Uhuru wa wachunguzi huru

Uhuru wa wachunguzi huru

Wadau,
Maswali machache ya kuanzia:

1: Je vyombo vya usalama vimeshaanza uchunguzi?

2: Kam Mh. Mbowe yuko Dar, je yule shahidi muhimu kabisa DEREVA nae amerudi TZ au bado yuko Nairobi?

3: Je vyombo vya usalama vimefanya proceses zozote ile mashahidi wote walioko nje ya nchi waweze kuhojiwa na Interpol?

4: Je ballistic na forensic reports ziko tayari?

5: Je zile namba za magari mawili tofauti yanayotajwatajwa kwenye media zinaonyesha mmiliki wa hayo magri ni nani?

My 2 cents
 
We ndo hujatumia akili! anachomaanisha huo upelekezi ungekuwa huru kiasi gan kwa maana ungeweza kuegemea kwa upande uliowaleta na kuwalipa, ungeanza hapo kujadili



Na wewe pia think out of box. Usifananishe FBI na hawamakanjanja wetu wanaoegemea upande mmoja.


Wapepelezi wamejijengea heshima na uadilifu miongo kwa miongo waje waharibu heshima ya taasisi yao kwa hili la lisu?
 
Kwanza naomba kuuliza, hivi kuna sheria Tanzania au nchi yoyote ambayo inaruhusu Jeshi la nchi moja kuingia kufanya kazi kwenye ardhi ya nchi nyingine? (Ukiacha peace making missions za UN kwenye maeneo yenye vita?).

Au Tuseme labda kuna mtu ambaye yupo very critical kwa serikali ya Marekani akauwawa, je Scotland Yard inaweza kweli kwenda kufanya uchunguzi Marekani? Kwa sababu eti wananchi wanahisi kuwa FBI au Homeland security hawatakuwa huru, je hili linawezekana?

Au hata kama wakiruhusiwa hapa Tanzania hao "wachunguzi huru" watawezaje kufanya kazi bila jeshi la polisi kuhusika? Maana wao ndio wana machinery ya all criminal investigations hapa Tanzania. Hao "wachunguzi huru" watakuwa huru kiasi gani kwenye nchi ambayo si ajabu hata lugha yake hawaiongei.

Labda tuseme Interpol watakuja.. sasa Interpol si ndio polisi hao hao, hata ofisi zao zipo pale Police headquarters.

Silazimishi mtu kunielewa.. Nyani Ngabu ameshasema ' You're entitled to your own imagination' lakini hivi hili swala tunaliangalia vizuri kweli?

Narudia sijakushikia akili, amini utakavyo.
 
Hahaha kwa hiyo Scotland yard watachukua rushwa ya chadema hahaha
 
Jambo la muhimu waruhusiwe kwanza wafanye huo uchunguzi.

Kitendo cha serikali kukataa huo uchunguzi huru unaleta picha gani ilihali vyombo vyetu vya usalama hadi sasa havijafanikiwa kukamata hao wasiojulikana japo namba za Nissan Patrol zimetajwa.

Uchunguzi huru uruhusiwe, matokeo yana sehemu mbili(positive & negative) na hayaepukiki

Mkuu unafahamu kitu chochote kuhusu National Security? Na je, Unafahamu maana ya Nchi kuwa huru? Tuna vyombo vya usalama vilivyo huru na kamwe kuachia wazungu kuja kuchunguza nchi ni kuuza uhuru na pia kuuza nchi yenyewe.
Acheni kuwa mnarahisisha mambo. Kibiti mbona kina Mbowe na timu yake hawakuomba uchunguzi huru? Wanataka kuficha madhambi yao eeh!?
 
Tokea Mh. Lissu anusurike kwenye shambulio dhidi ya uhai wake siku ashara na kitu zilizopita, kumekuwepo na sauti kadhaa zinazodai au zinazotaka tukio hilo lichunguzwe na wachunguzi 'huru' kutoka nje ya nchi.

Sababu yake kubwa ni kwamba vyombo vya ndani [ya nchi] vya usalama haviko huru kuweza kufanya uchunguzi huo kwa sababu vyenyewe ndivyo vinavyoshukiwa kupanga na kutekeleza jaribio hilo ili kutimiza matakwa ya mtu au watu wa huko serikalini na kwenye CCM.

Hisia hizo [za kuishuku na kuituhumu] nazielewa. Hivyo watu wanaotaka kuona wachunguzi huru wakichunguza nao nawaelewa.

Ila, kuna vitu vinanitatiza kidogo kuhusu huo u huru wa hao wachunguzi na utayari wa kambi ya Lissu na kambi ya serikali kuyakubali matokeo ya huo uchunguzi wao endapo utatokea.

