Uhusiano wa Franco na Mobutu

Uhusiano wa Franco na Mobutu

Basi Nenda

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2017
Posts
20,789
Reaction score
47,984
Wakuu habarini za muda huu,

mobutu-sese-seko-the-president-of-zaire-26-may-1989-poses-for-during-picture-id51525372.jpeg

arrival-of-president-mobutu-and-his-wife-with-his-personal-guards-for-picture-id541790488.jpeg


Zimeanzishwa thread nyingi kuhusu Franco na Mobutu, historia ya Mobutu imeelezwa na ya Franco pia, leo naleta historia ya uhusiano wa watu hawa wenye majina makubwa Africa na ulimwenguni, mwanasiasa na gwiji la muziki.

arrival-of-president-mobutu-and-his-wife-with-his-personal-guards-for-picture-id541790488.jpeg

zaire-president-mobutu-prepares-to-meet-with-french-president-picture-id583022796.jpeg


KUNYONGWA KWA KINA EVARISTE KIMBA

Mnamo mwaka 1965 Mobutu anakua rais wa Zaire na kuagiza kunyongwa kwa watu zaidi ya 6 wengi wao wakiwa mawaziri wa serikali aliyoipindua katika eneo la matonge jijini Leopold Ville (Kinshasa) kwa kosa la uhaini, mamilioni ya watu wanashuhudia hadharani, mmoja wao ni Franco, baada ya hapo Franco akatunga nyimbo iitwayo Luvumbu Ndoki (Luvumbu mchawi) hii ni hadithi ya kikongo kuhusu Mfalme Luvumbu aliyeuwa ndugu zake wa karibu kwa ajili ya kujinufaisha.

Nyimbo hii inaonekana na mamlaka kama dhihaka kwa mobutu kutokana na kitendo chake cha kunyonga mawazili wale Franco anakamatwa na kuachiwa alafu anakimbilia Brazaville kwa miezi 6 mpaka pale mambo yalipokuwa shwari.

AUNTHENTICATION POLICY (Zairenisation)

Mnamo mwaka 1971 mobutu anabadili jina la Congo kuwa Zaire, sarafu kua Zaire, pamoja na miji kuitwa majina ya kiafrika, Leopoldville inakua Kinshasa, Elizabeth Ville inakua Kisangani na kadhalika, kutokana na sera ya uafrika mpaka majina ya watu yanabadilishwa.

Bendi ya Franco, Tp Ok jazz inaandamana na mobutu nchi nzima kueneza sera ya mobutu na kutoa album iitwayo belela unthenticite na congress ya mpira.

MALIPO YA KAZI

Mobutu anampa Franco eneo la ardhi pale Kinshasa, Franco anajenga night club iliyoitwa un Deux trois, pia Mobutu baada ya kubinafsisha kampuni za kigeni anampa Franco kampuni ya muziki iitwayo mazadi.

JACKY NA HELEINE(nyimbo za Franco)

Franco añatoa nyimbo mbili Jacky na heleine ambazo serikali iliziona hazina maadili na kumpa Franco kifungo cha miezi 6 jela, na bar yake kufungwa miezi 2, alivobisha kua hazina maadili mama yake alisikilizishwa, yote haya yalifanywa na Kengo wa Dondo aliyekua attorney general.

Mobutu anamtoa jela Franco baada ya week 3 na kumshusha cheo Kengo wa Dondo kua balozi wa Zaire nchini Ubelgiji, Franco anaimba nyimbo ya kumponda Kengo iitwayo trailleur (anasema fundi nguo akikinyanganya sindano utawachomaje watu? Yaani kengo kaporwa madaraka na Mobutu)

Franco anaimba lettre a mr le directeur general (barua kwa director general) nyimbo ambayo añawaponda viongozi wa serikali kwa rushwa na usimamizi mbovu, hii inachukuliwa na wengi kama diss song kwa Mobutu.

Mwka 1984 anaimba nyimbo ya kumsifu Mobutu iliyoitwa Candida na biso, wakati wa uchaguzi ambapo watu walitakiwa kujibu ndio au apana kama wanamtaka Mobutu, hakukua na wapinzani.

