CHAGOSI GERALD
Senior Member
- Jan 25, 2020
- 162
- 284
Watanzania wengi wanapenda kuamini kwamba vyama vya siasa ndio injini za maendeleo: CCM, CHADEMA, ACT-Wazalendo, CUF, TLP, ADA-orodha ndefu, matumaini machache. Wanapenda kufikiri kwamba mabadiliko yatatoka kwenye sanduku la kura, kana kwamba sanduku limebeba miujiza, sio majina ya watu walioshindwa kujenga hata familia zao.
Lakini ukweli ndio huu:
Vyama vya siasa Tanzania sio vyombo vya ukombozi, ni mawakala wa mataifa yenye maslahi.
CCM haiko peke yake.
CHADEMA haiko peke yake.
Vyote vina kamba shingoni, tofauti ni nani anashika mwisho wa kamba.
CCM-Wamarekani.
CHADEMA-Ulaya.
Vyama vidogo-kepusi za kujaza mazingira ya “demokrasia.”
Hii ndiyo demokrasia “tuliopewa” mwaka wa uhuru:
Viongozi watakuwa weusi, lakini uchumi utaendeshwa na masilahi ya nje.
Hivyo ndivyo Nyerere alivyopewa mfuko wa urithi: nchi yenye bendera, lakini uchumi wa wakoloni.
Lakini hapa ndipo watu wasiomjua Mwalimu wanamkosea.
Watu wanaomchukia bila kuelewa, na wanaomsifu bila kusoma vitabu vyake.
Ukiondoa mapungufu yake, kulikuwa na jambo moja ambalo Mwalimu aliliona kwa macho ya kinabii:
Ardhi ikitwaliwa na wageni, taifa limekufa.
Angalia Afrika Kusini-ardhi bado ina jina la wakoloni kwa karatasi.
Lakini Tanzania?
Hilo halikutokea kwa sababu mzee mmoja mwenye shati jeupe alisema: “Hapana.”
Watu walikufa, si kwa mapanga ya wananchi, bali kwa migongano ya kimfumo kati ya mabeberu waliokuwa wamejificha kwenye vyeo na madaraka.
Hapo ndipo Azimio la Arusha lilipozaliwa-silaha ya kupasua minyororo ya uchumi wa kikoloni.
Watu wengi hawajui:
Azimio la Arusha halikuwaua raia, liliua viongozi waliokuwa washirika wa mfumo wa ukoloni baadaye.
Huo ndio mchezo uliokuwa ukifanyika nyuma ya pazia.
Na kutoka humo, Mwalimu alizaa kitu kingine kikubwa kuliko vyote:
JKT.
JKT: Mwanzo wa Taifa, Sio Kambi ya Ajira
Mwalimu hakuiunda JKT kama sehemu ya kupitisha vijana ili wajifunze kupiga magoti, kufyeka nyasi na kupiga gwaride.
Hapana-hii ni tafsiri ya watu waliolikoroga taifa miaka 30 baadaye.
JKT iliundwa kuwa shina la uchumi, injini ya taifa, mahali ambapo vijana ndio wanageuza ardhi kuwa utajiri.
Mwalimu alijua:
Vijana ndio wanaobeba ubunifu - wazee wanabeba kumbukumbu.
Na kama taifa linataka kushindana na mataifa makubwa, lazima liweke uchumi mikononi mwa nguvu za vijana, sio mikononi mwa mabepari wachache wajuaji wanaoishi Peacock Hotel wakila mamilioni ya mikataba ya bandari na madini.
Ndio maana ndoto yake ilikuwa hii (ambayo ilivurugwa baada ya yeye kuondoka):
JKT imiliki:
Migodi
Mashule
Hospitali
Benki
Mashamba
Airlines
Viwanja vya ndege
Kampuni za usafirishaji
Media
Real estate
Labs na research centres
Supermarkets
Vikosi vya ujenzi
Na kila sekta inayohusisha uzalishaji
Ikiwa hii ingetekelezwa:
Tanzania ingekuwa taifa pekee Afrika lenye uchumi unaotegemea vijana, sio wawekezaji wa kutoka Dubai, Mumbai, au London.
Lakini nini kilitokea?
Vyama vya siasa vikaingia.
Wanasiasa wakageuka madalali.
Wakaikata JKT kwa makusudi-ili watumie vijana kama nguvu ya kampeni, sio nguvu ya uchumi.
Wakati huo huo wakaweka lugha za utapeli:
“Hii bandari imeshindwa kutuendesha, bora tumpe mwekezaji.”
“Kampuni hii imefilisika, si bora tuiuze?”
“Huu mgodi tunaweka ubia, Watanzania hawana uwezo wa kuendesha.”
Uongo mtupu.
