Ufisadi jiji la Mwanza, Mwanasheria jiji Mwanza na wenzake wawili wapiga Tsh ML. 190

Nyanswe Nsame

Senior Member
Jul 9, 2019
158
175
Ufisadi jiji la Mwanza, Mwanasheria jiji Mwanza na wenzake wawili wapiga Tsh ML. 190

Jiji la Mwanza limegubikwa na vitendo vya ufisadi unaofanywa na baadhi ya watumishi wasiokuwa waadilifu wanaoenda rushwa.

Watumishi hao ni Mwanasheria wa jiji la Mwanza Mariam Ukwaju na wenzake wawili ambao wanatuhumiwa kula shilingi milioni 190.

Fedha zilizopigwa na watumishi hao ni kutoka mradi uliopo shule ya Sekondari ya Pamba ya jijini Mwanza.

Fedha hizo zinatokana na baadhi ya vyumba vilivyopo katika jengo hilo ambavyo havijaorodheshwa kwenye idadi ya vyumba vinavyopaswa kupangishwa na jiji.

Mariam Ukwaju na wenzake wakiwemo mafisa mapato, wameshindwa kuorodhesha baadhi ya maduka likiwemo Duka namba T 1 lililopo jengo la LEWICO ghorofa ya chini.

Duka hilo tangu mwaka 2009 mpaka Sasa, fedha zinazotokana na kodi ya chumba hicho, zimekuwa haziingii kwenye akaunti ya Serikali.

Fedha zote zinazopatikana kwenye chumba hicho na vingine viwili zinaingia kwenye mifuko ya watu hao watatu huku Serikali ikiambulia patupu..

Wakati fedha hizo zikipigwa na watu hao wachache, wanafunzi wanaosoma shuleni hapo baadhi yao wanakaa chini licha shule hiyo kuwa na miradi mikubwa.

Vyumba vya ghorofa ya chini vinaanzia na T 1 hadi T 18 na ghorofa ya kwanza kuna vyumba vinavyoanzia na T 19 hadi T 35.

Lakini kutokana na upigaji wa watumishi hao, duka T 1 ambalo lipo ghorofa ya chini halijaingizwa kwenye utaratibu wa upangishaji.

Uchunguzi uliofanywa na Mwandishi wa habari hii, unaonesha kuwa duka hilo, limebadilishwa namba na kuandikwa namba B 7.

Namba hiyo ni maduka yaliyopo eneo la upande wa pili unaotazamana na eneo la Zuberi yanayomilikiwa na mwekezaji Albert Swai kupitia kampuni yake ya HILGO CONSTRUCTION.

Mwekezaji wa upande wa pili, kwa mujibu wa mkataba wake uliosainiwa Oktaba 31 mwaka 2008 unaonesha kuwa mwekezaji huyo ana maduka 24.

Maduka hayo ya Albert Swai yanayoanza na namba B 1 - B 6, C 1 - C 6, D 1 - D 6 na E 1 - E 6 ambayo ujenzi wake ulifanyika 2009.

Maduka ya LEWICO kwa mujibu wa mkataba wake na shule ya pamba, yapo maduka 44 ambapo kwa sasa yapo maduka 47

Maduka mengine matatu yaliongezeka aliyanunua kutoka kwa mfanyabiashara mmoja anayefahamika kwa jina la MZIYA mwaka 2009.

Lakini kutokana na ubadhilifu unaliopo kwa watumishi hao wamechukua duka hilo na kulipa namba B 7 ambapo fedha inayopatikana huipiga.

Fedha zinazopigwa na watumishi hao ambao sio waaminifu ni kwenye duka hilo la T 1 tangu kipindi hicho.

mpaka sasa fedha zilizopigwa na watumishi hao ambao sio waadilifu ni Tsh. milioni 190

Maduka mengine ambayo fedha zake zinapigwa ni katika maduka T 14 na T 15 yaliyopo jengo la Pamba - LEWICO.

Mariam na wenzake ni miongoni mwa watu wanaotuhumiwa na wafanyabiashara kwa kuibua migogoro ya mara kwa mara inayohusu upangishaji wa vyumba vya biashara na miradi mingine.

Mwisho
 

Attachments

  • IMG20201230112227.jpg
    IMG20201230112227.jpg
    97.2 KB · Views: 8
  • IMG_20201230_112302.jpg
    IMG_20201230_112302.jpg
    121.9 KB · Views: 7
Pole kwa Mariam na wenzako wawili
Watanzania siku hizi wanasema sababu wanasikilizwa...... sasa ndio mshasemelewa hivyo, jipangeni na maelezo yanayoeleweka vinginevyo mtaingia kwenye lile kundi
 
Haya ndiyo yale matundu niliyokuwa nayasema ,

Wengine wanakusanya kuna ambao wao wapo busy kutengeneza matundu.
 