Mobutu alifadhili band nyingi kubwa za muziki nchini Zaire, ikiwemo TP OK JAZZ


KIFO CHA FRANCO

Franco anafariki jijini Ubelgiji mwka 1989, Mobutu akiwa Ufaransa ziarani,
Mobutu anatangaza siku 4 za maombolezo na radio zote kupiga nyimbo za Franco tu, mwili wa Franco unapelekwa Palais du people kuagwa
mobutu11-palais.jpeg


Mobutu aliporudi aliitembelea familia ya Franco pamoja na kaburi.

Kwa kiasi kikubwa Mobutu alimtumia Franco katika ku mobilize watu kwenye siasa zake na pia Franco alinufaika sana kwa kuendesha magari ya kifahari kama mercedes benz na kuishi vizuri, kuliko wanamuziki wengi wa Congo na nje ya Congo
 
asante sana sana sana. wakati nakua mzee alikuwa anapenda sana kusikiliza nyimbo za franco .sikuwa na muelewa kabisaa. mpaka leo jamaa simoendi kwa sababu ya kwamba nyimbo zake zilikuwa zinaninyima kusikiliza vipindi vingine nivipendavyo kama michezo RTD pindi mzee akiwepo. sasa nimeelewa
 
asante sana sana sana. wakati nakua mzee alikuwa anapenda sana kusikiliza nyimbo za franco .sikuwa na muelewa kabisaa. mpaka leo jamaa simoendi kwa sababu ya kwamba nyimbo zake zilikuwa zinaninyima kusikiliza vipindi vingine nivipendavyo kama michezo RTD pindi mzee akiwepo. sasa nimeelewa
Hahaha ,mkuu ,franco alipendwa sana na wazee enzi hizo,
 
Wakuu habarini za muda huu

View attachment 717548
View attachment 717549

Zimeanzishwa thread nyingi kuhusu franco na mobutu,historia ya mobutu imeelezwa na ya franco pia,leo naleta historia ya uhusiano wa watu hawa wenye majina makubwa africa na ulimwenguni,mwanasiasa na gwiji la muziki

View attachment 717532
View attachment 717529

KUNYONGWA KWA KINA EVARISTE KIMBA

Mnamo mwaka 1965 mobutu anakua rais wa zaire na kuagiza kunyongwa kwa watu zaidi ya 6 wengi wao wakiwa mawaziri wa serikali aliyoipindua katika eneo la matonge jijini leopold ville (kinshasa) kwa kosa la uhaini , mamilioni ya watu wanashuhudia hadharani ,mmoja wao ni franco , bada ya hapo franco akatunga nyimbo iitwayo luvumbu ndoki (luvumbu mchawi) hii ni hadithi ya kikongo kuhusu mfalme luvumbu aliyeuwa ndugu zake wa karibu kwa ajili ya kujinufaisha ,

Nyimbo hii inaonekana na mamlaka kama dhihaka kwa mobutu kutokana na kitendo chake cha kunyonga mawazili wale franco anakamatwa na kuachiwa alafu anakimbilia brazaville kwa miezi 6 mpaka pale mambo yalipokuwa shwari

AUNTHENTICATION POLICY (zairenisation)

Mnamo mwaka 1971 mobutu anabadili jina la congo kuwa zaire,sarafu kua zaire ,pamoja na miji kuitwa majina ya kiafrika ,leopoldville inakua kinshasa,elizabeth ville inakua kisangani na kadhalika,kutokana na sera ya uafrika mpaka majina ya watu yanabadilishwa

Bendi ya franco,Tp Ok jazz inaandamana na mobutu nchi nzima kueneza sera ya mobutu na kutoa album iitwayo belela unthenticite na congress ya mpr

MALIPO YA KAZI

Mobutu anampa franco eneo la ardhi pale kinshasa ,franco anajenga night club iliyoitwa un deux trois ,pia mobutu baada ya kubinafsisha kampuni za kigeni anampa franco kampuni ya muziki iitwayo mazadi

JACKY NA HELEINE(nyimbo za franco)

Franco añatoa nyimbo mbili jacky na heleine ambazo serikali iliziona hazina maadili na kumpa franco kifungo cha miezi 6 jela,na bar yake kufungwa miezi 2,alivobisha kua hazina maadili mama yake alisikilizishwa
Yote haya yalifanywa na kengo wa dondo aliyekua attorney general,

Mobutu anamtoa jela franco baada ya week 3 ,na kumshusha cheo kengo wa dondo kua balozi wa zaire nchini ubelgiji, franco anaimba nyimbo ya kumponda kengo iitwayo trailleur (anasema fundi nguo akikinyanganya sindano utawachomaje watu ? Yaan kengo kapolwa madarak na mobutu)