La kwanza, ni nani atayeingia gharama za hao wachunguzi?

Tuseme CHADEMA na wafadhili wao ndiyo wataingia hizo gharama.

Kama hivyo ndo itavyokuwa, je, hao wachunguzi watakuwa huru kiasi gani ilhali wanalipwa na upande wa mnusurika wa jaribio?

CHADEMA kweli inaweza kuwalipa hao wachunguzi huru halafu hao wachunguzi watoe uchunguzi ambao ni kinyume na madai ya CHADEMA [kwamba serikali kupitia vyombo vyake vya usalama ndiye mhusika]? Kama wataletwa na CHADEMA maana yake ni kwamba wao ni waajiriwa wa hicho chama. Akili yangu haioni ni jinsi gani hao wachunguzi huru wanaweza kutoa matokeo yaliyo kinyume na hisia za watu waliowaajiri.

Je, serikali nayo ipo tayari kweli kuyakubali matokeo ya hao wachunguzi huru ambao huenda wakalipwa na hicho chama pinzani?

Na vipi kwa mfano serikali ikubali ujio wa hao wachunguzi na iingie gharama kwa kazi watayoifanya, je, CHADEMA ipo tayari kuyapokea na kuyakubali matokeo ya huo uchunguzi hata kama yakiwa tofauti na vile wao wadhaniavyo?

Kumbuka, kama serikali ndiyo itayoingia gharama za hao watu maana yake ni kwamba watakuwa wanaitumikia serikali iliyopo madarakani ambayo ni ya CCM.

Kwa mtaji huo hao wachunguzi huru watakuwa wapo huru kiasi gani?

Hili suala ni gumu kwa kweli. Kila ninapowaza na kuwazua sipati majibu.

Sijui nyie wadau mnalionaje hilo suala.

Jumapili njema.
Napata mashaka sana kama kweli hii ID inatumiwa na muhusika wa ID.

Haiwezekani ageuke na kuwa mjinga wa viwango hivi tena mwenye exposure ya kutosha namna vyombo kama CIA na FBI wanavyofanyakazi zao.

Unasikitisha sana, sijui ni nini kimekutokea, hata Field Mashal Es tulikuwa naye humu sasa ni kwamba alikuwaga amekuwa mbeba briefcase ya Bashite.

Huko ndiko uendako and where you deserve.
 
You're entitled to your imagination.
Nyani ngabu, yule aliwahi kuandika "matako ya sufuria hayaogopi ukali wa moto", naomba usome my thinking not necessarily my imagination.

Nafikiri unakumbuka suala la kuchomwa kwa Shule ya Wasichana ya Shauritanga miaka ile ya 1990 mwanzoni. Swali la tafakari, nani aliwalipoa gharama Scotland yard katika uchunguzi ule ambao tunajua matokea ya uchunguzi yalitiwa kapuni lakini siri baadaye zikaanza kuvujishwa na hawa ambao leo wamestaafu?
 
Wale huwa wanajitolea, Kama sisi tulivyo jitolea kulinda amani Kongo na kwingineko

Kwahiyo swali la malipo halipo
 
Nyani ngabu, yule aliwahi kuandika "matako ya sufuria hayaogopi ukali wa moto", naomba usome my thinking not necessarily my imagination.

Can't read your thinking because I can't get in your head.

What else?
 
Uchunguzi huru wa kazi gani wakati tulisoma albadir waliohusika wote wapatwe na mabaya na tayari dreva kshaanza kupoteza kumbukumbu huko Nairobi
 
Kwanza naomba kuuliza, hivi kuna sheria Tanzania au nchi yoyote ambayo inaruhusu Jeshi la nchi moja kuingia kufanya kazi kwenye ardhi ya nchi nyingine? (Ukiacha peace making missions za UN kwenye maeneo yenye vita?).

Au Tuseme labda kuna mtu ambaye yupo very critical kwa serikali ya Marekani akauwawa, je Scotland Yard inaweza kweli kwenda kufanya uchunguzi Marekani? Kwa sababu eti wananchi wanahisi kuwa FBI au Homeland security hawatakuwa huru, je hili linawezekana?

Au hata kama wakiruhusiwa hapa Tanzania hao "wachunguzi huru" watawezaje kufanya kazi bila jeshi la polisi kuhusika? Maana wao ndio wana machinery ya all criminal investigations hapa Tanzania. Hao "wachunguzi huru" watakuwa huru kiasi gani kwenye nchi ambayo si ajabu hata lugha yake hawaiongei.

Labda tuseme Interpol watakuja.. sasa Interpol si ndio polisi hao hao, hata ofisi zao zipo pale Police headquarters.

