Ufuska, ulevi vyamkera Babu akemea

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,174
Ufuska, ulevi vyamkera Babu akemea Send to a friend Saturday, 28 May 2011 10:30

Mussa Juma, Samunge
MCHUNGAJI Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Mwasapila amekemea maovu anayodai kuwa yameibuka katika kijiji cha Samunge kutokana na ongezeko la watu walioweka makazi ya muda.

Akizungumza na gazeti hili katika mahojiano maalum jana, Mwasapila alisema katika siku za hivi karibuni, kumekuwa na ongezeko la matendo ya ngono na ulevi, mambo ambayo yanaelekea kupunguza heshima ya tiba yake.

Tangu aanze kutoa tiba ya magonjwa sugu mwanzoni mwa mwaka huu, Mwasapila amekuwa akikemea maovu hayo ambayo ni pamoja na ngono, ulevi na wizi ili kulinda heshima ya tiba yake.

Lakini, uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa vitendo vya ufuska vimekuwa vikifanywa katika mahema ambayo yanakodishwa kwa watu mbalimbali kwa gharama ya kati ya Sh5,000 hadi Sh20,000.

Huduma hiyo ya mahema inapatikana katika maeneo ambayo kuna migahawa na baa na hivyo baadhi ya wateja wakiwamo wagonjwa wamekuwa wakilala kwa kukodi kwa muda watakaohitaji kustarehe.

Uchunguzi katika baadhi ya mahema hayo umeonyesha kuwa huduma hiyo ya kupangisha imekuwa ikitolewa hadi nyakati za mchana kwa wenyeji, wakiwemo wafanyabiashara wengi wa vyakula na vinywaji, jambo ambalo limekuwa likiwasukuma pia kuyatumia kwa ufuska.

Baadhi ya wakazi wa Samunge, Joram Bugirwa na Peter Paulo waliieleza Mwananchi kuwa wageni wanaofika kijijini kwao ndio ambao wanaendesha vitendo hivyo na kuomba uiongozi wa serikali na Mchungaji Mwasapila kuwakemea.

"Kijiji chetu sasa kimeharibika sana, uhuni tu watoto wa kike wanaharibika kwani hawakuwahi kuona watu wengi hivi hapa na wanashawishika kufanya vitendo vibaya,"alieleza Peter.

Kwa upande wake, kaimu mwenyekiti wa kijiji hicho, Jonas Ngiroboi alikiri jana kupokea taarifa za kuwepo vitendo vya ufuska na kueleza kuwa tayari serikali ya kijiji inao mpango wa kuwaorodhesha wafanyabuiashara wote waliopo Samunge ili kujua kazi zao.

"Wapo wengi inawezekana wengine wamekuja kwa mambo yao tumeanza kufuatilia jambo hili kwani awali hata kodi walikuwa hawalipi sasa tunaweza utaratibu walipe kwa kijiji kutokana na kufanyabiashara hapa,"alisema Ngiroboi.

Mapema jana, Mchungaji Mwasapila aliamua kutolea kauli suala hilo akisema ameshangazwa na tabia ya baadhi ya watu kuanza kufanya ufuska wa kutisha na kuitia doa tiba yake.

"Asubuhi mipira ya kiume (kondomu) inaokotwa barabarani, muziki unapigwa hadi asubuhi na matendo mengine mabaya yanaonekana sasa.....hivi karibuni
Nitalisemea suala hili baada ya kukutana na watu wanaofanya biashara hapa,"alisema.

Katika siku za hivi karibuni baadhi ya watu wanaofika Samunge kwa ajili iya tiba wamewalalamikia baadhi ya wasaidizi wa mchungaji huyo kwa madai kuwa wamekuwa wakiendekeza ulevi.

Tiba ya mchungaji huyo imekigeuza kijiji hicho kuwa eneo la utalii hasa baada ya mamia ya wanyabiashara kutoka maeneo mbalimbali nchini kuweka makazi ya muda kwa kujenga mahema, kuuza vyakua, vinywaji na maduka ya bidhaa mbalimbali.

Vifo vyafikia 101

Katika hatua nyingine, idadi ya watu waliofariki dunia katika kijiji hicho kuanzia Machi 13 hadi Mei 25 mwaka huu imefikia 101

Idadi hiyo imeongezeka juzi baada ya watu wengine watatu akiwemo raia wa Kenya kufariki.

Mganga mfawidhi wa zahanati ya Kata ya Samunge, Elias Lubida aliliambia gazeti hili kuwa wagonjwa hao wamekuwa wakifariki dunia kutokana na kufika mahali hapo wakiwa katika hali mbaya kiafya.

