Ugawaji wa masafa ya redio: Ni kwanini kusiwe na ''frequency'' moja kwa kituo kimoja cha redio nchi nzima?

Mwanamaji

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
2,896
4,495
Habari zenu wajumbe....

Kwa muda mrefu kidogo nimekua nikijiuliza hili swali.
Ni kwanini kuna mkanganyiko katika ugawaji wa masafa ya vituo vya redio ?

Nitaeleza kwa mifano ili hoja yangu ieleweke vema kwa namna hali ilivyo sasa hivi.

Kituo chetu cha redio (cha mfano) tutakiita ''Tikiti maji FM''.

Kwa namna hali ilivyo sasa, utaipata Tikiti FM kwa masafa yafuatayo katika mikoa tofauti tofauti....

Mbeya 89.9 MHz
Tanga 102.3 MHz
Iringa 85.7 MHz
Dar Es Salaam 97.5 MHz
Kigoma 101.4 MHz
Mtwara 92.1 MHz
N.k

Tatizo liko hapa:
Hii inatupa mkanganyiko sisi wapenzi wa redio hii (Tikiti Maji FM) pale tunaposafiri kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine. Itatulazimu kuanza kuhangaika kujua redio yetu pendwa (Tikiti maji FM) inapatikana kwenye frequency zipi katika mkoa huu ''mpya'' tulioutembelea, ili tuweze kuisikia.

Mawazo yangu:
Ninadhani ingekua ni vema zaidi haya masafa yagawanywe ''kitaifa'' ukizingatia kwamba mamlaka inayogawa masafa haya ni moja yaani (TCRA), hivyo hakutakua na mkanganyiko.

Hali iwe kama hivi:
88.1 MHz ni Tikiti Maji FM
89.8 MHz ni Mapapai FM
92.3 MHz ni Nanasi FM
95.6 MHz ni Nazi Mbovu FM
98.5 MHz ni Embe Dodo FM
102.7 MHz ni Nyanya Mbichi FM
107.2 MHz ni Pilipili Kichaa FM
N.k
Masafa tajwa hapo juu yawe ni kwa nchi nzima na si kimikoa.

Manufaa:
Hii itasaidia yafuatayo:
1. Kuondoa mkanganyiko na usumbufu usio wa lazima kwa walaji (wasikilizaji).
2. Itasidia kwenye ''branding'' ya vituo vya redio. Mtangazaji akisema ''unasikiliza 88.1'', msikilizaji anaelewa moja kwa moja kwamba kituo kinachozungumziwa hapa ni Tikiti Maji FM.
(Itakua tofauti na sasa, ambapo ni lazima mtangazaji huyo ni afafanue anaizungumzia 88.1 ''ya mkoa upi'')

Kwa kifupi ni kwamba masafa fulani yanakua ni ''brand and identity'' ya kituo cha fulani cha redio nchi nzima.


Majibu ya hoja ''zinazoweza'' kujitokeza kufuatia pendekezo hili:

1. Itakuwaje kwa redio ambazo hazisikiki nchi nzima ?
Jibu: Katika eneo ambalo redio husika haisikiki, frequency ''yake'' inabaki ''wazi'' (Hakuna mwingine atakayeitumia hadi pale ''mwenyewe'' atakapoanza kurusha matangazo kwenye eneo hilo).

2. Je hii haitapunguza mapato ya serikali kupitia tozo za kuomba masafa ?
Jibu: Hapana, mapato yatapatikana kwenye kuomba hayo masafa ya ''kitaifa'' pamoja na ''vibali'' vya kurusha matangazo kwenye mikoa tofauti tofauti.

3. Tuna vituo vya redio vingi sana nchini, je, tukitaka kila redio ihodhi masafa ''kitaifa'', tunayo ''akiba'' ya masafa ya kumgawia kila mmoja (kila redio) ?

Jibu: Tunaweza kutanua ''uwanda'' wa masafa kutoka (87 hadi 108) yaliyopo sasa (endapo hayatatosha) na kuongezea zaidi (kwa kadri teknolojia itakavyoturuhusu).

Naombeni kuwasilisha.

NB: Mimi si mtaalam wa mambo ya ''telecommunications'' hivyo kunaweza kukawa na mapungufu ya kiufundi katika wasilisho langu hapo juu (hasa jibu la swali la 3), hivyo naomba tuutumie uzi huu kuelimishana kama kuna waliobobea katika masuala haya.

Karibuni.
 
Wait majibu utayapata ni kwa nini, maana nipo mbioni kufungua radio station yangu itakayoitwa MAFENESI FM, huko niakuwa natoa elimu ya mambo ya kuanzisha radio station!

