Uhamiaji bado kuna tatizo kubwa sana

Uhamiaji bado kuna tatizo kubwa sana

Kama kawaida watu wa kanda (maalum) ya ziwa huwa tunasahau hata salamu hivyo naenda moja kwa moja kwenye mada,
Kumekuwa na malalamiko mengi kuhusu vitabu vya hati ya kusafiria, kila mtu anasema lake leo nimekosa kazi nikaenda mapema kujionea makao makuu ya uhamiaji kurasini Dar es salaam, nilikaa kwa masaa mawili nikagundua yafuatayo vile vibanda vya kutoa copy pale nje ni biashara cover up kiuhalisia wale bila kumung'unya maneno nawaita mawakala wa pass port, niliingia duka la kwanza kutoa copy nikakuta kuna watu kadhaa nao wana subiri huduma hiyo yule dada mtoa copy anaongea na simu nanukuu "unataka express ama ya kawaida, kama ni express ni laki tatu inatoka ndani ya wiki" mwisho wa kunukuu yaani alikuwa anaongea bila uwoga na kwa ujasiri ukiangalia dukani humo kuna watu wengi kila mmoja anakukaribisha tena wababa wazima nikabahatika kumuona mmoja anamuhuri wa mwanasheria tayari kwa kutengeneza affidavity sh 15000.

Nikatoka nikaenda duka la pili baada ya kuona pale kuna msururu wa watu yule dada alikuwa ananitolea copy huku ameweka simu masikioni naye anaongea na mtu "ya wiki ni laki 3, wiki mbili laki 2 ya kawaida laki na nusu, kwa wewe unayesafiri haraka ntakupa hii ya laki tatu hiyo haipungui na kama uko serious njoo haraka manake naenda kumuona afisa mkubwa" kilichokuwa kinaendelea pale ni kwamba watu waliokuwa wanafika pale uhamiaji kwa ajili ya ku process passport wanaanza kupokelewa kwa kukatishwa tamaa na yule ndugu anayekaa pale kwenye dawati la huduma kwa wateja hivyo wanashawishika kurudi pale kwa wale watoa copy nje.

Swali langu kama mimi niliyeenda pale kwa mara moja nimejionea hayo niliyoona, hakuna wahusika ambao wanajua kuna biashara hii haramu? na je nani ni wanufaika wa mradi huu. Ntakuwa nikileta mrejesho ambapo kwa ukiwepo ushahidi wa picha na video Kama kuna watu wamekataa kuwajibika ngoja sasa tuwawajibishe [HASHTAG]#unokoniuzalendo[/HASHTAG]
Mi pass yangu nimechukulia mkoani wala haikuwa nanshida yoyote.

Nimejaza fomu nikasubiria siku 30 nikaitwa kuichukua. Nikawahamasisha na wenzangu nao wakajaza wakapata bila kikwazo.

Mi nadhani tatizo la dar ni msongamano unaosababishwa na uhitaji mkubwa
Mi niliwaambia nataka kwenda kusoma nje hivyo nimekwama kuendelea na application wanataka pasipoti namba na kwenye barua nilijieleza
...
.....,
 
Kama hauamini basi .sikulazimishi.
Mimi sijaleta hyo mada.
Ila nilishawahi kwenda kuomba passport niende cape town kuhangaika na maisha.form niliyopewa na viambatanisho nilivyokutana navyo ni kikwazo tosha.
Ukiomba passport kwa safari yoyote kuna viambatanisho vyake.na vyote vitimie.
Watanzania wengi tuna shida sana. Labda nikwambie kitu, Passport ni kitambulisho cha raia wa kigeni ndani ya nchi ambayo mwenye pasipoti sio raia. Pamoja na kwamba pasipoti anapewa mtu lakin bado inabaki ni mali ya serikali kwa maana matumizi ya hio pasipoti yaendane na kufuata sheria na taratibu za kiuhamiaji kwa nchi unayokwenda.

Sasa pamoja na kwamba pasipoti ni haki ya kila raia lakin lazima ukidhi vigezo vilivyowekwa kisheria ili kuweza kupatq pasipoti. Pamoja na kuambatanisha vyeti vya kuzaliwa, afidavit na vitambulisho vyote lakin lazima ulete documents za MADHUMUNI ya safari ambazo wengi hapo huwa wanakwama.

Madhumuni ya safari ndio yanayopelekea raia wa Tanzania upewe pasipoti kwani sio kitambulisho cha kukaa nacho ndani ni kitambulisho chako ukiwa nje ya nchi.