Aliwataja wagonjwa waliofariki wiki hii kuwa ni Ledama Maridani (70), mkazi wa Narok, Kenya, Lucia Mmasi (27) kutoka Hai mkoani Kilimanjaro na Nolekatu Mollel (3), mkazi wa Pinyinyi wilayani Ngorongoro.

"Tunaendelea kutoa wito watu wasilete huku wagonjwa mahututi ambao wanawatoa hospitali kwani miundombinu siyo mizuri na pia ni kuwatesa wagonjwa, ''alisema Lubida.

Mwenyekiti adaiwa kutoweka na vitendea kazi
Wakati huohuo, halmashauri ya kijiji cha Samunge imetoa siku tatu kwa mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho aliyeondolewa madarakani, Michael Lengume kukabidhi vitendea kazi.


Maamuzi hayo yalifikiwa juzi katika kikao kilichofanyika jioni chini ya kaimu mwenyekiti wa kijiji hicho, Jonas Ngiroboi na afisa mtendaji wa kata Michael Kimario.

Ngiroboi ambaye pia ni mwenyekiti wa kitongoji cha Samunge aliliambia gazeti hili kuwa wamempa siku tatu mwenyekiti huyo kukabidhi mali zaserikali na ofisi wakati suala lake linashughulikiwa na halmashauri ya wilaya hiyo.

''Tumepokea taarifa ya mapato na matumizi bado tunaifanyia kazi kwani kuna malipo ya watu ambayo yana utata, lakini tumeona kwanza tukabidhiwe ofisi ndipo kazi iendelee,''alisema Ngiroboi.

Hata hivyo, Lengume amekuwa akipinga kuondolewa kwake katika nafasi hiyo kwa maelezo kuwa taratibu hazikufuatwa ikiwepo kupewa muda wa kujibu tuhuma na kufafanya tuhuma nyingi hazina ukweli.

Foleni yapungua Samunge

Misafara ya magari jana imeendelea kupungua licha ya uwepo wa magari zaidi ya 150 yaliyopewa huduma jana yakiwepo mengi ya raia wa kigeni toka nchini Kenya, Uganda na Burundi.

Ataka urasimu wa vibali ukome

Katika hatua nyingine Mchungaji Mwasapila ametaka mamlaka zinazohusika na utoaji wa vibali kwa magari yanayopeleka wagonjwa Samunge kuacha urasimu ili kuwaondolea wagonjwa hao usumbufu usiokuwa wa lazima.Mchungaji huyo aliliambia gazeti hili kuwa amepata malalamiko mengi kutoka kwa wagonjwa kwamba utaratibu mzima wa upatikanaji wa vibali umetawaliwa na rushwa.

"Wawaachie watu waje kupata tiba kwa sasa hakuna haja ya kusumbua watu kwani tuna utaratibu mzuri wa kutoa dawa ambao unasababisha foleni kumalizika mapema," alisema Mwasapila.

Mchungaji huyo pia alieleza kuridhishwa na maafisa wa serikali wanaomsaidia kutoa huduma hapa Samunge kutokana na kupungua kwa kiasi kikubwa kwa foleni.
 
Comments




0 #4 malipoa 2011-05-29 00:22 hivi nyinyi waandishi wa gazeti hili munalipwa kiasigani kupigia debe kanisa hamuoni habari yakuandika kila siku babu babu huyo babu kwani anafanya kubwa lipi isipokua ni kanisa tu hebu andikeni mambo ya maana maisha yanavo kua magumu kwamtanzania kuipa serekali msukumo
Quote









0 #3 kiure 2011-05-28 19:58 wacha u[NENO BAYA]a ushamiri tumetaka wenyewe kwa kukubali tiba itokanayo na ndoto! hata hao nao wameoteshwa wabanjuane ndio watapona!
Quote









0 #2 Adolph Sendeu 2011-05-28 19:48 Hivi ni kwa nini kazi ya huduma hapo Samunge iachwe tu kwa mtu yeyote. Kwani kanisa liko wapi? hakuna wahudumu katika makanisa. Viongozi wa kanisa wachukue hatua kuwatambua watu hao na kukabithi majina yao serikalini ili waondolewe. Katika hali ya kawaida hata tu kuongea u[NENO BAYA] karibu na kanisa au msikiti watu wenye kumwogopa Mungu hawawezi kufanya hivyo. Inawezekanaje watu kufanya u[NENO BAYA], ulevi nk. katika eneo hilo?

