Ni tarehe 10 June 2018 namfikisha mwanangu amevunjika mkono ili apatiwe tiba. Tunalipia kila kitu natoka kulipia nakutana na Mama mmoja analia mwanae mkono wake umeunga vibaya baada ya kutibiwa hapo hapo na wamenwambia akalipie wauvunje wauunge tena.
Nafika kwa dokta muhusika namkuta Dada mwingine na mwanae wa miaka 3 nae mkono umeunga vibaya inabidi nae wauvunje waunge upya. Najipa moyo nikisema bahati mbaya. Mwanangu anafungwa POP naambiwa rudi baada ya siku 14.
Tarehe 25 June 2018 narudi POP inatolewa X Ray majibu mkono umeunga vibaya. Inabidi tuuvunje tuunge upya!! MMMH. Watoto hawa ni 2-5 years.
Jamani hii ni biashara au nini? Nidhamu iko wapi?
Naomba Advocate humu niwashtaki Lugalo Hospital. Sasa hivi naelekea MOI tu ila nina uchungu sana.
======
UPDATES: 14 Julai 2018
Habari hii imekanushwa..
Jeshi la Ulinzi la wananchi wa Tanzania limekanusha taarifa zilizosambazwa kupitia mitandao ya kijamii kuhusu malalamiko juu matibabu ya mtoto anayedaiwa kuvunjika na kupatiwa huduma katika Hospitali kuu ya jeshi ya Lugalo.
Akizungumza na waandishi wa habari Leo Jijini Dar es Salaam msemaji mkuu wa Jeshi Kanali Ramadhani Dogoli alimtaka aliyejinasibisha kama mlalamikaji kuwasilisha malalamiko yake kama yana ukweli ili hatua zichukuliwe kwa wahusika.
“ Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania JWTZ linamtaka malalamikaji alete taarifa kwenye uongozi ili kama matukio hayo yametokea tuweze kuchukua hatua kwa wahusika” Alisema kanali Dogoli.
Aliongeza kuwa iwapo aliyedai kulalamika atashindwa kufanya hivyo jeshi litaaamini kuwa mlalamikaji alikusudia kuichafua hospitali yetu kwa maslahi binafsi na kwa sababu hiyo tutamtafuta haraka na kumchukulia hatua zinazomstahili.
Nafika kwa dokta muhusika namkuta Dada mwingine na mwanae wa miaka 3 nae mkono umeunga vibaya inabidi nae wauvunje waunge upya. Najipa moyo nikisema bahati mbaya. Mwanangu anafungwa POP naambiwa rudi baada ya siku 14.
Tarehe 25 June 2018 narudi POP inatolewa X Ray majibu mkono umeunga vibaya. Inabidi tuuvunje tuunge upya!! MMMH. Watoto hawa ni 2-5 years.
Jamani hii ni biashara au nini? Nidhamu iko wapi?
Naomba Advocate humu niwashtaki Lugalo Hospital. Sasa hivi naelekea MOI tu ila nina uchungu sana.
======
UPDATES: 14 Julai 2018
Habari hii imekanushwa..
Jeshi la Ulinzi la wananchi wa Tanzania limekanusha taarifa zilizosambazwa kupitia mitandao ya kijamii kuhusu malalamiko juu matibabu ya mtoto anayedaiwa kuvunjika na kupatiwa huduma katika Hospitali kuu ya jeshi ya Lugalo.
Akizungumza na waandishi wa habari Leo Jijini Dar es Salaam msemaji mkuu wa Jeshi Kanali Ramadhani Dogoli alimtaka aliyejinasibisha kama mlalamikaji kuwasilisha malalamiko yake kama yana ukweli ili hatua zichukuliwe kwa wahusika.
“ Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania JWTZ linamtaka malalamikaji alete taarifa kwenye uongozi ili kama matukio hayo yametokea tuweze kuchukua hatua kwa wahusika” Alisema kanali Dogoli.
Aliongeza kuwa iwapo aliyedai kulalamika atashindwa kufanya hivyo jeshi litaaamini kuwa mlalamikaji alikusudia kuichafua hospitali yetu kwa maslahi binafsi na kwa sababu hiyo tutamtafuta haraka na kumchukulia hatua zinazomstahili.