Pole kwa Mariam na wenzako wawili
Watanzania siku hizi wanasema sababu wanasikilizwa...... sasa ndio mshasemelewa hivyo, jipangeni na maelezo yanayoeleweka vinginevyo mtaingia kwenye lile kundi
Hakuna anaye taka kuishi kinyonge
Kwann wenzetu wawe na majumba mazuri twna syo moja,magari mazuri pia

Ova
 
Hawa wasingekuwa walafi wasingekamatwa! Ukiwa mchoyo lazima uharibiwe
 
Unaona Raha ya bunge la kijan?? Hakuna mtu wa kuhoji ni mpaka ktl mitandao, ccm oyeeee
Ufisadi jiji la Mwanza, Mwanasheria jiji Mwanza na wenzake wawili wapiga Tsh ML. 190

Jiji la Mwanza limegubikwa na vitendo vya ufisadi unaofanywa na baadhi ya watumishi wasiokuwa waadilifu wanaoenda rushwa.

Watumishi hao ni Mwanasheria wa jiji la Mwanza Mariam Ukwaju na wenzake wawili ambao wanatuhumiwa kula shilingi milioni 190.

Fedha zilizopigwa na watumishi hao ni kutoka mradi uliopo shule ya Sekondari ya Pamba ya jijini Mwanza.

Fedha hizo zinatokana na baadhi ya vyumba vilivyopo katika jengo hilo ambavyo havijaorodheshwa kwenye idadi ya vyumba vinavyopaswa kupangishwa na jiji.

Mariam Ukwaju na wenzake wakiwemo mafisa mapato, wameshindwa kuorodhesha baadhi ya maduka likiwemo Duka namba T 1 lililopo jengo la LEWICO ghorofa ya chini.

Duka hilo tangu mwaka 2009 mpaka Sasa, fedha zinazotokana na kodi ya chumba hicho, zimekuwa haziingii kwenye akaunti ya Serikali.

Fedha zote zinazopatikana kwenye chumba hicho na vingine viwili zinaingia kwenye mifuko ya watu hao watatu huku Serikali ikiambulia patupu..

Wakati fedha hizo zikipigwa na watu hao wachache, wanafunzi wanaosoma shuleni hapo baadhi yao wanakaa chini licha shule hiyo kuwa na miradi mikubwa.

Vyumba vya ghorofa ya chini vinaanzia na T 1 hadi T 18 na ghorofa ya kwanza kuna vyumba vinavyoanzia na T 19 hadi T 35.

Lakini kutokana na upigaji wa watumishi hao, duka T 1 ambalo lipo ghorofa ya chini halijaingizwa kwenye utaratibu wa upangishaji.

Uchunguzi uliofanywa na Mwandishi wa habari hii, unaonesha kuwa duka hilo, limebadilishwa namba na kuandikwa namba B 7.

Namba hiyo ni maduka yaliyopo eneo la upande wa pili unaotazamana na eneo la Zuberi yanayomilikiwa na mwekezaji Albert Swai kupitia kampuni yake ya HILGO CONSTRUCTION.

Mwekezaji wa upande wa pili, kwa mujibu wa mkataba wake uliosainiwa Oktaba 31 mwaka 2008 unaonesha kuwa mwekezaji huyo ana maduka 24.

Maduka hayo ya Albert Swai yanayoanza na namba B 1 - B 6, C 1 - C 6, D 1 - D 6 na E 1 - E 6 ambayo ujenzi wake ulifanyika 2009.

Maduka ya LEWICO kwa mujibu wa mkataba wake na shule ya pamba, yapo maduka 44 ambapo kwa sasa yapo maduka 47

Maduka mengine matatu yaliongezeka aliyanunua kutoka kwa mfanyabiashara mmoja anayefahamika kwa jina la MZIYA mwaka 2009.

Lakini kutokana na ubadhilifu unaliopo kwa watumishi hao wamechukua duka hilo na kulipa namba B 7 ambapo fedha inayopatikana huipiga.

Fedha zinazopigwa na watumishi hao ambao sio waaminifu ni kwenye duka hilo la T 1 tangu kipindi hicho.

mpaka sasa fedha zilizopigwa na watumishi hao ambao sio waadilifu ni Tsh. milioni 190

Maduka mengine ambayo fedha zake zinapigwa ni katika maduka T 14 na T 15 yaliyopo jengo la Pamba - LEWICO.

Mariam na wenzake ni miongoni mwa watu wanaotuhumiwa na wafanyabiashara kwa kuibua migogoro ya mara kwa mara inayohusu upangishaji wa vyumba vya biashara na miradi mingine.

Mwisho
 
Utasikia Meko kaleta nidhamu ya kazi huwa nacheka Sana ukitaka ukweli fuatilia taarifa ya CAG kwa mlio nje ya serikali
 
Back
Top Bottom