Upotoshaji uliopo kati ya uhusiano wa teknolojia ya 5G na corona

Abdalah Abdulrahman

JF-Expert Member
Aug 29, 2019
222
201
Hivi karibuni kumetokea uvumi katika mitandao ya kijamii kuwa kuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya ugonjwa wa corona na Teknolojia ya 5G.Miongoni mwa hoja zinazotolewa ni kama zifuatazo:-

1. Kuwa karibu na 5G kuna sababisha corona, ndio maana nchi zilizo athirika zaidi ni zile zilizoanza kutumia teknolojia hii.

2. Teknolojia ya 5G inatoa miaonzi ambayo inasababisha kansa, na kuharibu kabisa vinasaba (DNA) vya binadamu.

3. Kuna dhana kuwa Corona imeanza China kutokana na China kuwa ya kwanza kujenga minara ipatayo 100,000 kwa ajili ya 5G.

4. Ipo dhana kuwa kinga dhidi ya corona itakuwa na kipandikizi cha kielekroniki (micro chip) kitakachopandikizwa kwenye mwili wa binadamu kuzuia athari za 5G. Ndio maana Bill Gate anadhamini utengenezaji wa dawa na kinga ili zisambazwe kwenye nchi maskini kwa malengo ya kiusalama.

Dhana zote hizi ni uongo, na ukweli kuhusu mfumo wa mawasiliano wa 5G ni unapatikana katika sayansi ya mionzi pamoja na ile ya mawasiliano kama ifuatavyo:-

Mfumo wa 5G kama ilivyo mifumo mingine kabla yake, mfano 2G, 3G, na 4G ambao mpaka sasa hivi unatumia/kusafiri kwa njia ya mawimbi ya redio (radio waves) ambayo ni aina moja wapo ya mionzi isiyo ainishi (non ionizing radiation) kama ilivyo katika spectra ya mionzi (electromagnetic spectrum).Mfano wa mionzi iliyo katika kundi hili la mionzi isiyo ainishi ni ile inayotumika katika microwave, ile ya jua (ultraviolet) nk.

Mionzi ainishi ambayo inaweza kuleta madhara kwenye mwili wa binadamu ni ile ya x-ray, alpha, betta, gamma ray na neutron na ile ya ultra-violet light ambayo ipo mwisho wa spectra ya mionzi (electromagnetic spectrum). Mionzi inayotokana na 5G haipo katika kundi hili.

Kwa kuwa mionzi inayotokana na 5G sio ainishi, ni wazi kuwa mionzi hii haiwezi kusababisha madhara ya cancer, kubadili kinasaba au kusababisha matatizo ya mifumo ya kupumua au yanayofana na hayo ndani ya mwili wa binadamu.

Madhara yanayoweza kupatikana katika teknolojia ya 5G ni kama yale yanayoweza kupatikana katika teknolojia ya 2G, 3G, na 4G, ambayo pia yanaweza kupatikana katika microwaves, ultraviolet ambayo ni kuongeza joto la seli.

Mfano ukiongea na simu kwa muda mrefu unapata maumivu kwani seli za sehemu za sikio ni laini. Vivyo hivyo tunashauriwa kutopakata laptop ili joto linaloongezeka kutokana na kupakata laptop lisiathiri sehemu za uzazi ambazo seli zake ni laini na ni rahisi kuathiriwa na joto.

Binafsi ninaweza kutoa mjumuisho ufuatao katika hili:-

Moja kuna upotoshaji unaofanyika kwa makusudi au kwa kutokujua kuhusu mionzi na corona, upotoshaji huu unaweza kuwa na madhara ya kiafya kwa watu kutokuchukua tahadhari stahiki kwa ugonjwa huu wa corona na kuongeza hofu ambayo haipo.

Pili, upotoshaji huu unalenga pia kujipatia kipato kwa wale wanaotafuta idadi kubwa ya watu wanaosoma makala zao katika mitandao ya kijamii.

Tatu, upotoshaji huu unaweza kuwa unafanywa na mataifa makubwa kama Marekani na washirika wake ambayo yanahofu na China kwenye Teknolojia ya 5G.

