Uhalisia wa maisha unazidi kuonekana

Uhalisia wa maisha unazidi kuonekana

wengi tu.. mi nilikuwa nalipa laki 3.. kwa sasa nalipa laki 2... na mwenye nyumba anapokea hata miezi mitatu.. zamani ilikuwa mwaka
Hongereni labda inategemea name eneo sie bado tunalipa ile ile kwa miezi 6
 
Sawa sawa, huku nimeona unga wa sembe na dona umefika 900 toka 2200/=, japo ni kilio kwa mkulima hio ni nafuu yangu.

P/kg
 
Kodi za nyumba zimeshuka wapi!??

Yani akili yako wewe kama uncle tu...

Kwamba sasahivi mshahara unatoka kila tar 21 hivyo basi hali ya watumishi iko bora kuliko hapo nyuma..!!!??
Sijui ni tusi gani zuri la kuweka hapa.....

Mishahara ni ileile aliyotuacha nayo JK....hivyo basi kama sasahivi haitoshi ..tulikuwa wapiga dili....

MUNGU KIMBIZA SIKU HARAKA.
Sisi Tulio Huku Huo Mshahala Unatutosha Sana Mkuu Shida Ni Malengo Tu
 
Mkuu viwanja vimeshuka wapi huko!??

Tegeta Masaiti, Bagamoyo, Mbezi Juu - Watu walikuwa wanajitamkia tu unamsikia mtu anasema kiwanja Milioni 30 mpaka Milioni 120 ilikuwa inaniuma sana sana, sasa nenda uliza bei ni milioni 15 kwenda chini hata 6 unapata
 
Now!! Wapangaji tuna ahuweni, walizidi mno.

Nilikuwa nalipa laki 8 kwa mwezi maeneo ya ununio, nikaambiwa na rafiki yangu mbona unalipa pesa nyingi sana, sikumuelewa ana maanisha nini? Ulipokaribia mwisho wa mwaka jana mwenye nyumba akanambia anataka kuongeza kodi na nimpe taharifa miezi mitatu kama nitaendelea ama sitaendelea. Nikamwambia sitaendelea nikahama. Alihangaika sana kupata mpangaji nasikia mpangaji aliyepatikana sasa analipa laki 5. Nyumba ilitaka kumdodea. Kiukweli ilikuwa ni mateso sana sana kwetu bei ya nyumba haikuwa ina fanana na hali halisi ila sikuwa na jinsi.
 
Hayo maoni yako na yanategemea sehemu ulipo na shughuli unayofanya, bei hiyo uangalie kote, huku kwangu sukari sh 2500-3000
Kiukweli kwenye suala la chakula bado bei zipo juu, inategemeana na uzalishaji wa chakula lakini tunategemea ndio kitu kitakachofuhata baadaye pamoja na gharama za usafiri,lakini katika upangaji, viwanja, mashamba hali ndio hiyo kasi ya kuelekea kwenye uhalisia wa kweli wa maisha ya mtanzania inafikiwa. Kuna rafiki yangu alinunua kiwanja tegeta masaiti kwa gharama kubwa akidhani anacheza kamari kutegemea kuwa atakiuza kwa mamilioni mengi siku za mbele sasa imekula kwakwe maana hakiuziki na alinunua millioni 60
 
Kuna mwenye nyumba kapunguza kodi ya pango mkuu.
Jaribu kuulizia nyumba wewe mwenyewe taratibu usitumie dalali asilani, nyumba za maana sana zimeshuka bei mpaka Masaki bei ni za kawaida, mikocheni kwa wanaopenda maeneo hayo. Ukikosea kutumia dalali umeumia. Namshukuru sana waziri wa ardhi kupiga marufuku madalali maana ndio walikuwa wanachangia bei kuwa juu. Sasa hivi ukimwambia mwenye nyumba nataka kuhama atakuuliza kimetokea nini, thamani ya mpangaji imeanza kurudi kama zamani
 
Viwanja vimeshuka bei? Mmmmh hapa mbona ukakasi
 
Back
Top Bottom