Uimara wa CHADEMA Umethibitika kwa sakata la Slaa

Uimara wa CHADEMA Umethibitika kwa sakata la Slaa

tuna hitaji mabadiliko mwaka huu ya kuiondoa ccm km Dr slaa anataka majaribio na aende zake
 
Jamani mjue kuwa yule ni Padre do kaweka mfungo na kajifungia. Kuna ule mfungo wenyewe wakatoliki huwa ukifungu huruhusiwi kuongea na mtu
 
Kwa jinsi mnavyomponda bora aondoke tu maana hata akirudi ofisini hamtamwamini.
 
Suala lolote linaloshirikisha imani, ni suala nyeti. Ila lina hatari moja huenda hicho kinacho aminiwa kikawa ni kweli au la.

Suala la msimamo wa Dr. Slaa limetawaliwa na imani, wapo wanaoamini bado yupo kwenye harakati na wengine ni tofauti.

Uhakika wa suala hili utapatikana punde tu Dr. Slaa atakapotoa kauli yake na sio vinginevyo.

Kwa takribani juma moja sasa tumeona na kusikia dhahania nyingi sana kuhusiana na suala hilo.

Wasiwasi wangu hao wanaoamini amejiondosha kwenye taasisi na harakati za siasa watakuwa katika hali gani ikiwa kauli yake itakuwa tofauti.

Pia wanao amini ataendelea kuwemo katika ulingo wa vita baada ya kipindi fulani, pia nao watakuwa katika hali gani ikiwa tofauti.

Vilevile wanao amini atajitoa taasisi moja na kujiunga na taasisi nyingine ama taasisi hasimu nao watakuwa katika hali gani ikiwa tofauti na imani yao...

Kwa upande wetu sisi watazamaji tu, tunasubiri kauli na msimamo wa Dr. Slaa ndio tutaweza kuchangia maono yetu.....

Kitu pekee ambacho sijafurahishwa nacho ni kuona watu wanatumia lugha za matusi, kejeri wao kwa wao ama kumkejeri Dr. Slaa badala ya kuchangia hoja za msingi katika uzi huu....
 
Cdm c imara kama unavyodhani, kwanza kwa kuungana na vyama vingine tuu hiyo ni sababu kuwa haina nguvu , kama haitoshi kumtegemea kada wa ccm kuwa ndio mgombea ngazi ya urais hiyo ni sababu ingine tena kudhihirisha udhaifu , sababu ya tatu ni kitendo cha kuweka sharti la kupokea kiasi cha fedha ili kuachia nafasi ya mgombea wa urais huo ni udhaifu mkubwa zaidi, kwa ujumla cdm na upinzani bado ni wachanga sana,. Na udhaifu wa kuamini kuwa wingi wa washabiki cyo ukubwa wa chama kwani kwa siasa watu hao leo wanaweza kukuunga ww na kesho wakamuunga mwingine.

Wewe ni Gamba! Potelea mbali! CDM imara sasa kuliko huko awali!
 
mm pia nilimuamini Dr. Slaa kama kasusa basi kila la heri vita yetu cyo mtu vita yetu ni mfumo mmbaya wa ccm kwa hiyo yy kama anataka kuisaidia ccm sawa tu

Katika makubaliano ya kuunda ukawa lengo kubwa lilikuwa kumsimamisha mgombea uraisi mmoja na kuungwa mkono na wanachama wao wote kuitoa ccm na mfumo wao m-baya madarakani kwanza mengine yangeangaliwa baadae. Hivyo hivyo kwa wabunge na madiwani. Kenya walifanya hivyo na wakashinda. Chadema na hata Slaa wanaamini katika muungano kupata ushindi na pia wanaamini bila ccm kutoka madarakani hakuna maendeleo ya nchi na mwananchi mmoja mmoja. Vyama vyote kupitia halimashauri kuu zao waliwachagua wagombea uraisi wao ambao miongoni mwao angepatikana mmoja ambae angeteuliwa kushindanishwa na ccm na vyama vingine vya upinzani ambavyo vitasimamisha wagombea uraisi wao.

Edward Lowassa hatimae akawa ameshaomba kujiunga chadema na halimashauri kuu ikaitishwa na kuelezwa juu ya ujio wa Lowassa na wao baada ya kuamini hakika kwa nguvu kubwa aliyo nayo kwa wananchi na wafuasi wengi anaoingia nao kwenye chama anaweza kupata ushindi kwa ngazi ya uraisi wakamteua kubeba bendera hiyo.Kumbuka hapo ni baada ya chadema kupata ridhaa ya vyama washirika kuridhia chadema kumsimamisha mgombea uraisi na cuf visiwani kutoa mgombea mwenza ambae kwanza angepaswa kujiunga chadema kukidhi sharti la kikatiba.Katika kikao cha halimashauri kuu ya chadema kilichomteua Lowassa Slaa alikuwepo. Kilichofuata ni Lowassa kukaribishwa chadema na viongozi wakuu wa vyama washirika wakahudhuria wote ila Slaa hakutokea na Lowassa kukabidhiwa kadi ya chadema na m/kiti na siku hiyo mh. Mbowe alitoa hotuba nzuri mno ambayo haiwezi kufananishwa na ya kiongozi yeyote aliepo na waliopita labda mwl. Nyerere peke yake. Siku iliyofuata Lowassa alienda kuchukua fomu ya kugombea uraisi makao makuu ya chadema na kukabidhiwa na m/kiti Mbowe. Kama kawaida Slaa hakuwepo.