Franco anaimba lettre a mr le directeur general (barua kwa director general) nyimbo ambayo añawaponda viongozi wa serikali kwa rushwa na usimamizi mbovu,,hii inachukuliwa na wengi kama diss song kwa mobutu,

Mwka 1984 anaimba nyimbo ya kumsifu mobutu iliyoitwa candida na biso,,,wakati wa uchaguzi ambapo watu walitakiwa kujibu ndio au apana kama wanamtaka mobutu,hakukua na wapinzani,

Mobutu alifadhili band nyingi kubwa za muziki nchini zaire,ikiwemo TP OK JAZZ


KIFO CHA FRANCO

franco anafariki jijini ubelgiji mwka 1989 ,mobutu akiwa ufaransa ziarani,,
Mobutu anatangaza siku 4 za maombolezo na radio zote kupiga nyimbo za franco tu,mwili wa franco unapelekwa palais du people kuagwa
View attachment 717547

Mobutu aliporudi aliitembelea familia ya franco pamoja na kaburi


Kwa kiasi kikubwa mobutu alimtumia franco katika ku mobilize watu kwenye siasa zake,,,na pia franco alinufaika sana kwa kuendesha magari ya kifahali kama mercedes benz na kuishi vizuri,kuliko wanamuziki wengi wa congo na nje ya congo
Asante sana ubarikiwe
 
mkuu lucas mobutu
mm n kijana ila ktk simu yangu nyimbo zangu 90%, n za Franco, aisee Jamaa alikuwa na nyimbo tamu wazee wananishangaa Mimi kijana napendaje nyimbo zao? kiukweli nilizipenda nyimbo za Franco kupitia radio moja ya Kenya iitwayo citizen walikuwa wana zitafsir nilizpenda kweli kweli
Franco alikuwa rafiki wa Mobutu lkn walikuwa wanakosana na kupatana
pia kuna kisa kimoja mwaka 1973 Franco na mdg wake walikuwa wanagombnia demu sasa mdg wa Franco akaamua kusafiri na huyo demu ktk gari mdg wa franco akaamua kuangusha gari maksud ili wafe wote lkn huyo demu alivunjka mguu ila Jamaa akafariki
Franco alipata ukimwi miaka ya 1980's na hawara yake alikuwa mwanamuzk ktk bendi ya okk jazz alieitwa mpongo love
Franco alikuwa anamiliki majumba hko Belgium na France
baada ya kutunga wimbo wa kumpamba Mobutu,Franco alipewa malori 6 kama zawadi
pia Mobutu alikuwa na vituko aliwahi chukua waganga wa kienyeji nchi nzma akasafiri nao na timu ya taifa ili ishinde lkn timu hiyo ilifungwa 7_0
baadhi ya nyimbo za Franco ni
matata ya mwasi
naloba nini
fabrice
Mario
mamuu
muongo na mulozo
cooperation
lisolo ya nzambe na adamu
fc Gabon
colonel bangala
republique du Zaire
azda
masuu
muya
liberte
arzon
1200 leters
kimpa kisangameni
ngungi
attention na sida
Franco alikuwa na albamu 150, na single 1200
 
daaahhhh Franco mbona kama alikuwa ana ng'ata nakupuliza hivi ""

ila mimi sijawahi kumjua huyo Jamaa kabisaaaa ...sijui kwaajili ya utoto enzi hizo...lakini mbona nawajua watu kama kina "" Thomas ..Sankara .Mobutu mwenyewe ''na kina Thom mboya''' huyo ilikuwaje mpka nikashindwa kumfahamu huyo Franco ""!!?
 
Nyimbozake Marehem Mama yangu alikuwa anazipenda sana enzi hizo dah nimekumbuka sana aisee
 
daaahhhh Franco mbona kama alikuwa ana ng'ata nakupuliza hivi ""

ila mimi sijawahi kumjua huyo Jamaa kabisaaaa ...sijui kwaajili ya utoto enzi hizo...lakini mbona nawajua watu kama kina "" Thomas ..Sankara .Mobutu mwenyewe ''na kina Thom mboya''' huyo ilikuwaje mpka nikashindwa kumfahamu huyo Franco ""!!?
Hukuwa serious
 
Back
Top Bottom