Uhalali wa CCM kumiliki viwanja vya michezo

Uhalali wa CCM kumiliki viwanja vya michezo

ccm na uporaji, wizi, ufisadi, uhujumu uchumi, uchawi, utekaji, mauaji, na kila aina ya uovu; havitenganishiki.
 
Kuna viwanja na majengo ambavyo kiuhalali sio mali ya ccm hata kdg!
viwanja kama Kirumba na majengo kibao yalitakiwa kurudi serikali kwani yalijengwa kwa raslimali za |Taifa na sio chama!
Ila siku zaja mali zote zitarudi na ccm ndio watajua kuwa maharage ni mboga au futari
 
Muda umewadia sasa kwa chama tawala kuvirudisha viwanja vyote vya michezo ilivyojimilikisha, ili viwe chini ya serikali. Ni ukweli usiopingika ya kwamba utaratibu uliotumika katika kuvimiliki haukuwa mzuri hata kidogo, na unaacha maswali mengi sana juu uhalali wa CCM wa kuvimiliki kama mali binafsi, huku kimsingi ukweli ni kuwa hivi ni mali ya umma.

Viwanja hivi, mathalani Kirumba - Mwanza, Sokoine- Mbeya, Samora - Iringa, Mkwakwani - Tanga, Sheikh Amri Abeid - Arusha, Ali Hassan Mwinyi - Tabora, n.k. vyote vilijengwa kupitia nguvu za wananchi wenyewe, katika maeneo ya serikali yaliyotengwa mahususi kwa ajili hiyo, lakini tu katika kipindi cha utawala wa chama kimoja cha kidola. Kwa hiyo hakuna hoja yoyote ile ya msingi ya CCM ya kuzidi kung'ang'ania kuvimiliki kama mali binafsi katika mazingira ya sasa ya uwepo wa vyama vingi.

Ukiachilia mbali suala la uhalali wa kuvimiliki, lakini jambo lingine ni dhahiri pia kuwa CCM imeshindwa kuviendeleza ili vikidhi mahitaji ya sasa ya maendeleo ya vijana kwa michezo mbalimbali. Viwanja vyote vya kisasa huwa na miundombinu bora ambayo huchochea maendeleo ya michezo yote kwa ujumla, na pia ndiyo kichocheo kingine cha kuzalisha ajira nyingi kwa vijana katika soko la ndani na hata lile la kimataifa.

Kwa sasa hali ya viwanja hivi ni mbaya na hairidhishi hata kidogo kutokana na ufinyu wa bajeti wa kutenga fedha za kuviendeleza, ama pia mapato kiduchu yanayopatikana ili kuweza kuviboresha ili viwe na muonekano wa kisasa sambamba na miundombinu bora na ya kisasa. Jambo ambalo litakuwa ni rahisi kulifanyika endapo vitakuwa chini ya manispaa za miji ama majiji.

Uongozi wa CCM Taifa uwiwe kufanya maamuzi yenye tija kwa Taifa letu, wapate busara ya kuona kuna kila aina ya haja, na pia ni takwa la wakati la kuvirudisha viwanja hivi viwe ni mali ya wananchi wote chini serikalini. Ni vyema njia za kistaarabu zikatumika kwa sasa kuvirudisha kwa hiyari kuliko kusubiri aibu ya kuja kunyang'anywa kwa nguvu siku za mbeleni, ambazo kwa akili ya kawaida kabisa zinaonyesha kuwa wala hazipo mbali kutoka hivi sasa.

Ndiyo! Ajenda ya kuwa katiba mpya na tume huru ya uchaguzi ni maana sana, lakini vyama vya upinzani pia vinapaswa pia kupaza sauti zao juu ikiwa ajenda nyingine pia inayopaswa kupelekwa kwa wananchi kwa ajili ya maslahi mapana ya nchi yetu. Na mwisho ni vyema michakato ya kufungua shauri la kisheria ili kupata tafsiri, na hata kuhoji uhalali ma utaratibu uliotumika kwa CCM kujimilikisha baadhi ya mali zake ikiwemo hivi viwanja katika kipindi cha kuanzishwa kwa utawala wa vyama vingi.
Mkuu kwa vile gharama za harusi yako na kitanda unacholalia wewe na mme/mkeo vilitokana na michango chini ya kamati ya harusi kwa hiyo mme/mke ni wa watu wote walichanga?