Tumesoma michango mingi humu jamvini mingine ikidai waandishi kuwasiliana na Slaa mwenyewe na majibu ni kuwa kaamua kupumzika siasa. Mingine ikidai bado mimi nimo lakini wakati huo akiwa kwake.Tumeona hata baadhi ya tweets za mkewe akilalamika mumewe hakutendewa haki kutopewa nafasi ya kugombea uraisi yeye.Waandishi wengine walidai walipomfuata Slaa kwake waliambulia matusi kwenye simu toka kwa mkewe Slaa. Mchango wa juzi ukadai Slaa kahama kwake hayupo na ofisini hajaonekana. Pia niliona bandiko lake lenye picha yake humu jf akionya watu kuendelea kumsema vibaya kwa yanayotokea. Mwingine kasema Slaa kaomba ushauri kwa kiongozi wa kanisa lake na kuambiwa ni vizuri apumzike siasa. Kwamba Vatican wameahidi akapumzike Italia na mkewe kwa miaka mitano baadae arudi kijijini kwao. Kama yote yana ukweli tutegemee arudishe kadi na mali nyingine alizo nazo kwenye chama na kuendelea na mipango yake.

Ikiwa atafanya hivyo kwa kisingizio chochote cha kutolamba anachoita matapishi ya Lowassa atakuwa sio mkweli kama anavyotaka kutuaminisha na wafuasi wake wachache ambao hajagundua ni mamluki ya ccm. Kwanza naamini alimsikia vizuri Lowassa alivyojibu swali la mwandishi wa habari kuhusu richmond. Alisema yeye hahusiki kwa njia yoyote kwani amri ilitoka juu kupitia msemaji wake wa ikulu kwamba mkataba usisitishwe. Ulikuja kusitishwa aliporejea nchini.Nae Slaa kwa umri wake ameshashuhudia shuhuda nyingi za waliokuwa waovu sana kwenye jamii kubadilika na leo ni wachungaji na maaskofu wa makanisa.Na kwa ukweli kabisa kwenye richmond kamati zote mbili ya takukuru na ya Mwakyembe walikiri walichoona pale ni taratibu kukiukwa wala hakuna senti ya serikali ililipwa kwa kampuni ile maana haikuwahi kuiuzia hata unit moja ya umeme. Ufisadi hapo upo wapi mbona miaka yote minane hawatamki kiwango cha hasara kama ufisadi mwingine?Aliyemeza matapishi endapo atajiuzulu atakuwa Slaa mwenyew kwa kuwasaliti wananchi,viongozi wenzie wote wa vyama vilivyounda ukawa kwani atakuwa ameliacha lengo walilokubaliana la kuiondoa ccm kwanza mengine yakafuata na yeye kufuata matamanio aliyokuwa nayo moyoni mwake.Tunauelewa ukaribu wa kanisa katoliki na ikulu hivyo kwenda kuomba ushauri huko anazidi kutuona hatunazo. Kwao kiongozi mkristo lazima awe mkatoliki na tayari wanae tinga tinga huko ccm. Sasa uvumilivu wa kisiasa aliokuwa anauhubiri kila siku uko wapi?Awe na ngozi ngumu. Mwisho ukawa na chadema ni taasisi zitaendelea kuwepo tu.
 
uimara wa kulikumbatia fisadi nakuwaona watu waadilifu hawafai
 
Chadema ni chama chenye intelijensia ya hali ya juu,ndiyo maana uzushi unazidi kuzagaa lakini hakuna aliyepata taarifa sahihi kuhusu Dr.slaa. Nahuu ndiyo mkakati wa chadema kuchezea akili za wanafiki wote wa chadema.
 
11825237_1477379572583655_852364606187970497_n.jpg
 
Chadema ya leo,siyo ya 1992,na hakuna mkubwa kuliko chama.Hata aondoke Dr Slaa,Mbowe au Mzee Mtei,Chadema shall overcome.Hii ni taasisi,itakuwa kama alivyoondoka Zitto tu
 
Binafsi nampenda dr lakin kwa hatua tulipofikia hakutakiwa kubehave vile hii ni safari ya ukombozi tunahitaji kila silaaa muhimu kuangamiza adui,kurudi nyuma ktk wakati huu,si tu ubinafsj bali nikusaliti wanamapinduzi wote duniani na waliotangulia mbele ya haki
 
Hivi kuna siku Dr kawambia amesaliti chama. Hatakapo jitokeza live utaujua ukweli msianze kuwa na hofu bila ya evidence yoyote. Chadema iko imara kila pande
 
Ukiona kobe kainama jua anatunga sheria.
 
jitahidini kuweza kuchanganua mambo vizuri mbowe kadhirisha wazi kua ana power kubwa kwenye chama na isitoshe tunajua mwanzilishi wa chama baba mkwe wake........dr slaa anacho kifanya ni sahihi kabisa...........mlio kua mnamwita mwizi miaka zaidi ya kumi leo kawa msafi na mnamsimamisha kugombea........tafakari kwa kina hapo
 
Dr yupo na ataendelea kuwepo, wanaozusha kazi kwenu
 
Back
Top Bottom