Vile vile upotoshaji huu unaweza kuwa na athari za kuhofia Teknolojia ya 5G ambayo ndio dunia inapoelekea na hivyo kuwabakisha watu nyuma.
 
Coronavirus: Madai ya wanasayansi kuhusu 5G ni 'upuuzi mtupu'

Woman using mobile phone

Dhana zinazodai kuwa teknolojia ya 5G ilisaidia kusambaza coronavirus zimelaaniwa na wanasayansi.

Video imekua ikisambazwa kwenye mitandao ya kijamii ikionyesha minara ya mawasiliano ya simu za mkononi ikiungua katika miji ya Birmingham na Merseyside - sambamba na madai hayo.

Video hiyo imekua ikishirikiswa watu kupitia mitandao ya Facebook, YouTube na Instagram - zikiwemo kurasa rasmi zenye maelfu ya wafuasi.

Lakini wanasayansi wanasema kuwa wazo la uhusiano kati ya Covid-19 na 5G ni "upuuzi mtupu" na lisilowezekana kibaiolojia.

Nadharia hizi zimetajwa kama "taarifa mbaya zaidi feki" na Mkurugenzi wa tiba katika taasisi ya huduma za afya nchini Uingereza Bwana Stephen Powis.

Nadharia fiche

Wengi wa wale wanaoshirikisha ujumbe huu wanasambaza taarifa potofu zinazodai kuwa teknolojia ya 5G - ambayo inatumiwa katika mitandao ya simu za mkononi na hutegemea taarifa zinazosambazwa na mawimbi ya radio - inahusika kwa namna fulani na coronavirus.

Nadharia hizi zinaonekana kujitokeza kwa mara ya kwanza kupitia jumbe za Facebook mwishoni mwa mwezi wa Januari, wakati mbapo kisa cha kwanza cha virusi hivyo kilipotokea nchini Marekani.
Madai hayo yanaonekana kwa kiasi kikubwa kuwa ya aina mbili:
  • Dai moja nikwamba 5G inaweza kuzuia utendaji wa mfumo wa kinga, na hivyo kuwafanya watu kuwa kupata virusi kwa urahisi.
  • Madai mengine yanasema virusi vinaweza kwa namna fulani kuambukizwa kupitia matumizi ya teknolojia ya 5G.
Madai haya yote ni "upuuzi mtupu ," anasema Dkt Simon Clarke, profesa wa masuala ya seli za microbiolojia katika Chuo Kikuu cha Reading.

mobile network


Minara ya mawasiliano ya simu za mkononi Birmingham na Merseyside, uliungua na kusababisha uchunguzi

" Wazo kwamba 5G hupunguza mfumowa kinga ya mwili si swala hata la kuchunguzwa ," anasema Dkt Clarke.

"Mfumo wako wa kinga ya mwili unaweza kupunguzwa na vitu mbali mbali mkiwemo mchoko wa mwili wa siku moja, au kwa kutokula lishe bora. Mabadiliko hayo si makubwa lakini yanaweza kukufanya uwe katika hali ya kupatwa na virusi."

Huku mawimbi thabiti ya radio yakiwa na uwezo wa kusababisha joto, 5G si imara vya kutosha kuweza kuwatia joto watu kiasi cha kuleta madhara.

"Mawimbi ya Radio yanaweza kuvuruga saikolojia unapopatwa na joto, ikimaanisha kuwa mfumo wako wa kinga ya mwili hauwezi kufanya kazi ipasavyo. Lakini viwango vya nishati kutoka kwa mawimbi ya radio ya 5G ni vidogo sana na haviko imara kiasi cha kusababisha athari kwenye mfumo wa kinga ya mwili . Hakuna uchunguzi uliokwishafanyika juu ya hili ."

Graphic shows 5G's frequencies on the electromagnetic spectrum - within the non-ionising band at the lower end of the scale.


