Maisha yanazidi kuwa magumu kote duniani

Maisha yanazidi kuwa magumu kote duniani

Kamgomoli

JF-Expert Member
Joined
May 3, 2018
Posts
1,926
Reaction score
4,110
Ukiangalia mwenendo wa kiuchumi duniani utagundua hali ya maisha kwa sasa ni mbaya. Si Marekani,China,Ujerumani au Uingereza kote kimeumana. Bei kubwa ya mafuta na gesi,chakula,ukame na uhaba wa maji safi, na"Rent" yote haya yamepelekea kupandisha sana gharama za maisha.

Leo Marekani miji kama ya Florida na Califonia kuna idadi kubwa ya Homeless people kutokana na watu kushindwa kumudu kodi ya nyumba(rent). Uingereza kuna mgomo wa wafanyakazi wa reli wakidai nyongeza ya mishahara ili kukabiliana na ukali wa maisha.

Nimekaa na kutafakari nikagundua sababu zinazosababisha dunia kuingia kwenye huu ugumu wa maisha.

1. Nchi kuwekeza pesa nyingi kwenye miundo mbinu ya kisasa. Siku hizi serikali za nchi nyingi duniani zimewekeza mabilioni ya dola kwenye miundombinu mipya ya kisasa km bandari,reli,viwanja vya ndege,barabara n.k na hivyo kuwasababishia wananchi mzigo mkubwa wa kodi.

2. Nchi kubwa kuendekeza vita vya kijinga na kutafta ubabe usio na maana. Kuna muda najiuliza hii vita ya Urusi na Ukraine ilikuwa na sababu gani za msingi km sio ubabe wa Urusi na NATO. Angalia ilivyoharibu hali ya uchumi wa dunia.Mbolea,Chakula,mafuta gesi vyote havishikiki.

3. Nchi kubwa kufanya uwekezaji mkubwa(mega investments) kwenye sayansi na technologia.

Kutokana na ushindani mkubwa uliopo baina ya Urusi,Marekani,China na washirika wao mabilioni ya pesa yamewekezwa kwenye sayansi na technology ili kila upande uwe juu ya mwingine. Kuna ushindani mkubwa wa silaha,anga za juu,mawasiliano n.k.

Marekani kwa mfano wametengeneza Telescope kubwa ya kutazama anga za juu itwayo James Webb Telescope(JWT) ambayo hadi inakamilika imegharimu dola bil.10 zaidi yaTrillion 20 za Kitanzania. Hapo unazungumzia karibu theluthi mbili ya bajeti yetu ya mwaka mzima. Vipi km pesa hii ingepelekwa kwenye kununua chakula na kuboresha huduma za maji ingeokoa watu wangapi duniani?

4.Mabadiliko ya tabia ya nchi. Hapa tunarudi palepale kwenye Ubabe wa kijinga. Nchi zinazoongoza kwa uchafuzi na uharibifu wa mazingira duniani kila mmoja hayuko tayari kupoteza. Ndio maana kila wakikubaliana kutia saini mkataba wa kupunguza gesi chafu kesho unasikia yule kagoma.

Wiki kadhaa zilizopita Ulaya wamekumbwa na joto na ukame mkali la hadi nyuzi joto 40 sababu kuu ni mabadiliko ya tabia ya nchi. Dunia inaangamizwa na maslahi ya wachache.

Kwa kifupi ugumu huu wa maisha kwa kiasi kikubwa umesababishwa na ubabe na ubinafsi wa mataifa makubwa uliopitiliza na ndo chanzo cha maumivu haya yote.

Nawasilisha.
 
Vitu vyovyote vikiwa bei juu wewe tafuta mbadala wake utajirike. Muhimu ni kuongeza ubunifu na utafiti kwa kuacha kukimbizana na bei.

Mfano sio lazima tununue gas, petrol, Diesel, jet fuel toka nje hali tunaweza tukatumia mbadala wake kwa kuzalisha hapa hapa nchini kwenye malighafi tele na tukapata clean fuel toka kwenye biofuel, kupitia bioethanol, biomethanol, biogas, biodiesel, syngas, nk.

Ukija kwenye sketa ya ujenzi zipo teknoloji si lazima utumie cement, nondo, chuma, bati, nk Ili upate jengo bora. KILA chochote kinambadala wake. Ni kuongeza tu ubunifu
 
Vitu vyovyote vikiwa bei juu wewe tafuta mbadala wake utajirike. Muhimu ni kuongeza ubunifu na utafiti kwa kuacha kukimbizana na bei...
Mkuu hivyo vyote ulivyovitaja vinahitaji nguvu ya mzungu kuanzia mtaji hadi technologia. Uliza gharama ya kutengeneza kiwanda cha kusindika gesi asili ndo utajua namaamisha nini. Haya mambo ni rahisi kuyasema lakini si kwenye utekelezaji.
 
