Uganda: Wanafunzi wa chuo kikuu wagoma kuingia madarasani baada ya kutokuwepo kuku kwa siku tatu mfululizo

Donatila

JF-Expert Member
Oct 23, 2014
7,557
21,512
Uganda: wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Nkumba kilichopo mjini Entebbe, wamegoma kuingia madarasani, baada ya kutokuwepo kuku kwa siku tatu mfululizo.

Mgomo huo ulioanza leo, umeridhiwa na idadi kubwa ya wanafunzi. Mbali na kudai kutowepo kwa kitoweo cha nyama ya kuku, wanafunzi hao wanalalamikia upungufu wa uma za chakula, maziwa, ubovu wa chakula na kudai maji ya kunywa ya chupa yenye ubora. Ili kushinikiza zaidi kutekelezwa kwa madai hayo, uongozi wa wanafunzi hao uliandamana kuelekea ofisi ya makamu mkuu wa chuo ambako walifanya kikao.

Katika kikao hicho, wanafunzi hao walidai uongozi umepokea malalamiko Yao na kwamba yatafanyiwa kazi haraka. Hatua hii ya wanafunzi hao imeonekana kuwa tofauti kidogo na madai yaliyozoeleka kwa wanafunzi wa vyuo ambao mara nyingi hudai ubora wa masomo, upungufu wa wahadhiri, lakini sasa hawa wa Nkumba, wao wanalilia kuku kuwemo kwenye mlolongo wa vyakula vyao kila siku.
 
Huko nyama zao za ng'ombe ndo zile za madawa ya kukaushia maiti..
Sio mbaya n halali yao
 
Kwa Uganda hiki ndio chuo chao cha kata. Lakini sidhan km Udom kwa hapa kwetu wanaweza kuacha masomo na kuanza kulilia nyama ya kuku.
 
Data mkuu. Weka data kama Udom ni chuo cha kata.
Mkuu nani kasema udom ni chuo cha kata? Mimi sijasema kabisa, LAKINI anyway ngoja nikupe data
>Udom ni chuo cha kata kwa sababu mademu wengi wenye GPA kali ni wale ambao lectures wameona uwezo wao wa KUKATA mauno wawapo kitandani.
>Udom ni chuo cha kata kwa sababu ufundishaji Wa pale katika chuo ni Wa kuunga unga km michuzi. Topic hazifundishwi vizuri na kwa ufanishi. Topic mnazi KATA KATA tu.
 
Back
Top Bottom