Tokea Mh. Lissu anusurike kwenye shambulio dhidi ya uhai wake siku ashara na kitu zilizopita, kumekuwepo na sauti kadhaa zinazodai au zinazotaka tukio hilo lichunguzwe na wachunguzi 'huru' kutoka nje ya nchi.
Sababu yake kubwa ni kwamba vyombo vya ndani [ya nchi] vya usalama haviko huru kuweza kufanya uchunguzi huo kwa sababu vyenyewe ndivyo vinavyoshukiwa kupanga na kutekeleza jaribio hilo ili kutimiza matakwa ya mtu au watu wa huko serikalini na kwenye CCM.
Hisia hizo [za kuishuku na kuituhumu] nazielewa. Hivyo watu wanaotaka kuona wachunguzi huru wakichunguza nao nawaelewa.
Ila, kuna vitu vinanitatiza kidogo kuhusu huo u huru wa hao wachunguzi na utayari wa kambi ya Lissu na kambi ya serikali kuyakubali matokeo ya huo uchunguzi wao endapo utatokea.
La kwanza, ni nani atayeingia gharama za hao wachunguzi?
Tuseme CHADEMA na wafadhili wao ndiyo wataingia hizo gharama.
Kama hivyo ndo itavyokuwa, je, hao wachunguzi watakuwa huru kiasi gani ilhali wanalipwa na upande wa mnusurika wa jaribio?
CHADEMA kweli inaweza kuwalipa hao wachunguzi huru halafu hao wachunguzi watoe uchunguzi ambao ni kinyume na madai ya CHADEMA [kwamba serikali kupitia vyombo vyake vya usalama ndiye mhusika]? Kama wataletwa na CHADEMA maana yake ni kwamba wao ni waajiriwa wa hicho chama. Akili yangu haioni ni jinsi gani hao wachunguzi huru wanaweza kutoa matokeo yaliyo kinyume na hisia za watu waliowaajiri.
Je, serikali nayo ipo tayari kweli kuyakubali matokeo ya hao wachunguzi huru ambao huenda wakalipwa na hicho chama pinzani?
Na vipi kwa mfano serikali ikubali ujio wa hao wachunguzi na iingie gharama kwa kazi watayoifanya, je, CHADEMA ipo tayari kuyapokea na kuyakubali matokeo ya huo uchunguzi hata kama yakiwa tofauti na vile wao wadhaniavyo?
Kumbuka, kama serikali ndiyo itayoingia gharama za hao watu maana yake ni kwamba watakuwa wanaitumikia serikali iliyopo madarakani ambayo ni ya CCM.
Kwa mtaji huo hao wachunguzi huru watakuwa wapo huru kiasi gani?
Hili suala ni gumu kwa kweli. Kila ninapowaza na kuwazua sipati majibu.
Sijui nyie wadau mnalionaje hilo suala.
Jumapili njema.
Alipokuja Obama Tanzania ikulu ya Magogoni ilikuwa chini ya walinzi wa Kimarekani.Ukirudia kusoma hiki ulichoandika nadhani hutaamini macho yako. Sijui una umri gani lakini nikukumbushe tukio la kulipuliwa ubalozi wa Marikani hapa Dar. Ni FBI ndio walikuja nchini kufanya upelelezi na hata kugundua ni nani walihusika. Sijui kama unakumbuka mauaji ya Padri kule Zanzibar? Kikwete aliruhusu wapelelezi kutoka nje waje wasaidie kufichua wahusika wa mauaji yale. Kwa hiyo mjomba uhuru wa nchi hauuzwi kwa kuruhusu wapelelezi wa nje kuja kusaidia hawa wa ndani. Labda hujui tu kwamba baadhi ya hao wapelelezi wetu wamepata mafunzo kutoka kwa hao wazungu unaowaogopa.
Kama ni hivyo ina maana tunarudi kwenye original post, je nani atawalipa?
Unasumbuliwa na nnya.
Hiyo ni ndani yabTanzania jinga wewe.
View attachment 594761View attachment 594762View attachment 594763
If you really mean it, hao US na UK wafute madeni wanayotudai ambayo walitumia uhuni kutuingiza mkenge.The UK has a budget of $1.04 trillion. The US has a budget of over $3.8 trillion. They can easily afford the cost of sending Scotland Yard or FBI for few weeks to conduct an independent investigation. Also, to receive money for services rendered to a poor third world country would be shameful for U.K. or U.S.
Labda tujiulize jambo moja, wale wapelelezi waliofichua mauaji ya Robert Ouko wa Kenya walilipwa na nani? Na kwa nini findings zao zilikubaliwa na kila MTU?
Hpo ndpo nashangaa na mimi, wenye maelezo yote wako nje.Vyombo vya usalama vitamkamata nani ikiwa mashahidi wa muhimu wote wapo Nairobi?
Kuna mtu kapost mitandaoni anashangaa kwamba Kibiti wameuliwa watu zaidi ya 40 lakini hatukusikia habari za wapelelezi wa kimataifa kuja kuwatafuta wauaji!!.
Wakati wanauliwa wale wananchi wasio na hatia humu mitandaoni kulijaa kejeli nyingi za ajabu, tena nyingine kutoka kwa hawa ambao wanataka wapelelezi wa kimataifa waje kufanya uchunguzi wa jaribio la mauaji.
Yaani mauaji ya watu zaidi ya 40 hayakustahili kufanyiwa uchunguzi wa kimataifa, lakini jaribio moja tu ndilo muhimu kwa sasa kwa taifa letu!!.
Mungu na anisamehe kama nimemkwaza mtu yoyote yule, ni katika kujaribu kuchangia mawazo yangu katika jumapili ya leo.
What benefits they get after spending their budget for this investigation?
Kuna mtu kapost mitandaoni anashangaa kwamba Kibiti wameuliwa watu zaidi ya 40 lakini hatukusikia habari za wapelelezi wa kimataifa kuja kuwatafuta wauaji!!.
Wakati wanauliwa wale wananchi wasio na hatia humu mitandaoni kulijaa kejeli nyingi za ajabu, tena nyingine kutoka kwa hawa ambao wanataka wapelelezi wa kimataifa waje kufanya uchunguzi wa jaribio la mauaji.
Yaani mauaji ya watu zaidi ya 40 hayakustahili kufanyiwa uchunguzi wa kimataifa, lakini jaribio moja tu ndilo muhimu kwa sasa kwa taifa letu!!.
Mungu na anisamehe kama nimemkwaza mtu yoyote yule, ni katika kujaribu kuchangia mawazo yangu katika jumapili ya leo.
Hpo ndpo nashangaa na mimi, wenye maelezo yote wako nje.
Hawahitaji pesa wanachohitajinibarua ya serikali ya kuwaruhusu tu
Words came straight from my soul. Sometimes true words make us better human beings.Shhhh....can't say that...
Hivi kwenye hii sayari inayoitwa earth iliwahi kutokea aliefanya uhalifu akajikamata yeye mwenyewe?Vyombo vya usalama vitamkamata nani ikiwa mashahidi wa muhimu wote wapo Nairobi?