawa sikubaliani na sheria hii kulazimisha mistikiti na makanisa kufungisha ndo hizi..!

Sheria ipi inalazimisha misikiti na makanisa kufungisha hizo ndoa?
 
Uingereza imehalalisha kisheria ndoa za jinsia moja baada ya mswada uliopitishwa na bunge lao jana kuwa sheria kusainiwa na Malkia leo Jumatano saa tisa na dakika sita mchana kwa saa za Uingereza.

Sheria hiyo inajulikana kama Marriage (Same Sex Couples) Act 2013. Ndoa za jinsia moja zitaanza kufungishwa rasmi kuanzia katikati ya mwaka 2014.

Sheria hiyo mpya inaungwa mkono na viongozi wa vyama vyote vya siasa nchini humo akiwemo Waziri Mkuu wa sasa David Cameron. Cameron alipata upinzani mkali kutoka kwa baadhi ya wabunge wa chama chake cha Conservative.

Hata hivyo, mswada huo ulipitishwa kiulaini kabisa na kuwa sheria baada ya kuungwa mkono na wabunge wengi wa vyama vya Labour na Liberal Democrats.

Sheria hiyo inaruhusu mpaka ndoa za kidini za jinsia moja, lakini hailazimishi madhehebu ya dini kufungisha ndoa hizo ndani ya madhabahu yao. Pia makanisa, misikiti, nk hayatashtakiwa mahakamani kwa kukataa kuwafungisha ndoa watu wanaotaka kufunga ndoa ya kidini.

Church of England ni moja ya makundi ya kidini yaliyopinga ndoa za jinsia moja.

Waingereza uzinzi ni jadi yao. kanisa la Anglikan lilitokana na King wao kutaka kuoa mke mwingine (baada ya kutengna na wa ndoa) wakati kanisa haliruhusu kuoa mke mwingine kabla ya wa kwanza KUFA and only KUFA. Akaona amkane Papa , akwa mkuu wa kanisa alilolitenga kutoka Roma(???). Uzinzi ni wao tu!
 
Kwa uzi huu tutawatambua mashoga wa hapa kwetu. Nimeanza kuona dalili...
 
Waingereza uzinzi ni jadi yao. kanisa la Anglikan lilitokana na King wao kutaka kuoa mke mwingine (baada ya kutengna na wa ndoa) wakati kanisa haliruhusu kuoa mke mwingine kabla ya wa kwanza KUFA and only KUFA. Akaona amkane Papa , akwa mkuu wa kanisa alilolitenga kutoka Roma(???). Uzinzi ni wao tu!

Kwa hiyo hii wala haitushangazi kabisa....
 
Mwisho wa dunia sasa umekaribia kuliko tunavyofikiri.

Warumi1:24- Kwa ajili ya hayo Mungu aliwaacha katika tamaa za mioyo yao, waufuate uchafu, hata wakavunjiana heshima miili yao.

25-Kwa maana waliibadili kweli ya Mungu kuwa uongo, wakakisujudia kiumbe na kukiabudu badala ya Muumba anayehimidiwa milele. Amina.
26-Hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili;

27-wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao.
28-Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa. 29-Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya; wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na hadaa; watu wa nia mbaya, wenye kusengenya, 30-wenye kusingizia, wenye kumchukia Mungu, wenye jeuri, wenye kutakabari, wenye majivuno, wenye kutunga mabaya, wasiowatii wazazi wao, 31-wasio na ufahamu, wenye kuvunja maagano, wasiopenda jamaa zao, wasio na rehema; 32-ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali

Yehoshua Hamochiah
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom