Ugeni Mzito.

Ugeni Mzito.

uporoto01

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2008
Posts
4,698
Reaction score
1,429
Nina furaha kuwatangazia watanzania wenzangu kwamba tuna ugeni mzito siku 2-3 hizi tumetembelewa na Rais wetu akitokea South Afrika na atakuwepo nchini kwa mapumziko mafupi kabla ya kusafiri tena wiki ijayo.Wenye matatizo ya kuhitaji ufumbuzi wake waandike barua na kumpa Waziri mkuu ambaye atamkabidhi atakapokuja tena kupumzika safari nyingine.
 
Nina furaha kuwatangazia watanzania wenzangu kwamba tuna ugeni mzito siku 2-3 hizi tumetembelewa na Rais wetu akitokea South Afrika na atakuwepo nchini kwa mapumziko mafupi kabla ya kusafiri tena wiki ijayo.Wenye matatizo ya kuhitaji ufumbuzi wake waandike barua na kumpa Waziri mkuu ambaye atamkabidhi atakapokuja tena kupumzika safari nyingine.

Hapo penye nyekundu hapo...
 
atakuwa na mapumziko ya siku 3.
Tukitilia maanani kuwa mwezi ujao ni Ramadhan, atakuwepo nchini kwa wiki 3 kuanzia sasa.
Wiki ya pili ya Ramadhani atakwenda kufutari nchi za Falme za Kiarabu, baadaye Singapore na Malaysia.
Sikukuu atakuwepo hapa na baada ya mfungo wa sita "intensive schedule" itaanza.
 
Wakuu mnadhani mapumziko haya yatakuwa ya siku ngapi ? otea,atakaye toa jibu sahihi kuna ZAWADI nono.
atakaa wiki moja tu kwa ajili ya kuulizia ishu ya jairo akishapata ubuyu huo anaendelea na uvumbuzi wa dunia..
 
hahahahaha!
Kweli huu ni ugeni mzito. Mi naona atakuwepo hapa Tz sio zaidi ya siku 2!...
 
Huenda Mdau anataka kuweka record ya kutembea nchi nyingi zaidi duniani,ila pia huenda haipendi Tz ndo maana hakai akatulia jamani!
Kwa nn asiwe anazungukia mikoani aone watu tunavyotaabika!
 
kwa hiyo nyie shida yenu ni nini? Mlitaka muwe mnamwona ofisini kila siku. Au huko ambako huwa anakwenda huwa anajipeleka tu? I believe and I will always believe kwamba Rais haamui tu kwamba aende huku au kule kama si tu ana mwaliko au kuna mkutano unaomtaka awepo au kuna jambo la msingi analokwenda kulifanya kama sehemu ya uwakilishi wa taifa.
 
Ushauri wangu ni kwamba tuombe nchi za nje zisimpe mualiko tena.
 
kwa hiyo nyie shida yenu ni nini? Mlitaka muwe mnamwona ofisini kila siku. Au huko ambako huwa anakwenda huwa anajipeleka tu? I believe and I will always believe kwamba Rais haamui tu kwamba aende huku au kule kama si tu ana mwaliko au kuna mkutano unaomtaka awepo au kuna jambo la msingi analokwenda kulifanya kama sehemu ya uwakilishi wa taifa.
Nakubaliana na wewe kuwa si yeye anayefanya maamuzi ndo maana Waziri Mkuu Pinda alisema si Bunge, Mahakama,TAKUKURU,usalama wa Taifa,Ikulu wala Yeye anayeweza kutoa maamuzi mpaka Vasco Da Gama atoke South Africa ndo aamue nn cha kufanya!
 
Back
Top Bottom