Mawimbi ya radio yanayotumiwa katika 5G na teknolojia nyingine za simu za mkononi hutumia masafa ya chini ya kiwango cha sumaku ya umeme. Nishati yake ni ya chini kuliko hata kiwango cha nishati ya mwanga wa taa , haina nguvu kiasi cha kuharibu seli za mwili-kinyume na mionzi yenye masafa ya juu ambayo inajumuisha miale ya jua na mionzi ya kimatibabu (medical x-rays)

Haiwezekani kwa 5G kueneza virusi vya corona, Adam Finn, profesa wa matibabu ya watoto katika Chuo kikuu cha Bristol, anaongeza.

"Janga la sasa la coronavirus lilisababishwa na virusi vinavyoambukizwa kutoka kwa mtu mmoja aliyeathiriwa kwa mtu mwingine. Tunafahamu hili ni kweli. Hata tuna virusi vinavyokuzwa katika maabara zetu, vilivyochukuliwa kutoka kwa mtu aliyekua anaugua. Virusi na mawimbi ya nishati ya umemeinayotengeneza mawasiliano ya mitandao ya intaneti na simu za mkononi hufanya kazi tofauti. Tofauti yake ni sawa na ya chaki na jibini," anasema.

Ni muhimu pia kutambua kuwa nadharia nyingine zinazosambazwa kwamba - coronavirus inasambazwa katika miji ya Uingereza ambako teknolojia ya 5G haijatumiwa, na katika nchi kama Iran ambazo bado hazijaanza kutumia teknolojia hiyo.

Kulikua na taarifa nyingi za kutisha kuhusu 5G zilizosambazwa kabla ya mlipuko wa coronavirus ambazo kitengo cha BBC cha uchunguzi wa ukweli wa taarifa zinazoenea- Reality Check has kilikua tayari kinazichunguza , moja ya taarifa hizo ni kuhusu ikiwa 5G inasababisha hatari za kiafya

Mapema mwaka huu, uchunguzi wa muda mrefu kutoka kwa Shirika linalosimamia ulinzi wa mawasiliana ya kimataifa yasiyotumia mionzi (ICNIRP) lilipinga madai haya, likisema hakuna ushahidi kwamba mitandao ya simu inasababisha saratani au ugonjwa mwingine wowote ule.
 
Mwaka huu wata tajana tu naona wameshachokana na conspiracy theory zao. lakini kiukweli hapa kuna kitu kinafichwa kuhusu corona, how come wapo confident itatokomea baada ya miezi mi3, wao Mungu?.
 
Siku zote Marekani inataka ionekane ipo juu. China ilipoanzisha mfumo wa 5G hawakupenda kabisa na wakajitahidi kuyatisha mataifa ya Ulaya yasikubali mfumo huu wa Wachina, mojawapo ni Uingereza.

Hizo ni mbinu tu kuhakikisha kwamba wao ndio wanaweza kuendesha mfumo huo kwa hali ya juu zaidi.
 
Sasa utatoa hoja gani kama hujawahi kusoma Genetics na biology kwa ujumla, kama wewe physics yako uliishia tu archimedes principle na yenyewe hata hukuilewa na vitu kama bombardment, half live of nuclear material au aina za mionzi kama gama, alfa nk hujawahi kuzisikia hata zina sifa gani.

Wewe elimu uliyosoma ni mwanamutapa empire, sijui glaciation features, sijui viambishi vya a unganifu, sijui syntax na sasa ni sasa unajiita mwanaharakati unaandika maugoro kwenye mitandao ama unawahubiria watu kwenye makanisa yako na wanakupigia makofi si utajuaje tofauti ya corona na 5G?

Si utafikiri mafaili yakijichanganya jibu lako la mwisho la mtu asiyefikiria akikosa jibu la mafanikio ya mtu ama kitu kigumu ataita '' freemason ''?
 
Kama kuna scientific evidence to link 5G Technology na Novel Coronavirus tusibishe tusubiri tutaona kwa sababu China wameikomalia mno hii technology.
 
DESTURI YA 5G . inapogusa mwili wa binadamu inaleta sumu. Haya mambo usiyaseme tu kwa elimu ya kitaaluma. unatakiwa uwe unafuatilia na mambo ya kiroho kidogo. Wengi huko ndiyo watupu. Shetani hataki kabisa watu waelewe.
Mimi nipo kiroho zaidi, naamini watu wa Psychic, wanaamini. Wewe endelea kuwa wa mwisho kuamini ili utimilize lengo lao, wazee wa ILLUMINATI .