Hio 4.Hizo Tilioni 20 ni SAwa na gharama za mradi wote wa SGR, ambao haukuwa wa lazima Sana au haraka sana kihivyo bali zilikuwa ni sifa tu aliyepita.

Hizo pesa zingewekezwa kwenye kilimo ikiwemo miundombinu ya umwagailiaji zingekuza uchumi wa nchi zingezalisha ajira za kudumu milioni 12 nchini nzima, na zingesharudi ndani ya miaka 3.
 
Kuishi kwa kutegemea athari za ubabe wa wakubwa napo ni ufinyu wa akili zetu kwann sisi tusiangalie njia mbadala wa kutatua changamoto zetu za uchumi bila kutegemea mabadiliko toka nje.

Check mfano nchi kama Brasil wao walipoona bei ya mafuta sio stable soko la Dunia sababu ya factor kubwa huwa ni vita vya kipumbavu yaani ubabe tu wa viongozi, wao wakajikita kwenye uzalishaji wa mafuta mbadala.

Leo wamepunguza uagizaji mafuta toka nje kwa kuzalisha mafuta mbadala na wameokoa pesa nyingi na kuzalisha ajira nyingi nchini mwao, mfano magari yao yanatumia 80% ya nishati wanayozalisha wenyewe ikiwemo ethanol kwa E85 au E100.
E85 ni unamix petrol lita 15 na ethanol lita 85.

Na E 100 means gari yako unatumia ethanol asilimia mia kwa mia bila kumix na petrol.
 
Maisha hayajawahi kuwa magumu, ugumu wa maisha uja pale mind akili inapogota kureasoning au umestaki, unaweza iboost au iformat kwa kuiingizia taarifa mpya kutoka vyanzo mbalimbali vya taarifa za maarifa mapya then unapata mwanga mpya unasonga.
 
Maisha hayajawahi kuwa magumu, ugumu wa maisha uja pale mind akili inapogota kureasoning au umestaki, unaweza iboost au iformat kwa kuiingizia taarifa mpya kutoka vyanzo mbalimbali vya taarifa za maarifa mapya then unapata mwanga mpya unasonga.
Naunga mkono hoja
 
Ukiangalia mwenendo wa kiuchumi duniani utagundua hali ya maisha kwa sasa ni mbaya. Si Marekani...
Maskini wa Marekani anaweza kuingiza pesa nyingi kuliko mtu wa kipato cha Kati hapo Tanzania. Sasa wewe kaa hapo jidanganye wote mnapitia ugumu sawa.
 
Maskini wa Marekani anaweza kuingiza pesa nyingi kuliko mtu wa kipato cha Kati hapo Tanzania. Sasa wewe kaa hapo jidanganye wote mnapitia ugumu sawa.
 
Maskini wa Marekani anaweza kuingiza pesa nyingi kuliko mtu wa kipato cha Kati hapo Tanzania. Sasa wewe kaa hapo jidanganye wote mnapitia ugumu sawa.
Lakini hana nyumba,ni homeless,amudu basic needs still ni masikini tu ukilinganisha na mtu wa maisha ya kati wa Tza
 
Maskini wa Marekani anaweza kuingiza pesa nyingi kuliko mtu wa kipato cha Kati hapo Tanzania. Sasa wewe kaa hapo jidanganye wote mnapitia ugumu sawa.
Hata Kama anaingiza hela nyingi ila zote zinaishia kwenye chakula anaishia kuwa homeless kuna maana gan sasa! Si Bora mi napata pesa kidogo lkn Nina uhakika wa kula na kulala nyumban kwangu
 
Lakini hana nyumba,ni homeless,amudu basic needs still ni masikini tu ukilinganisha na mtu wa maisha ya kati wa Tza
Hahaha.. huyo mwenzako homeless sababu hataki kukubaliana na hali halisi kwamba mji au State aliyopo na kazi aliyonayo hawezi kumudu rent. Ana opportunities nyingi tu mezani. Anaweza kwenda miji au States nyingine zenye affordable housing akaacha kuwa homeless. Acha hiyo akija nchi za kiafrika mtampa kazi na mshahara mrefu sababu ni mzungu na vi degree vya US. Umewahi kufika Marekani?
 
Lakini hana nyumba,ni homeless,amudu basic needs still ni masikini tu ukilinganisha na mtu wa maisha ya kati wa Tza
Mtu wa kipato cha Kati wa Tanzania atamudu maisha hadi akistaafu ataanza kusumbua watoto waanze kumtunza. Pension plan mbovu ya Bongo itamfanya awe na poor health plan, ashindwe ku maintain maisha yake ya zamani unakuta mtu anakaa na gari miaka 20, marekebisho ya nyumba hadi watoto wajichange, kusafiri kwenda vacation ndio sahau kabisa.
 
Leo nimepita barabaran nikakuta petrol 3400...nikajisemea kwa mwendo huu nitaendelea kupark sana kasubaru kangu
 
Back
Top Bottom