Uongo wa kupaka shilingi mafuta ya mgongo wa chura ili iuzwe kama nyoka.
Uongo wa madalali wa kimataifa wanaoitwa ‘viongozi wa kizalendo.’
Kwa nini vyama haviwezi kuokoa Tanzania?
Kwa sababu vyama havimiliki uchumi.
Vinamiliki maneno.
Na kila chama kina mfadhili wa nje anayechonga ajenda kulingana na masilahi yake.
Kila chama kinachoingia madarakani huwa na msamiati uleule:
Ubinafsishaji
Uwekezaji wa nje
Soko huria
Ubia
Ni lugha ya kukabidhi mali ya taifa kwa mwekezaji huku wakilipa vijana milioni 700 kwa mwezi kwenye ajira hewa.
Hivyo Watanzania wanaingia kweny safari ya ‘mabadiliko ya kisiasa’ na kutoka upande mwingine wakiwa maskini zaidi.
Suluhisho?
Sio CCM.
Sio CHADEMA.
Sio uchaguzi.
Ni Mfumo.
Na mfumo pekee unaoweza kurejesha JKT kama injini ya taifa ni:
KATIBA MPYA.
Katiba inayotamka wazi:
Rasilimali zote zitasimamiwa na taasisi za umma zilizo chini ya vijana.
Hakuna sekta ya kimkakati inayoweza kuuzwa.
Uchumi unachochewa na uzalishaji wa vijana, sio wawekezaji wa nje.
Jeshi la kujenga taifa linakuwa nguzo ya viwanda, utafiti, kilimo, teknolojia na uchumi.
Uzalendo unarudishwa kama maadili ya taifa, sio nyimbo za kampeni.
Kwa katiba mpya ndipo taifa linatoka kwenye “uhuru wa bendera” na kuingia kwenye uhuru wa uchumi.
Kwa sasa tupo wapi?
Tupo katika taifa ambalo vijana wanangoja ajira hewa, wakati JKT yenyewe ilikuwa iwaajiri miaka 60 iliyopita.
Tupo katika taifa ambalo wanasiasa wanauza bandari kama wanauza shamba la babu yao.
Tupo katika taifa ambalo vyama vinaendeshwa kama franchise za mataifa makubwa.
Hii ndio sababu mfumo ndio tatizo, sio chama.
Lakini ukweli ndio huu:
Vyama vya siasa Tanzania sio vyombo vya ukombozi, ni mawakala wa mataifa yenye maslahi.
CCM haiko peke yake.
CHADEMA haiko peke yake.
Vyote vina kamba shingoni, tofauti ni nani anashika mwisho wa kamba.
CCM-Wamarekani.
CHADEMA-Ulaya.
Vyama vidogo-kepusi za kujaza mazingira ya “demokrasia.”
Hii ndiyo demokrasia “tuliopewa” mwaka wa uhuru:
Viongozi watakuwa weusi, lakini uchumi utaendeshwa na masilahi ya nje.
Hivyo ndivyo Nyerere alivyopewa mfuko wa urithi: nchi yenye bendera, lakini uchumi wa wakoloni.
Lakini hapa ndipo watu wasiomjua Mwalimu wanamkosea.
Watu wanaomchukia bila kuelewa, na wanaomsifu bila kusoma vitabu vyake.
Ukiondoa mapungufu yake, kulikuwa na jambo moja ambalo Mwalimu aliliona kwa macho ya kinabii:
Ardhi ikitwaliwa na wageni, taifa limekufa.
Angalia Afrika Kusini-ardhi bado ina jina la wakoloni kwa karatasi.
Lakini Tanzania?
Hilo halikutokea kwa sababu mzee mmoja mwenye shati jeupe alisema: “Hapana.”
Watu walikufa, si kwa mapanga ya wananchi, bali kwa migongano ya kimfumo kati ya mabeberu waliokuwa wamejificha kwenye vyeo na madaraka.
Hapo ndipo Azimio la Arusha lilipozaliwa-silaha ya kupasua minyororo ya uchumi wa kikoloni.
Watu wengi hawajui:
Azimio la Arusha halikuwaua raia, liliua viongozi waliokuwa washirika wa mfumo wa ukoloni baadaye.
Huo ndio mchezo uliokuwa ukifanyika nyuma ya pazia.
Na kutoka humo, Mwalimu alizaa kitu kingine kikubwa kuliko vyote:
JKT.
JKT: Mwanzo wa Taifa, Sio Kambi ya Ajira
Mwalimu hakuiunda JKT kama sehemu ya kupitisha vijana ili wajifunze kupiga magoti, kufyeka nyasi na kupiga gwaride.
Hapana-hii ni tafsiri ya watu waliolikoroga taifa miaka 30 baadaye.