Hili kundi la secret society, unalijua? Hawa wana akili na pesa nyingi sana, hawa wanaweza kukupangia dunia iwe na ikwawa kwa matakwa yao .

Kwa swala la 5G... Mwili wa mwanadamu unapopata ile mionzi ya 5G . cell zinapata sumu . Huku mwili ukiwa unafanya harakati za kujilinda. Unatoa uute Fulani na majimaji ( DNA na RNA ), hapo ndipo mtu anapata mafua . ULE UTE ULIOTOKA BAADA YA MIONZI HIYO NDIYO INAITWA KIRUSI. Ila si cha corona. Kwa sababu cell ya mtu imepata sumu . Ukimpima utaona hao virus, dalili zote kama za corona, utaona kwa sababu mtu huyo amaeingiliwa na virusi .

Swali ninalojiuliza virusi hivi, kama vinaleta dalili hizi, vinaitwaje vya corona vinatoka kwa mnyama wa aina ya popo. Mwenye akili atajua .
 
China ndiyo wanatengeneza ili wawe wakwanza kuwa na 5G kweli maana wanaosema wana 5G si kweli ndiyo nguzo zinaanza kuwekwa
 
Ukitaka kujua ujinga wa watu ktk sayansi, ni jambo hili la 5G. Kuna watu hawana hata sifa ya kujadili sayansi kama Gwajima, eti naye anajadili 5G na corona na anashangiliwa kasema ya maana. Nimefikia uamuzi kwamba kama kuna muda wa kujadili hili na kubishana, basi tuacheni kule kwetu nasi tuwe wachawi kwa hisia zetu.
 
China ndiyo wanatengeneza ili wawe wakwanza kuwa na 5G kweli maana wanaosema wana 5G si kweli ndiyo nguzo zinaanza kuwekwa
China wawe wa kwanza huku South Korea waliishazindua kupitia LG project yao?
 
Sasa utatoa hoja gani kama hujawahi kusoma Genetics na biology kwa ujumla, kama wewe physics yako uliishia tu archimedes principle na yenyewe hata hukuilewa na vitu kama bombardment, half live of nuclear material au aina za mionzi kama gama, alfa nk hujawahi kuzisikia hata zina sifa gani.

Wewe elimu uliyosoma ni mwanamutapa empire, sijui glaciation features, sijui viambishi vya a unganifu, sijui syntax na sasa ni sasa unajiita mwanaharakati unaandika maugoro kwenye mitandao ama unawahubiria watu kwenye makanisa yako na wanakupigia makofi si utajuaje tofauti ya corona na 5G?

Si utafikiri mafaili yakijichanganya jibu lako la mwisho la mtu asiyefikiria akikosa jibu la mafanikio ya mtu ama kitu kigumu ataita '' freemason ''?
Na mwisho kabisa akikosa jibu utawasikia haya ni mambo ya kiroho. Hapo ujue umekutana na asiyejua kitu huku akidhani anajua kila kitu
 
Kulingana theory mageuko au mabadiliko kisayansi MUTATION .inawezeka 5G Ika badilisha Coronavirus asiye na madhara kwenda Coronavirus mwenye maradha( COVID-19). It may be 5G As radiation mutate it in covi-19
 
Kama nilivyo andika hapo juu. Ni kwamba hakuna nchi au mtu anayeweza kufikiri kutengeneza virus vya corona ili kuua watu. Sio china, wala us , wala nchi yeyeto. Bali coronavirsus wamebadilisha kibaiolojia wame mutate kutoka form isiyo na madhara kwende kwenye form madhara(covid-19) huenda ni kutoka na mabadiliko ya tabia nchi. Also Technology ya 5G inaweza ku mutate au kubadilisha virus... Ingawa lengo 5G ni kwaajiri maendeleo yetu. Kama 5G Imemutate corona to covid-19 ni bahati mbaya . tumuogope Mungu China haikuwa na lengo Lengo baya kutulete 5G. I
 
Back
Top Bottom