Uhamiaji pitieni hapa

bora hao wabongo wanaajira za kudumu huku kwa mengi sis ni vibarua na wapakiaji masanduku ya vyoda sehem zenye tija wahindi ndo wapo na wakenya
Sisi waajiriwa tumeongezewa mshahara. Vipi nyinyi vibarua bado mnalipwa 5000 kwa siku? Hawajawaongezea?
 
Uhamiaji na maafisa kazi wa mkoa wa.dsm wanahitaji kutumbuliwa. Huwa ninapitiaga sea cliff casino, le grand na hii casino ya waturuki hapa IT PLAZA.

Pale wamejaa foreigners mpaka waitress, acha dada zetu wanaojiuza kutoka thailand,nepal na uturuki. Hivi unaweza kuamini kuna labour officer na hawa uhamiaji hawazijui hizi ofisi kama zina wageni wasio na vibali.

Kuna pesa nyingi ya serikali wanaikwepa hawa watu.
 
what you say is true
 
Dawa ni kususa hicho kinywaji cha Cocacola.
 
High Spirit??
 


Inasikitisha lakini tuangalie hali halisi kwanza. Wabongo wengi ni magumashi when it comes to kufanya kazi. Sisi ni wavivu na watoro wa kazi, wazembe, waongo, na wengi wetu hawana ujuzi wa kazi na wana vyeti bandia.

Najuwa wengi wenu mtakasirika ila hizi habari alinitonya mtu muhimu sana maishani mwangu nami nilipo chunguza nikaona ukweli wake. Utakuta mtu kaajiriwa serikalini ila hana taaluma yeyote na hajuwi why yuko pale.

Matokeo yake raia unakwenda tafuta huduma unamkuta mtu yuko bize kwenye Istagram na Fesibuku wakati wa kazi na watu kibao wamejaa kusubiri huduma, ukiuliza huduma anakuambia anayeshughulika na hilo suala katoka kumbe ni yeye mwenyewe ila anashindwa tu kukuambia kuwa yuko incompetent.

Kingine, utakuta mtumishi wa serikali asiyejuwa jukumu lake, anakwenda kazini kusaini tu kisha anarudi kwenye mataptap, muda wa kazi kwisha ukikaribia ndipo anarudi kusaini out. Who needs to hire ppl like these?

We need to change our mentality ya kupenda kufanya kazi bila visingizio na wizara husika kuajiri watu wenye ufanisi na waliosoma si tu watoto wa mjomba na kutuletea madhara haya tuliyonayo sasa ya uzembe na uvivu.

Haya makampuni ya kigeni yanajuwa kuwa watanzania ni wazembe na waongo ndiyo maana hawataki ku deal nasi. Je, hata kama wewe mleta mada ni muwekezaji hapa nchini, utapenda kuwekeza kwa watu wavivu na wazembe?

Nini lengo lako la kuwekeza, kuingiza pesa au kujipa hasara? Mi nasema, rais Magufuli atumbue watu wa dizaini hii serikalini, wanatuhaibisha watanzania.
 
Kwani wewe ulikubali bei gani? Sasa km umeona wengine walioshawishi kupewa zaidi kinakuuma nini?

Ndio ubepari huo, km wapo mataifa mengi ni wazi kwamba kwamba hapo ni wewe tuu ulipoingia. Km una akili ya kijamaa ni wazi uliomba kazi ukajichekesha kwa boss usimuudhi, wakati nae anataka bei rahisi iwezekanvyo.

Na km hadi sasa hujaweza thibitisha umuhimu wako ili sasa urudi mezani kupatana nyongeza, unachofanya hapa hakitowasaidia sana watz wavivu.
 
Unadhani kinachofanya awe buzz na mambo mengine ni uvivu? Najua kuna mambo mengi sana yanayowakatisha tamaa wafanyakazi wengi Wa serikali. Miongoni mwa hayo ni vipato duni. Hii imekuwa chanzo cha kukata tamaa ya kazi na bahati mbaya viongozi wetu wengi hawalioni hili wanaongelea uvivu. Graduate anamaliza chuo anaanza na gross lk saba. Ataishia kukata tamaa tu na kuona lzm afanye mengine kupata kipato. Nadhani hili suala lisichukuliwe kijuujuu tu. Watalaamu wa human resource wanayajua haya.

Nimefanya kazi private na public sector. Private sector wageni wanapewa mshahara mkubwa sana ikilinganishwa na wenyeji ingawa mara nyingi kazi kubwa hufanywa na wenyeji. Nimeshafanya kazi na org moja dada moja wa nchi jirani yeye alikuwa mzuri wa kuongea na hasa lugha ya wenzetu, lkn kwenye evaluation atakwambia anatengeneza strategies. Wenye mradi walimwamini sana wakampa cheo cha kuwa makamu mkuu Wa mradi lkn baadae wakagundua hakuna chochote anacho deliver na wakamshusha madaraka.

Najua wapo watanzania wengi wavivu km walivyo watu toka nchi zingine lkn mazingira yana nafasi kubwa sana ya kutengeneza tuweje
 
Uzalendo ndio ubaguzi wenyewe ila ni wa kitaifa. Huwezi kuwa mzalendo wa kweli bila kuwa mbaguzi.
 
hapa ni nini hasa..wivu wa watu kulipwa laki sita ya chakula au?

hio ni kampuni binafsi arif
Wewe freeland kama unavyojiita una lako jambo! Kwenye post mbali mbali tumeshakuona Kila Kinachoongelewa wewe kazi yako ni KUPINGA, KUFANYA MAJUNGUKUFITINISHAKUCHONGANISHA,KUKEJELI. NA MAMBO YOTE MABAYA. WEWE UMETUMWA NA SI M TANZANIA UNATAKA TWENDE PABAYA. WEWE SI MWENZETU. WE MBAYA NA WAKUOGOPWA KAMA UKOMA. UTUACHE NA TANZANIA YETU KAFILIE MBALI
 
jitumeni acheni ku panic bila sababu...ninyi competence zero unategemea nani akuajiri...kwa taarifa yako Coca-Cola kwanza ni Ya mengi...hadi kufikia kuajiri wageni ninyi ni incompetent. ...

Sawa lakini afuate basi utaratibu maana utambuzi wa wageni na stahili zao ni muhimu miaka hii mkuu wangu, mfano Mgeni mwenye Residence permit class A, B na exemptions certificate i hope wote hao hawastahili exemptions, stahili zao zijulikane vilevile itapelekea kujua working permit zao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…