Mlundikano wa watu ndio unaovuta wafanya biashara na walu wengine. Naiomba Serikali iharakishe kutengenea barabara ya kwenda samunge ili watu wafike na kuondoka kwa haraka kupunguza mlundikano huo unaowavutia wafanya biashara na wahini.

Vileo vipigwe marufuku Samunge

Quote









0 #1 kipara 2011-05-28 15:51 ushirikina ulevi na uzinzi ni mapacha matatu ambayo yamegandana na hayawezi yakatenguka.
Quote

 
Code:
Tiba ya mchungaji huyo  imekigeuza kijiji hicho kuwa  eneo la utalii hasa baada ya mamia ya  wanyabiashara kutoka maeneo  mbalimbali nchini kuweka makazi ya muda kwa  kujenga mahema, kuuza  vyakua, vinywaji na maduka ya bidhaa mbalimbali.
 
Vifo vyafikia 101
 
Katika hatua nyingine, [COLOR=red]idadi ya watu waliofariki dunia[/COLOR] katika kijiji  hicho kuanzia Machi 13 hadi Mei 25 mwaka huu imefikia[COLOR=red] 101[/COLOR]
 
Idadi hiyo imeongezeka juzi baada ya watu wengine watatu akiwemo raia wa Kenya kufariki.

Swali ni lile lile.............kweli Muumba yupo hapo SAMUNGE?
 
Naomba niulize hivi, je ni sehemu gani hapa duniani yenye kusanyiko la watu ambayo haina mapacha hao watatu(ulevi, uzinzi na ushirikina?)
Samunge ilianza kama medical gathering, lakini with time tabia zote za binadamu( zinaanza kujitokeza baada ya baadhi ya watu kufahamiana na kuwa pamoja kwa muda mwingi, eg wafanyabiashara! na wanakijiji!(ecological &antropological interactions have driven home).
Jamani hata vyuoni huwa tunaenda kwa nia moja tu ya kusoma, lakini with familiarization watu wanaanzisha mapenzi, na hata wengine kunywa sumu kwa wivu!...
 
Code:
Tiba ya mchungaji huyo  imekigeuza kijiji hicho kuwa  eneo la utalii hasa baada ya mamia ya  wanyabiashara kutoka maeneo  mbalimbali nchini kuweka makazi ya muda kwa  kujenga mahema, kuuza  vyakua, vinywaji na maduka ya bidhaa mbalimbali.
 
Vifo vyafikia 101
 
Katika hatua nyingine, [COLOR=red]idadi ya watu waliofariki dunia[/COLOR] katika kijiji  hicho kuanzia Machi 13 hadi Mei 25 mwaka huu imefikia[COLOR=red] 101[/COLOR]
 
Idadi hiyo imeongezeka juzi baada ya watu wengine watatu akiwemo raia wa Kenya kufariki.

Swali ni lile lile.............kweli Muumba yupo hapo SAMUNGE?



If you believe that God is omnipresent you can't ask such a question. Unafikiri ni wapi ambapo hayupo?
 
Kweli yupo Muumba hapo Samunge kweli?

Code:
Tiba ya mchungaji huyo imekigeuza kijiji hicho kuwa eneo la utalii hasa baada ya mamia ya wanyabiashara kutoka maeneo mbalimbali nchini kuweka makazi ya muda kwa kujenga mahema, kuuza vyakua, vinywaji na maduka ya bidhaa mbalimbali.

Vifo vyafikia 101

Katika hatua nyingine, [COLOR=red]idadi ya watu waliofariki dunia[/COLOR] katika kijiji hicho kuanzia Machi 13 hadi Mei 25 mwaka huu imefikia[COLOR=red] 101[/COLOR]

Idadi hiyo imeongezeka juzi baada ya watu wengine watatu akiwemo raia wa Kenya kufariki.

Swali ni lile lile.............kweli Muumba yupo hapo SAMUNGE?

huyo muumba unayemjua wewe anaishi wapi? europe au USA? tujibu kwanza then na wewe utapata jibu lako
 
popote kwenye mikusanyiko hivyo vitu si rahisi kuvitenganisha, hasa kwa wale ambao hawajaenda kutibiwa
 
Tuliombali na ambao hatujahudhuria huko hatuna namna ya kujua ukweli, tunaamini iko siku ukweli utafahamika na tunaomba hilo lifahamike mapema. Na kama katika muitikio wote huo suala zima si la kweli basi kazi bado ngumu Tanzania.
 
Back
Top Bottom