Halafu mbona hujauliza ni kwa nini hizo radio frequency za fm zinaishia na decimal point ambayo ni namba witiri..!?!
 
Bado mpaka sasa vifaa local kuwa digital hapa ila kwa ulaya teyari.
Mfano star tv wanatumia frequency moja ya mawimbi TV kuchambua tv zote.
Kwa nini!
Frequency zina masafa yanayo kwenda na geograph na yanapo ishia
IMG_4154.jpg


IMG_4155.jpg


Vizuizi
Hali ya hewa mfano ukanda baridi,ukanda wajoto na n.k
Sehemu ya miinuko,ukanda wa bahari,tambarare na n.k

Hivi vote vinaweza kufanya frequency kushinda kufika maana inazidi kupotea kwa kuwa frequency ni wave.
Wave ina tegemeana na uwezo mnaotumia
IMG_4156.jpg

IMG_4157.jpg


Kama wave zinazotumia fm ni ngumu kufika mbali sana ila zinaweza kuboreshwa.
Siwezi kueleza kwa kuandika sana
 
Bado mpaka sasa vifaa local kuwa digital hapa ila kwa ulaya teyari.
Mfano star tv wanatumia frequency moja ya mawimbi TV kuchambua tv zote.
Kwa nini!
Frequency zina masafa yanayo kwenda na geograph na yanapo ishia
View attachment 1719220

View attachment 1719221

Vizuizi
Hali ya hewa mfano ukanda baridi,ukanda wajoto na n.k
Sehemu ya miinuko,ukanda wa bahari,tambarare na n.k

Hivi vote vinaweza kufanya frequency kushinda kufika maana inazidi kupotea kwa kuwa frequency ni wave.
Wave ina tegemeana na uwezo mnaotumia
View attachment 1719222
View attachment 1719223

Kama wave zinazotumia fm ni ngumu kufika mbali sana ila zinaweza kuboreshwa.
Siwezi kueleza kwa kuandika sana
Uonekana unajua lakini umejibu as if wote tunajua Kama wewe.
 
Wait majibu utayapata ni kwa nini, maana nipo mbioni kufungua radio station yangu itakayoitwa MAFENESI FM, huko niakuwa natoa elimu ya mambo ya kuanzisha radio station!

Halafu mbona hujauliza ni kwa nini hizo radio frequency za fm zinaishia na decimal point ambayo ni namba witiri..!?!
Nasubiri majibu kwa hamu sana. Bila shaka nitakua msikilizaji mzuri wa Mafenesi FM.
Sifahamu pia ni kwanini hayo masafa yanaishia namba witiri kama ulivyotanabaisha.
 
Inasemekana Radio nyingi za FM zinalilia kuwepo kwenye FREQ za chini kwa sababu

1. FREQ ndogo = WAVELENGTH kubwa = na so usafiri wa information una cover ENEO kubwa

2. Radio zilizo kwenye magari nyingi zinatoka JAPAN, na ukizichunguza zimeishia kwenye FREQ za chini nafkiri mwisho 90 MHz, hivyo kurusha matangazo yako kwenye masafa haya kunafanya uwe na wasikilizaji wengi

3. Sasa kupata izo FREQ za chini kila mkoa ni issue, ndio maana utapigania upate baadhi ya mikoa na mingine umuachie Mungu muumba
 
Habari zenu wajumbe..
Una hoja nzuri ingawa sina uhakika na mitambo yetu kama inaweza kusambaza mawimbi kwa nchi nzima pasipo frequencies kubadilika. Kuna siku nilijikuta nachanganyikiwa maana nilikuwa napenda kusikiliza redio fulani (kuna kipindi nilikuwa nakifuatilia), siku moja nikapata safari ya Mbeya, shida ikaja pale nilipoanza kutafuta frequency za redio hiyo kwa kukariri zile zinazotumika Dar es Salaam...
 
Habari zenu wajumbe....

Kwa muda mrefu kidogo nimekua nikijiuliza hili swali.
Ni kwanini kuna mkanganyiko katika ugawaji wa masafa ya vituo vya redio ?

Nitaeleza kwa mifano ili hoja yangu ieleweke vema kwa namna hali ilivyo sasa hivi.

Kituo chetu cha redio (cha mfano) tutakiita ''Tikiti maji FM''.

Kwa namna hali ilivyo sasa, utaipata Tikiti FM kwa masafa yafuatayo katika mikoa tofauti tofauti....