Silazimishi mtu kunielewa.. Nyani Ngabu ameshasema ' You're entitled to your own imagination' lakini hivi hili swala tunaliangalia vizuri kweli?

Narudia sijakushikia akili, amini utakavyo.
Mwandishi Wetu, Zanzibar

ASKARI wa Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI), wamewasili Zanzibar kufanya uchunguzi wa kuwabaini waliomuua kwa kumpiga risasi, Padri Evarist Mushi wa Kanisa Katoliki.


Kamishna wa Polisi wa Zanzibar, Mussa Ali Mussa alisema kwa simu jana kuwa wapelelezi wa kigeni wamewasili Zanzibar na tayari na wameanza kazi hiyo.
Wapelelezi hao wameingia kazini kushirikiana na wenzao wa Tanzania kuwasaka wauaji wa padri huyo aliyepigwa risasi Februari 17, mwaka huu.


Padri Mushi aliuawa asubuhi alipokuwa akienda kuongoza ibada katika Kanisa la Mtakatifu Teresia, Beit el Raas, nje kidogo ya Mji wa Zanzibar na kuzikwa Kitope, Kaskazini Unguja Februari 20, mwaka huu.


“Wapelelezi kutoka nje wamefika na wapo kazini,” Kamishna Mussa alisema bila ya kutaja wanatoka nchi gani.


Pia Kamishna Mussa hakutaka kueleza ni lini wapelelezi hao walifika Zanzibar na idadi yao kwa maelezo kwamba hizo ni siri za Polisi na zikivuja, zitaingilia uchunguzi wanaoufanya.
Hata hivyo, vyanzo vya ndani ya Serikali, vililithibitishia gazeti hili kuwa FBI walikuwa wameanza kuwasaka wauaji wa Padri Mushi.


Kutua kwa wapelelezi hao wa Marekani kunafuatia kauli iliyotolewa na Rais Jakaya Kikwete katika salamu zake za rambirambi baada ya mauaji ya Padri Mushi kuwa ameliagiza Jeshi la Polisi kutumia nguvu zake zote pamoja na kushirikiana na vyombo vingine vya usalama vya ndani na mashirika ya upelelezi ya nchi rafiki katika kufanya uchunguzi wa mauaji hayo.


Awali, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi alihusisha tukio hilo na vitendo vya ugaidi wakati akitoa tamko la Serikali na kueleza kuwa Rais Kikwete ameidhinisha Serikali kugharamia wapelelezi kutoka nje.


Pia ujio wa FBI unaweza kuhusishwa moja kwa moja na dhamira iliyoonyeshwa mapema na Serikali ya Marekani iliyokuwa tayari kusaidia upelelezi wa mauaji hayo na hiyo ilibainishwa katika salamu za rambirambi za kifo hicho na Balozi wa Marekani nchini, Alfonso Lenhardt.
Vyanzo mbalimbali kutoka ndani ya Serikali vimeeleza kuwa kabla ya kuanza kwa operesheni hiyo, maofisa wa FBI walifanya mazungumzo na Waziri Nchimbi na viongozi wengine wa Serikali kwa ajili ya kuangalia ni namna gani watafanya shughuli hiyo.


“Pia hawa jamaa wa FBI walifanya vikao na maofisa wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), ili kuweka sawa mazingira ya kufanya upelelezi huu,” kilisema chanzo kingine.


Habari zaidi zinaeleza kuwa uchunguzi wa wapelelezi hao wa FBI na wale wa Tanzania hautajikita katika kusaka wauaji wa Padri Mushi pekee, bali watakwenda mbali zaidi na kuchunguza wale wote wanaojihusisha na wimbi la vurugu za kidini nchini ambalo linatishia amani.


Hii itakuwa mara ya pili kwa FBI kuja nchini kufanya operesheni kubwa ya upelelezi. Mwaka 1998 walifika kuchunguza kulipuliwa kwa Ubalozi wa Marekani na kugundua kuwa Kundi la Al-Qaeda lilihusika.


Aidha hiyo ni mara ya tatu kwa wapelelezi wa Tanzania kushirikiana na wageni kuchunguza matukio ya uhalifu baada ya mwaka 1984, Idara ya Upelelezi ya Uingereza, Scotland Yard ya Uingereza kuchunguza kuungua kwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT).


Habari zaidi zinaeleza kuwa kabla ya ujio wa FBI, Serikali ya Tanzania ilizungumza na taasisi za upelelezi za nchi tano ili kuongeza nguvu. Taasisi nyingine zinazodaiwa kuombwa kufanya kazi hiyo ni pamoja na Scotland Yard na Shirika la Upelelezi la Israel, Mossad.


