Uhamiaji wazidi kutafuna posho zaidi

Uhamiaji wazidi kutafuna posho zaidi

mgonjwa

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2013
Posts
514
Reaction score
223
attachment.php
Wakati wahanga wa nafasi za konstebo na koplo wa uhamiaji wakisubiri hatma yao wizara husika imeiongezea siku zaidi za uchunguzi kamati hiyo baada ya kushindwa kukamilisha kazi waliyopewa kwa wakati ambao ni siku kumi !! Tume hiyo imeomba iongezewe muda zaidi ambao haujaweka wazi ni siku ngapi hiii ni ishara ya wao pia kuendelea kula posho kama wanafanya wengine kule dodoma !! Subira yavuta heri tuendelee kusubiri


Chanzo: Mwananchi
 

Attachments

  • 1407910552666.jpg
    1407910552666.jpg
    48.4 KB · Views: 775
wapewe tu muda wa kutosha vizuri tena waweze kuja na majibu mazuri ila sitegemei kama watu wataomba upya kwa hali hii wanakuja wengine wale wanasubiri wao.maskin jaman wenye moyo na nia pia wito wa dhati wanasubiri
 
Uzembe wa wachache umegharimu wengine wasiohusika.... Mbona kila kitu kipo wazi, sasa kinachocheleweshwa hapo ni nini kisichoweza kutolewa majibu..?
 
Mkuu kilichopo wazi ni kipi kamanda sijaelewa statement yako...mana inaonesha unaufahamu ukweli mpaka kusema kila kitu kipo wazi...tukikuita utoe maelezo utaweza kutuonesha uwazi uko wapi..
 
duh we jamaa mbona umewakomalia hivyo uhamiaji,kwani kazi ni hiyo tu?
 
Wakati wahanga wa nafasi za konstebo na koplo wa uhamiaji wakisubiri hatma yao wizara husika imeiongezea siku zaidi za uchunguzi kamati hiyo baada ya kushindwa kukamilisha kazi waliyopewa kwa wakati ambao ni siku kumi !! Tume hiyo imeomba iongezewe muda zaidi ambao haujaweka wazi ni siku ngapi hiii ni ishara ya wao pia kuendelea kula posho kama wanafanya wengine kule dodoma !! Subira yavuta heri tuendelee kusubiri
source mwananchi la leo !!!

Mimi muda mwingine huwa nashindwa kuwaelewa utashi na IQ za sisi binadamu. Hivi kweli mambo ya msingi yanafanywa kama ya masihara kwa kuunda kamati ya uchunguzi kutoka ofisi hizo hizo za maofisa walioharibu katika kutoa ajira kwa watoto/ndugu zao. Ama kweli ule usemi kwamba Mbuzi kafia kwa mama muuza supu!
 
uchunguzi wa nini tena?, mbona tumeshapangiwa vituo vya kazi?
 
Watu wanalindana hapo wameshachunguza na ukweli wanao sasa kilichobaki ni kulindana kwa mtindo wa kuvuta muda ili kushusha tension
 
Kwa upande wangu naona ni vema waongezewe muda wa kutosha ili waweze kukamilisha uchunguzi vizuri..nyie si mnasema mnataka haki itendeke sasa unadhani kuwa wasipochunguza vizuri watabaini vipi ukweli..binafsi naona kama siku kumi zilikuwa chache kiukweli ukiangalia process ni ndefu ya uchunguzi ukizingatia mazingira ya uwazi na ushirikiano kutoka kwa watu wa idara husika..unadhani uhamiaji watatoa ushirikiano kwenye huo uchunguzi wakati ni sawa na kujichimbia kaburi...mimi naomba kamati isikurupuke mana nao pia wanaweza kuingia matatizoni..Takukuru wanaweza sema hawakuridhika na uchunguzi hivyo wanataka wafanye wenyewe mwisho wa siku mambo yakaharibika tena..hivyo kama tunataka haki itendeke kwa wadogo zetu hatuna budi kuwa na subira ili waje na majibu ya kweli..we should not jump into conclusion very easy like that pengine ni kweli kuwa bado wanapitia mafile ya wasailiwa wote na bado hawajapata ushirikiano wa kutosha..LET US WAIT.
 
Kwani shida hapo ni nini maana hata muda wa depo bafo hadi mwezi wa 10 mana intake nyingi huwa zinaingia mwezi wa kumi CCP hadi mwezi wa 10 mwakani ndo inatoka..depo la polisi lita passout tar.15/09 kwaiyo hapo maandalizi ya intake nyingine yataanza..so tulieni tusubiri mpaka kamati itoe maamuzi..Mimi binafsi naiamini hiyo kamati kwa kiasi kikubwa mana namuamini Abdul Wakil na najua atakuwa ameteua watu makini kikubwa tujenge imani juu ya kamati husika...UCHUNGUZI MAKINI KWA MATOKEO MAKINI..Kumbukeni ile ni kashfa kubwa sana kwa nchi huwezi toa siku kumi halafu including na weekend..watu waache kusali jmos na j2 wakachunguze tuhuma kubwa namna hiyo..watu 200 upitie wote. washukiwa pamoja na watoto wa wakulima..ubaini upendeleo kisha uandike report na maamuzi yafanyike sio kazi ndogo kusema ukweli..WENYE HAKI WATAPEWA HAKI YAO
 
Mkuu kwani wewe ulitaka nani aunde kamati na itoke wapi hiyo kamati ya uchunguzi..sikia hata kama kamati ingetoka eneo lisilo na uhusiano na uhamiaji kama imeridhia kutenda haki itatenda tu na kama imenuia kuupindisha ukweli watafanya hivyo..nikupe mfano kamati ya kudumu ya ardhi bungeni iliyokuwa na wajumbe 9 na Lembeli(Mb-CCM) alikuwa m/kiti iliyokuwa inachunguza tuhuma za ukiukwaji wa haki za binadamu kwenye operesheni tokomeza ujangili..Kamati haikumlinda mtu yeyote japokuwa mawaziri walikuwa ni wa CCM ila walichukuliwa hatua..sasa katika hili nadhani ni suala la commitment kwa wajumbe husika kutenda haki..
 
wakichunguza ukweli mnawabeza wanakula posho, muwape mda wa kukamilisha kazi nzuri tuone wenye nacho wataongezewa na wasio nacho watabakia kuwa wapambe wao wenye kuongezewa
 
Mgonjwa mwaka huu lazima ufe kwa sononeko

...kwani HUKUMU ya TUME ishatoka? Na kama wamewafutilia mbali watoto wa WAKULIMA waliopita kwa jitihada za vigezo stahiki watakuwa wamefanya UONEVU ambao dunia nzima itawalaani na mengineyo yanaweza kutokea... N.b. Mwanafunzi 4m4 alijinyonga kwa uzembe wa NECTA.
 
Back
Top Bottom