Mbeya 89.9 MHz
Tanga 102.3 MHz
Iringa 85.7 MHz
Dar Es Salaam 97.5 MHz
Kigoma 101.4 MHz
Mtwara 92.1 MHz
N.k

Tatizo liko hapa:
Hii inatupa mkanganyiko sisi wapenzi wa redio hii (Tikiti Maji FM) pale tunaposafiri kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine. Itatulazimu kuanza kuhangaika kujua redio yetu pendwa (Tikiti maji FM) inapatikana kwenye frequency zipi katika mkoa huu ''mpya'' tulioutembelea, ili tuweze kuisikia.

Mawazo yangu:
Ninadhani ingekua ni vema zaidi haya masafa yagawanywe ''kitaifa'' ukizingatia kwamba mamlaka inayogawa masafa haya ni moja yaani (TCRA), hivyo hakutakua na mkanganyiko.

Hali iwe kama hivi:
88.1 MHz ni Tikiti Maji FM
89.8 MHz ni Mapapai FM
92.3 MHz ni Nanasi FM
95.6 MHz ni Nazi Mbovu FM
98.5 MHz ni Embe Dodo FM
102.7 MHz ni Nyanya Mbichi FM
107.2 MHz ni Pilipili Kichaa FM
N.k
Masafa tajwa hapo juu yawe ni kwa nchi nzima na si kimikoa.

Manufaa:
Hii itasaidia yafuatayo:
1. Kuondoa mkanganyiko na usumbufu usio wa lazima kwa walaji (wasikilizaji).
2. Itasidia kwenye ''branding'' ya vituo vya redio. Mtangazaji akisema ''unasikiliza 88.1'', msikilizaji anaelewa moja kwa moja kwamba kituo kinachozungumziwa hapa ni Tikiti Maji FM.
(Itakua tofauti na sasa, ambapo ni lazima mtangazaji huyo ni afafanue anaizungumzia 88.1 ''ya mkoa upi'')

Kwa kifupi ni kwamba masafa fulani yanakua ni ''brand and identity'' ya kituo cha fulani cha redio nchi nzima.


Majibu ya hoja ''zinazoweza'' kujitokeza kufuatia pendekezo hili:

1. Itakuwaje kwa redio ambazo hazisikiki nchi nzima ?
Jibu: Katika eneo ambalo redio husika haisikiki, frequency ''yake'' inabaki ''wazi'' (Hakuna mwingine atakayeitumia hadi pale ''mwenyewe'' atakapoanza kurusha matangazo kwenye eneo hilo).

2. Je hii haitapunguza mapato ya serikali kupitia tozo za kuomba masafa ?
Jibu: Hapana, mapato yatapatikana kwenye kuomba hayo masafa ya ''kitaifa'' pamoja na ''vibali'' vya kurusha matangazo kwenye mikoa tofauti tofauti.

3. Tuna vituo vya redio vingi sana nchini, je, tukitaka kila redio ihodhi masafa ''kitaifa'', tunayo ''akiba'' ya masafa ya kumgawia kila mmoja (kila redio) ?

Jibu: Tunaweza kutanua ''uwanda'' wa masafa kutoka (87 hadi 108) yaliyopo sasa (endapo hayatatosha) na kuongezea zaidi (kwa kadri teknolojia itakavyoturuhusu).

Naombeni kuwasilisha.

NB: Mimi si mtaalam wa mambo ya ''telecommunications'' hivyo kunaweza kukawa na mapungufu ya kiufundi katika wasilisho langu hapo juu (hasa jibu la swali la 3), hivyo naomba tuutumie uzi huu kuelimishana kama kuna waliobobea katika masuala haya.

Karibuni.
Kwenye namba moja, kusema Frequency ibaki wazi, ni matumizi mabaya ya Frequency.
 
Bado mpaka sasa vifaa local kuwa digital hapa ila kwa ulaya teyari.
Mfano star tv wanatumia frequency moja ya mawimbi TV kuchambua tv zote.
Kwa nini!
Frequency zina masafa yanayo kwenda na geograph na yanapo ishia
View attachment 1719220

View attachment 1719221

Vizuizi
Hali ya hewa mfano ukanda baridi,ukanda wajoto na n.k
Sehemu ya miinuko,ukanda wa bahari,tambarare na n.k

Hivi vote vinaweza kufanya frequency kushinda kufika maana inazidi kupotea kwa kuwa frequency ni wave.
Wave ina tegemeana na uwezo mnaotumia
View attachment 1719222
View attachment 1719223

Kama wave zinazotumia fm ni ngumu kufika mbali sana ila zinaweza kuboreshwa.
Siwezi kueleza kwa kuandika sana
Naomba nikuulize swali
 
Back
Top Bottom