Akizungumzia upelelezi wa mauaji ya Padri Mushi, Kamishna Mussa alisema watu kadhaa wametiwa mbaroni kwa mauaji lakini asingeweza kutaja idadi.


Kuuawa kwa padri huyo ni miongoni mwa matukio ya kushambuliwa kwa viongozi wa dini huko Zanzibar baada ya kumwagiwa tindikali Katibu wa Mufti, Fadhil Soraga, kupigwa risasi kwa Padri Ambrose Mkenda wa Kanisa Katoliki na kuuawa kwa Sheikh Ali Khamis shambani kwake huko Kidoti, Mkoa wa Kaskazini Unguja.
 
Tokea Mh. Lissu anusurike kwenye shambulio dhidi ya uhai wake siku ashara na kitu zilizopita, kumekuwepo na sauti kadhaa zinazodai au zinazotaka tukio hilo lichunguzwe na wachunguzi 'huru' kutoka nje ya nchi.

Sababu yake kubwa ni kwamba vyombo vya ndani [ya nchi] vya usalama haviko huru kuweza kufanya uchunguzi huo kwa sababu vyenyewe ndivyo vinavyoshukiwa kupanga na kutekeleza jaribio hilo ili kutimiza matakwa ya mtu au watu wa huko serikalini na kwenye CCM.

Hisia hizo [za kuishuku na kuituhumu] nazielewa. Hivyo watu wanaotaka kuona wachunguzi huru wakichunguza nao nawaelewa.

Ila, kuna vitu vinanitatiza kidogo kuhusu huo u huru wa hao wachunguzi na utayari wa kambi ya Lissu na kambi ya serikali kuyakubali matokeo ya huo uchunguzi wao endapo utatokea.

La kwanza, ni nani atayeingia gharama za hao wachunguzi?

Tuseme CHADEMA na wafadhili wao ndiyo wataingia hizo gharama.

Kama hivyo ndo itavyokuwa, je, hao wachunguzi watakuwa huru kiasi gani ilhali wanalipwa na upande wa mnusurika wa jaribio?

CHADEMA kweli inaweza kuwalipa hao wachunguzi huru halafu hao wachunguzi watoe uchunguzi ambao ni kinyume na madai ya CHADEMA [kwamba serikali kupitia vyombo vyake vya usalama ndiye mhusika]? Kama wataletwa na CHADEMA maana yake ni kwamba wao ni waajiriwa wa hicho chama. Akili yangu haioni ni jinsi gani hao wachunguzi huru wanaweza kutoa matokeo yaliyo kinyume na hisia za watu waliowaajiri.

Je, serikali nayo ipo tayari kweli kuyakubali matokeo ya hao wachunguzi huru ambao huenda wakalipwa na hicho chama pinzani?

Na vipi kwa mfano serikali ikubali ujio wa hao wachunguzi na iingie gharama kwa kazi watayoifanya, je, CHADEMA ipo tayari kuyapokea na kuyakubali matokeo ya huo uchunguzi hata kama yakiwa tofauti na vile wao wadhaniavyo?

Kumbuka, kama serikali ndiyo itayoingia gharama za hao watu maana yake ni kwamba watakuwa wanaitumikia serikali iliyopo madarakani ambayo ni ya CCM.

Kwa mtaji huo hao wachunguzi huru watakuwa wapo huru kiasi gani?

Hili suala ni gumu kwa kweli. Kila ninapowaza na kuwazua sipati majibu.

Sijui nyie wadau mnalionaje hilo suala.

Jumapili njema.
Hao wachunguzi wanajitolea toka nchi zao,Mh.lissu ni MTU Wa kimataifa.Kwani matibabu amepataje????
 
We ndo hujatumia akili! anachomaanisha huo upelekezi ungekuwa huru kiasi gan kwa maana ungeweza kuegemea kwa upande uliowaleta na kuwalipa, ungeanza hapo kujadili
Option ya tatu ambayo hajaizungumzia ni kuwa hao wachunguzi huru wanaweza kulipwa na nchi husika.
 
Mkuu unafahamu kitu chochote kuhusu National Security? Na je, Unafahamu maana ya Nchi kuwa huru? Tuna vyombo vya usalama vilivyo huru na kamwe kuachia wazungu kuja kuchunguza nchi ni kuuza uhuru na pia kuuza nchi yenyewe.
Acheni kuwa mnarahisisha mambo. Kibiti mbona kina Mbowe na timu yake hawakuomba uchunguzi huru? Wanataka kuficha madhambi yao eeh!?
Nani kakwambia kuwa kuachia "wazungu" kuja kuchunguza ni kuuza uhuru? Mbona mambo mengi mmewaachia kama kuchimba madini, kuchimba gesi nk
 
Back
Top Bottom