1.Madhumuni yanaweza kuwa ni Matembezi Binafsi hapa utatakiwa kuleta bank statement ili kujiridhisha kuwa huko uendako hutoigharimu serikali kukuridisha nchini baada ya kuwa Destitute huko. Binafsi ingine unaweza kuwa unaenda kumtembelea nduguyo nje ya nchi hivyo utatakiwa kuleta barua ya mwaliko na pasipoti na permit ya nduguyo huko aliko kama ni mtanzania, kama ni raia wa huko basi anatakiwa aandike barua ya mwaliko pamoja na kitambulisho cha uraia wake au paspoti.

2. Madhumini ya kibiashara unatakiwa kuwa na leseni na tin namba

3. Madhumini ya kimasomo unatakiwa kuwa na admission letter toka chuo unachokwenda kusoma.

4. Madhumini ya kidini, barua ya bakwata kwa mahujaji na barua zingine toka taasisi za kidini kama kanisani kwa ziara za kwenda israel.

Mengine utaongezea na ww ila jua kuwa vijana wengi wanadanganya wamealikwa na ndugu zao arabuni kumbe wanaenda kuwa watumwa wa kingono na mahausigeli tu. Watanzania wengi wanaoenda Sauzi wanakuwa mapusha na mateja kiti kinachoitia aibu serikali kila mara na pia kuigharimu kuwaridisha nchini.
 
Kama hauamini basi .sikulazimishi.
Mimi sijaleta hyo mada.
Ila nilishawahi kwenda kuomba passport niende cape town kuhangaika na maisha.form niliyopewa na viambatanisho nilivyokutana navyo ni kikwazo tosha.
Ukiomba passport kwa safari yoyote kuna viambatanisho vyake.na vyote vitimie.
Watanzania wengi tuna shida sana. Labda nikwambie kitu, Passport ni kitambulisho cha raia wa kigeni ndani ya nchi ambayo mwenye pasipoti sio raia. Pamoja na kwamba pasipoti anapewa mtu lakin bado inabaki ni mali ya serikali kwa maana matumizi ya hio pasipoti yaendane na kufuata sheria na taratibu za kiuhamiaji kwa nchi unayokwenda na nchi yako ikikuombea ulinzi pindi uwapo nchi ya kigeni.

Sasa pamoja na kwamba pasipoti ni haki ya kila raia lakin lazima ukidhi vigezo vilivyowekwa kisheria ili kuweza kupatq pasipoti. Pamoja na kuambatanisha vyeti vya kuzaliwa, afidavit na vitambulisho vyote lakin lazima ulete documents za MADHUMUNI ya safari ambazo wengi hapo huwa wanakwama.

Madhumuni ya safari ndio yanayopelekea raia wa Tanzania upewe pasipoti kwani sio kitambulisho cha kukaa nacho ndani ni kitambulisho chako ukiwa nje ya nchi.

1.Madhumuni yanaweza kuwa ni Matembezi Binafsi hapa utatakiwa kuleta bank statement ili kujiridhisha kuwa huko uendako hutoigharimu serikali kukuridisha nchini baada ya kuwa Destitute huko. Binafsi ingine unaweza kuwa unaenda kumtembelea nduguyo nje ya nchi hivyo utatakiwa kuleta barua ya mwaliko na pasipoti na permit ya nduguyo huko aliko kama ni mtanzania, kama ni raia wa huko basi anatakiwa aandike barua ya mwaliko pamoja na kitambulisho cha uraia wake au paspoti.

2. Madhumini ya kibiashara unatakiwa kuwa na leseni na tin namba

3. Madhumini ya kimasomo unatakiwa kuwa na admission letter toka chuo unachokwenda kusoma.

4. Madhumini ya kidini, barua ya bakwata kwa mahujaji na barua zingine toka taasisi za kidini kama kanisani kwa ziara za kwenda israel.

Mengine utaongezea na ww ila jua kuwa vijana wengi wanadanganya wamealikwa na ndugu zao arabuni kumbe wanaenda kuwa watumwa wa kingono na mahausigeli tu. Watanzania wengi wanaoenda Sauzi wanakuwa mapusha na mateja kiti kinachoitia aibu serikali kila mara na pia kuigharimu kuwaridisha nchini.
 