Nyumba au viwanja vinajengwa kwa mawe- nyie CHADEMA mnahamasisha watu wasombe mawe ya kupopoa polisi; CHADEMA badala ya kuhamasisha watu wajenge viwanja mnahamasisha watu waandame, waache kutumia mtandao wa TIGO kisa uliibua UGAIDI wa Mbowe.

Sikiliza tunataka kuona CHADEMA Mkolani ikiwa sambamba na CCM Kirumba badala ya mawazo ya kijinga unayopendekeza. Ni bora ueleweshe mapema kuwa hizo ni mali za CCM kisheria. Hii haizuii kutaifishwa ila lazima fidia itolewe ikiaamanisha kuwa CCM itapata hela zaidi
 
Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Kaluta uliopo Arusha haukujengwa na CCM wala nguvu za umma.

Uwanja huu ulijengwa na Mkoloni mwingereza anayeitwa Middleton.Uwanja huu ulikuwa mpaka na taa na mechi za usiku zilichezwa bila matatizo.

Middleton alipoondoka aliukabidhi kwa Town Council ya Arusha wakati huo.Waliuendesha mpaka mwaka 1977 ulipochukuliwa na CCM na wakaufanyia ukarabati kwa kuongeza majukwaa.
Ukarabati huo wananchi wote wa Arusha tulilazimishwa kuchanngia hiyo CCM haikutoa hata senti moja.
Jukwa la kaskazini lilijengwa na hayati Phillip Olotu kwa fedha na ufundi wake
Haya majizi tuu
 
Kama kuna jambo linalokera sana ni pale viwanja vilivyokuwa vya umma kabla ya mfumo wa vyama vingi kuporwa na CCM ambayo imeshindwa kuviendeleza. Inaonekana kama wangekuwa na uwezo walitaka hata jengo la Ikulu liwe la CCM.

Natoa hoja kuwa viwanja vyote ambavyo vilikuwa vya umma kabla ya mfumo wa vyama vingi virudiswhe serikalini kama ilivyo uwanja wa Uhuru.

Mkwakwani, Amri Abeid, Kirumba, Ali Hassan Mwinyi, Nelson Mandela, Samora na vingine vingi virudishwe serikali mara moja; havikujengwa na CCM bali vilijengwa na wananchi wote. Uwanja wa Mkwakwani umekuwapo tangu wakati wa Ukoloni; uwanja wa Amri Abeid ulijengwa kabla hata CCM haijazaliwa; na hata vile vilivyojengwa baada ya CCM havikuwa vimejengwa kama vitega uchumi vya CCM bali vilijengwa kama viwanja vya burudani kwa wanachi wote.

Sijui kama nimeeleweka.
 
Naunga mkono hoja 100% ila hili suala ni gumu kutekelezwa bila msukumo wa kisheria na kijamii. Lakini una uhakika viwanja vyote ulivyotaja vilirudishwa serikalini? Mbona bado Kirumba unaitwa CCM Kirumba? Kuna ule wa CCM Liti upo Singida. Na serikali inapeleka fedha za umma kuviboresha.
 
Naunga mkono hoja 100% ila hili suala ni gumu kutekelezwa bila msukumo wa kisheria na kijamii. Lakini una uhakika viwanja vyote ulivyotaja vilirudishwa serikalini? Mbona bado Kirumba unaitwa CCM Kirumba? Kuna ule wa CCM Liti upo Singida. Na serikali inapeleka fedha za umma kuviboresha.
hukunielewa
 
Itakavyobadilisha ni either katiba mpya au chama kingine Kishinev hatamu
 
Ccm lazima itaondoshwa kwenye hivyo viwanja na baada ya hapo lazima wataburuzwa mahakamani ili walipe damages kwa muda wote ambao wamevitumia hivyo viwanja.
 
Back
Top Bottom