JKT iliundwa kuwa shina la uchumi, injini ya taifa, mahali ambapo vijana ndio wanageuza ardhi kuwa utajiri.
Mwalimu alijua:
Vijana ndio wanaobeba ubunifu - wazee wanabeba kumbukumbu.
Na kama taifa linataka kushindana na mataifa makubwa, lazima liweke uchumi mikononi mwa nguvu za vijana, sio mikononi mwa mabepari wachache wajuaji wanaoishi Peacock Hotel wakila mamilioni ya mikataba ya bandari na madini.
Ndio maana ndoto yake ilikuwa hii (ambayo ilivurugwa baada ya yeye kuondoka):
JKT imiliki:
Migodi
Mashule
Hospitali
Benki
Mashamba
Airlines
Viwanja vya ndege
Kampuni za usafirishaji
Media
Real estate
Labs na research centres
Supermarkets
Vikosi vya ujenzi
Na kila sekta inayohusisha uzalishaji
Ikiwa hii ingetekelezwa:
Tanzania ingekuwa taifa pekee Afrika lenye uchumi unaotegemea vijana, sio wawekezaji wa kutoka Dubai, Mumbai, au London.
Lakini nini kilitokea?
Vyama vya siasa vikaingia.
Wanasiasa wakageuka madalali.
Wakaikata JKT kwa makusudi-ili watumie vijana kama nguvu ya kampeni, sio nguvu ya uchumi.
Wakati huo huo wakaweka lugha za utapeli:
“Hii bandari imeshindwa kutuendesha, bora tumpe mwekezaji.”
“Kampuni hii imefilisika, si bora tuiuze?”
“Huu mgodi tunaweka ubia, Watanzania hawana uwezo wa kuendesha.”
Uongo mtupu.
Uongo wa kupaka shilingi mafuta ya mgongo wa chura ili iuzwe kama nyoka.
Uongo wa madalali wa kimataifa wanaoitwa ‘viongozi wa kizalendo.’
Kwa nini vyama haviwezi kuokoa Tanzania?
Kwa sababu vyama havimiliki uchumi.
Vinamiliki maneno.
Na kila chama kina mfadhili wa nje anayechonga ajenda kulingana na masilahi yake.
Kila chama kinachoingia madarakani huwa na msamiati uleule:
Ubinafsishaji
Uwekezaji wa nje
Soko huria
Ubia
Ni lugha ya kukabidhi mali ya taifa kwa mwekezaji huku wakilipa vijana milioni 700 kwa mwezi kwenye ajira hewa.
Hivyo Watanzania wanaingia kweny safari ya ‘mabadiliko ya kisiasa’ na kutoka upande mwingine wakiwa maskini zaidi.
Suluhisho?
Sio CCM.
Sio CHADEMA.
Sio uchaguzi.
Ni Mfumo.
Na mfumo pekee unaoweza kurejesha JKT kama injini ya taifa ni:
KATIBA MPYA.
Katiba inayotamka wazi:
Rasilimali zote zitasimamiwa na taasisi za umma zilizo chini ya vijana.
Hakuna sekta ya kimkakati inayoweza kuuzwa.
Uchumi unachochewa na uzalishaji wa vijana, sio wawekezaji wa nje.
Jeshi la kujenga taifa linakuwa nguzo ya viwanda, utafiti, kilimo, teknolojia na uchumi.
Uzalendo unarudishwa kama maadili ya taifa, sio nyimbo za kampeni.
Kwa katiba mpya ndipo taifa linatoka kwenye “uhuru wa bendera” na kuingia kwenye uhuru wa uchumi.
Kwa sasa tupo wapi?
Tupo katika taifa ambalo vijana wanangoja ajira hewa, wakati JKT yenyewe ilikuwa iwaajiri miaka 60 iliyopita.
Tupo katika taifa ambalo wanasiasa wanauza bandari kama wanauza shamba la babu yao.
Tupo katika taifa ambalo vyama vinaendeshwa kama franchise za mataifa makubwa.
Hii ndio sababu mfumo ndio tatizo, sio chama.
Attachments
-
Picsart_25-12-01_05-08-02-841.jpg225.1 KB · Views: 10 -
Picsart_25-12-01_05-08-02-841.jpg225.2 KB · Views: 10 -
Picsart_25-12-01_05-27-18-980.jpg265.6 KB · Views: 11 -
Picsart_25-12-01_05-12-24-225.jpg204.9 KB · Views: 9 -
Picsart_25-12-01_05-17-25-309.jpg198 KB · Views: 8 -
Picsart_25-12-01_05-20-12-182.jpg295 KB · Views: 11 -
Picsart_25-12-01_05-24-39-933.jpg286.9 KB · Views: 8