Kweli kabisaaaa. CCM na Rushwa ni sawa na Uhamiaji na Passport. Nashangaa Uhamiaji wanatoa work permit kwenye NGOs Yaani unakuta NGO ina foreigners kibao ambao wangeweza Kurudi kwao tu
Naomba ufahamu kuwa Kibali cha kufanya kazi kinatolewa na Wizara ya Kazi, akishapata kibali cha kufanya kazi anakuja Uhamiaji kuomba Residency permit
 
WaTz tunapenda kulalamika bila kucheck ground na ile form imeandikwa kabisa ijazwe na mhusika na imetaja mahitaji kadri ya nia ya safari ya mhusika ila kwenye hiyo kutoka kwa pasipoti siku 7 au 14 limekaa ki siasa zaidi kwa sababu kuna uvumi ulikuwa unazagaa kuwa hakuna vile vijitabu watu wamekaa muda mrefu sana bila kupata pass zao mpaka leo watumishi wenzangu hawajapata pasipoti zao na miezi kama mitatu
Kweli hata mie nilisikia kuna tatizo la uhaba wa vitabu na hili sio la uhamiaji peke yao kwani hata TRA mwaka jana walitoa Press Release kuwa hawana kadi za kutengenezea Leseni. Na hata polisi waliwahi kulalamikiwa kuwa hawana vitabu vya Notifications na vitabu vya risiti japo nilisikia tu kwa madereva sina hakika kwa kuwa mara nyingi vyombo vya ulinzi na usalama huwa havianiki mambo yao hadharani
 
Kweli hata mie nilisikia kuna tatizo la uhaba wa vitabu na hili sio la uhamiaji peke yao kwani hata TRA mwaka jana walitoa Press Release kuwa hawana kadi za kutengenezea Leseni. Na hata polisi waliwahi kulalamikiwa kuwa hawana vitabu vya Notifications na vitabu vya risiti japo nilisikia tu kwa madereva sina hakika kwa kuwa mara nyingi vyombo vya ulinzi na usalama huwa havianiki mambo yao hadharani
Hata kama ni vyombo vya ulinzi na usalama kama inahudumia raia basi watoe Tanganzo kujurisha tatizo kwenye umma kuliko kukaa kimya mpaka waliowahudumia huku mikoani tunahisi wamekula hela.Mi nahisi hili linahusishwa na kulinda image ya kuwa huyu bwana kaja kashindwa kuhudumia wananchi wake na hivyo mnamsuport kwa kutoeleza kinachowasibu.Kama bajeti ametoa ndogo nyie elezeni tu jamii kuwa capacitor yetu kutoa pass kwa mwezi ni kiasi fulani once vikiisha toeni chapisho kuiambia jamii la sivyo jamii tutaona kama hujuma tu zimeandaliwa ili tupigwe mpunga.
 
Watanzania wengi tuna shida sana. Labda nikwambie kitu, Passport ni kitambulisho cha raia wa kigeni ndani ya nchi ambayo mwenye pasipoti sio raia. Pamoja na kwamba pasipoti anapewa mtu lakin bado inabaki ni mali ya serikali kwa maana matumizi ya hio pasipoti yaendane na kufuata sheria na taratibu za kiuhamiaji kwa nchi unayokwenda.

Sasa pamoja na kwamba pasipoti ni haki ya kila raia lakin lazima ukidhi vigezo vilivyowekwa kisheria ili kuweza kupatq pasipoti. Pamoja na kuambatanisha vyeti vya kuzaliwa, afidavit na vitambulisho vyote lakin lazima ulete documents za MADHUMUNI ya safari ambazo wengi hapo huwa wanakwama.

Madhumuni ya safari ndio yanayopelekea raia wa Tanzania upewe pasipoti kwani sio kitambulisho cha kukaa nacho ndani ni kitambulisho chako ukiwa nje ya nchi.

1.Madhumuni yanaweza kuwa ni Matembezi Binafsi hapa utatakiwa kuleta bank statement ili kujiridhisha kuwa huko uendako hutoigharimu serikali kukuridisha nchini baada ya kuwa Destitute huko. Binafsi ingine unaweza kuwa unaenda kumtembelea nduguyo nje ya nchi hivyo utatakiwa kuleta barua ya mwaliko na pasipoti na permit ya nduguyo huko aliko kama ni mtanzania, kama ni raia wa huko basi anatakiwa aandike barua ya mwaliko pamoja na kitambulisho cha uraia wake au paspoti.

2. Madhumini ya kibiashara unatakiwa kuwa na leseni na tin namba

3. Madhumini ya kimasomo unatakiwa kuwa na admission letter toka chuo unachokwenda kusoma.

4. Madhumini ya kidini, barua ya bakwata kwa mahujaji na barua zingine toka taasisi za kidini kama kanisani kwa ziara za kwenda israel.

