Ufanye nini mwenye pesa akikupora mke?

Ufanye nini mwenye pesa akikupora mke?

Mke haporwi! Mke anaenda mwenyewe! Ukisema kaporwa manake kalazimishwa au kabakwa!
Jiulize kwa nini kakuacha wewe kaenda kwa mwingine? Hakutaki huyo! Huna haja ya kumbembeleza au kupambana na mume mwenzio!
Muache aende salama mpe na nauli!
Atafunzwa na dunia!
 
Jamaa ana pesa, nguvu ya ushawishi, vyombo vyote vya dola kaviweka mkononi.
Sasa umegundua anatembea na mkeo umejaribu kumkanya mkeo, mkeo anakujibu ukifanya lolote bwana mapesa atakupotezea jela.
He ufanyeje
Kama naye ana mke jipendekeze au jilengeshe kwa mke wake....nawe utalelewa kiaina....
 
Jamaa ana pesa, nguvu ya ushawishi, vyombo vyote vya dola kaviweka mkononi.
Sasa umegundua anatembea na mkeo umejaribu kumkanya mkeo, mkeo anakujibu ukifanya lolote bwana mapesa atakupotezea jela.
He ufanyeje
Achana nae tumia fursa hiyo kuchagua Tena mtoto mkali endelea na maisha
 
Waganga wapo sana...
Laki moja ya kuweka mambo sawa haitanihangaisha sana.
 
Kama mmezaa watoto je?
Huyo anaekuja atawalea na kwasasa wabaki na house girl na kama wamefikia umri wa shule hawana shida hao, ila ukiendelea kumg'ang'ania huy mke wako wewe ndio utaumia mzee mwenzangu move on angalia watoto fanya mambo Yako coz hata ukifanikiwa kumrudisha mtangalianaje humo ndan! Je? Ile heshima itaendelea kuwepo
so sisi wanaume wenzio tutakushauri piga chini ila wewe ndio mwenye uamuzi wa mwisho coz unajuwa reason behind mpaka mkafikia hapo
Maybe ww ndio ulianza kucheat so zamu Yako kulipiziwa kwahiyo tulia dose ikuingie atarudi muamze upya
 
Jamaa ana pesa, nguvu ya ushawishi, vyombo vyote vya dola kaviweka mkononi.
Sasa umegundua anatembea na mkeo umejaribu kumkanya mkeo, mkeo anakujibu ukifanya lolote bwana mapesa atakupotezea jela.
He ufanyeje
Mimi nyumba ya udongo sihimili vishindo,mpe talaka muachane kwa amani aende kwa amani
 
Jamaa ana pesa, nguvu ya ushawishi, vyombo vyote vya dola kaviweka mkononi.
Sasa umegundua anatembea na mkeo umejaribu kumkanya mkeo, mkeo anakujibu ukifanya lolote bwana mapesa atakupotezea jela.
He ufanyeje

Unamwacha mke wako, hata kama Hana hela, we unamwacha mke wako, ajakupora wala, mke wako hakupendi na hakutaki, utalazimisha?
 
Mkuu kwani angekufa we usingeendelea kuishi?
Seti akili Yako kuwa amekufa, mtoe akilini tu, ujue muda unaoutumia kumuwaza ndo muda unaupoteza kutafuta Hela, halafu huyo mwanamke sio mtoto mdogo useme amebakwa, kaipeleka mwenyewe, afu unaweza kuwa unawaza kuwa mke kachukuliwa sababu ya Pesa kumbe mke kamwelewa tu jamaa, ni vyema kuchunguza tabia za mwenza wako kabla ya kufunga hizo mnazoita pingu za maisha, kumbuka mtu hujaribiwa Kwa tamaa zake mwenyewe, kimsingi jamaa Hana kosa na kosa lipo Kwa mwanamke wako!
Hapo atatumika na baada ya muda jamaa ataichoka, na kingine mkuu ukiwa na Hela wanawake huwa wanajileta tu huna haja ya kutia sound, na huwa hawaoneani wivu hata wawe 100 maana wote huamini wakikaa karibu na uwaridi lazima watanukia! So fanya Yako!
 
Jamaa ana pesa, nguvu ya ushawishi, vyombo vyote vya dola kaviweka mkononi.
Sasa umegundua anatembea na mkeo umejaribu kumkanya mkeo, mkeo anakujibu ukifanya lolote bwana mapesa atakupotezea jela.
He ufanyeje
Mwanamke sio nyumba ukiona kachepuka tena wazi wazi huyo sio wako achana naye katafute wako.
 
Back
Top Bottom