Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,478
- 40,000
Ugali kweli mtamu,
Kwa huo ninayo hamu,
Kwa mboga yenye saumu!
Ugali tangu shuleni
Jamani hadi jeshini
Nikaula na chuoni
Ugali iwe mchana
Kwenye upepo mwanana
Mwenzenu ninajichana
Ugali hata jioni,
Mezani au jikoni
Nikishatoka kazini
Ugali iwe kwa mboga
Sima kwa kweli yanoga
Kwa tembele na maboga!
Ugali kwa kurumagia
Vidole kujilambia
Na nyama inanukia!
Ugali ule kwa mchuzi
Wa samaki hata mbuzi,
Mwanawane kama kazi!
Ugali msosi wa nguvu
Haupikwi kwa wavivu,
Au walio wachovu
Ugali uwe kiporo
Alfajiri na mmajoro
Kwa mapanki ya Nyamanoro!
Ugali nimesifia
Wali ninautungia
Beti nitaupangia,
Ugali nafakamia
Matonge navingiria
Nakula nafikiria
UGALI KWELI MTAMU!!
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
Kwa huo ninayo hamu,
Kwa mboga yenye saumu!
Ugali tangu shuleni
Jamani hadi jeshini
Nikaula na chuoni
Ugali iwe mchana
Kwenye upepo mwanana
Mwenzenu ninajichana
Ugali hata jioni,
Mezani au jikoni
Nikishatoka kazini
Ugali iwe kwa mboga
Sima kwa kweli yanoga
Kwa tembele na maboga!
Ugali kwa kurumagia
Vidole kujilambia
Na nyama inanukia!
Ugali ule kwa mchuzi
Wa samaki hata mbuzi,
Mwanawane kama kazi!
Ugali msosi wa nguvu
Haupikwi kwa wavivu,
Au walio wachovu
Ugali uwe kiporo
Alfajiri na mmajoro
Kwa mapanki ya Nyamanoro!
Ugali nimesifia
Wali ninautungia
Beti nitaupangia,
Ugali nafakamia
Matonge navingiria
Nakula nafikiria
UGALI KWELI MTAMU!!
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)