Uhusiano wa Franco na Mobutu

Mimi huwa zinanichanganya hizi Congo mbili, Brazzaville na Congo Kinshasa, hebu nipeni itofauti hapo, hawa wanamuziki kina Koffi, Werrason n.k wanaishi Congo ipi? Kabila anaongoza Congo ipi? Congo ipi ni maarufu kuliko nyingine na kwa nini?
wanamzk hao woote n wa Congo DRC
brazavile haina exposure kuzid DRC
 
Mobutu alifuja hela za nchi mno
hadi anakufa alikuwa na Pesa cash dola billion 3 za marekan achana na asset nyingne
hadi juz juz serikali ya uswiss ambalo kulikuwa na akaunt ya Mobutu waliamua kuwagawia hizo hela familia ya mobutu
 
mkuu ID yako imenikumbusha mwanamzk wa okk jazz alieitwa simaro lutumba masiya
alicharaza wimbo matata unaitwa Maya
Ile album ya Maya wenyewe wanaita "Album des albums" ilipigwa na OK Jazz tawi la Kinshasa wakati Franco na OK Jazz bendi kubwa wako ulaya. Kitu ile ilipotua mikononi mwa Franco ilibidi aite bendi nzima waisikilize na akawaambia anataka wajitume. Simaro ana nyimbo nyingi kali-bahati mbaya au nzuri-ni mtu muungwana sana, hajitutumui lakini vigongo vyake Luambo alivikubali hadi kumpa Chef D'Orchestre, Vice President na baada ya kufariki Franco akawa President of OK Jazz na Vice wake akiwa Josky Kiambukuta. Wanamuziki wenzake walimheshimu sana ndio maana familia ya Luambo ilipo mvua u-president, yeye aliamua kutoak OK Jazz na wanamuziki wote waliobaki wakaiacha bendi hapo hapo pamoja na Josky ambae familia walitaka awe President. Leo hii anapiga 80 years na anastaafu muziki baada ya miaka 60.
 
hebu nifafanulie kidgo mkuu kuhusu sintofaham hiyo please
 
mke wa kwanza wa Mobutu aliejulikana kama Marie Antoine alifark mwaka 1977 kutokana na kipigo kutoka kwa Mobutu alikimbizwa hospital nchini uswiss lkn alifariki
watoto wawili wa Mobutu walikufa kwa ngoma
mmoja mwaka 1994(huyu ndie mtoto wake wa kwanza alizaliwa 1955)
meingine anaitwa kongulu Mobutu alifariki mjini Monaco 1998 huyu alizaliwa 1975 na alikuwa askari ktk kikosi cha kumlinda Mobutu alikuwa anabaka msichana yoyote amtakae hakukuwa na wa kumuuliza,akiamua anaenda shule anatafuta mwanafunz yyote anaenda kumla,mwishow ukimwi ulimmaliza
 
aisee story nzuri sana hii
mzee simaro lutumba yy hakuangaika na sketi ndio maana ukimwi ulimuepuka
Franco aliwacharaza mademu mno
Sam mangwama pia nampenda mno sijui yupo wapi now
 
[emoji119] [emoji119]
 
Kama kumbukumbu zangu ziko vizuri ni kwamba UKIMWI uliingia Afrika miaka ya 80, sasa ikawaje UKIMWI huo huo ambao tunambiwa na watalaam huchukua miaka nane tangu kuambukizwa ndo dalili zake zionekane ukagharimu maisha ya Franco ndani ya miaka hiyo ya 80..Niko tayari kurekebishwa..Vinginevyo shukrani zimwendee aliyetuletea historia hii na pia wale wote ambao hawakusita kuchangia pale ambapo waliona wana cha kuchangia na wale pia waliouliza maswali yaliyopelekea historia hii kuongezewa nyama.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…