Mengine utaongezea na ww ila jua kuwa vijana wengi wanadanganya wamealikwa na ndugu zao arabuni kumbe wanaenda kuwa watumwa wa kingono na mahausigeli tu. Watanzania wengi wanaoenda Sauzi wanakuwa mapusha na mateja kiti kinachoitia aibu serikali kila mara na pia kuigharimu kuwaridisha nchini.
Mleta mada.ana tatizo na zile fremu.sio utaratibu wa Uhamiaji.
 
Shida watanzania wagumu kufuata utaratibu, mtu anakata passport hadi inaisha hajaenda hata burundi arafu anataka nyingine
Sababu ya safari hana pia yeye anataka aende tu kama wale walioenda airport kutaka kwenda israel bila visa wala
Me nadhani ukikamilisha vigezo hautosumbuliwa
 
Watanzania sisi tulizoeshwa short cut hivyo wengi ni wavivu kuvikamilisha vigezo na hapo ndipo unafungua milango ya kupigwa mpunga.We kams umeambiwa katoe photocopy then njoo na barua ya mtendaji then unaanza kulia lia aa bwana huwezi kumaliza vyote huko mi sipendi mambo ya nenda rudi utajikuta unapigwa cha juu.Mi nilipewa maagizo nikatimiza tena niliyaandika kabisa sasa hapo ataniomba rushwa kwenye nini?
 
Hata mie sijawahi kutoa rushwa. Ila siku zote ukitaka kwenda nje ya utaratibu ujue unakaribisha rushwa
Watanzania wengi ZIMAMOTO. Na wengi ujuaji mwingi, tena aiku hiz ndo kujazia online hizo application bado nashangaa watu wanatoa rushwa. Maajabu haya. Sitoi rushwa, hata makosa ya barabarani, kama nina kosa niandikie faini nilipe.
 
Shida watanzania wagumu kufuata utaratibu, mtu anakata passport hadi inaisha hajaenda hata burundi arafu anataka nyingine
Sababu ya safari hana pia yeye anataka aende tu kama wale walioenda airport kutaka kwenda israel bila visa wala
Me nadhani ukikamilisha vigezo hautosumbuliwa
Uko sahihi kabisa. Jamaa yangu mmoja pasipoti yake aliomba 2005 akiadai anaenda kibiashara China, mwaka jana kaenda ku-renew hana hata mhuri mmoja yaani hajawai kusafiria, wakamkatalia hadi aje na sababu ingine maana miaka 10 hajaitumia.
 
Hata kama ni vyombo vya ulinzi na usalama kama inahudumia raia basi watoe Tanganzo kujurisha tatizo kwenye umma kuliko kukaa kimya mpaka waliowahudumia huku mikoani tunahisi wamekula hela.Mi nahisi hili linahusishwa na kulinda image ya kuwa huyu bwana kaja kashindwa kuhudumia wananchi wake na hivyo mnamsuport kwa kutoeleza kinachowasibu.Kama bajeti ametoa ndogo nyie elezeni tu jamii kuwa capacitor yetu kutoa pass kwa mwezi ni kiasi fulani once vikiisha toeni chapisho kuiambia jamii la sivyo jamii tutaona kama hujuma tu zimeandaliwa ili tupigwe mpunga.
Ni maoni mazuri ila mie sio mmoja wao hivyo unaweza kuwaandikia hoja zako au kufika ofisi ya uhusiano watakujibu vizuri sana
 
HUU MTINDO WA KUTUMIA VISHOKA NDIYO UNASABABISHA WASIO WALENGWA KUPATA PASPORT
 
Lakini kuna matangazo yamebandikwa kila mahali hapo uhamiaji ya kuwatahadharisha wateja kuepuka madalali. Sema watanzania wanapenda sana shortcut
Ni sahihi kabisa. Na hata wale waliokuwa wakihisiwa ni vishoka zaidi ya nane walikamatwa wakapigwa picha na kupigwa marufuku kufika uhamiaji
 
Passport nimeomba toka September 2017, nimefuata taratibu zote kama walivyo nielekeza nikaweka viambatanisho vyote, fomu wakaikagua wakaniambia iko sawa... na Bank nikalipia, wakanichukua na finger prints kabisa...

Ila sasa toka hiyo September hadi hivi leo Passport yangu bado haijatoka..... Alafu kuna mtu anatoa laki tatu anapata ndani ya wiki.
 
Back
Top Bottom