Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,177
- 34,444
UFALME WA NUGUTU
Mtunzi – Nea Makala
Sehemu ya 1
+255 713 373731
"Wanakuja hao..! Hakikisha hamna anayetoroka akiwa hai!",
"Sawa mkuu, shambuliaa......"
zilikuwa kauli za Viongozi wa jeshi la ufalme wa nchi ya Nugutu, ambao waliamuru maadui zao wote kuangamizwa na asibaki hata mmoja, ivyo agizo lao lilitimizwa na mashujaa wao na kuleta ushindi kwa nchi yao.
"Uishi miaka mingi Nugutu, Kimbilio la wanyonge Nugutu, Nchi yenye Baraka na neema Nugutu"
Mashujaa wa Nugutu waliendelea kuimba huku wakirejea nyumbani kwa furaha sana. Wakiwa karibu kabisa na lango la kuingilia kwenye ufalme wao, tayari wake zao na watu wengine walishajipanga kwa ngoma, makofi na nderemo kushangilia ushindi ulioletwa na makamanda wao.
Nugutu ni nchi inayoongozwa kwa kuzingatia mashauri ya wazee wenye hekima na hata wale wenye ukaribu zaidi na miungu, Hivyo katika maamuzi yeyote yanayohusu wananchi au nchi kwa ujumla, lazima wazee wakae waombe miungu yao ili iwaoneshe njia sahihi ya kuamua. Ushindi wao ulichagizwa na maamuzi yenye busara pamoja na maombi kwa miungu ya Nugutu.
"Ndugu zangu wananchi, afya ya mfalme wetu si nzuri ivyo kuanzia kesho tutaanza maombi kwa miungu yetu ndani ya siku 9, hili kujua ni mtoto yupi sahihi kushika nafasi ya mfalme Gaiya"
Yalikuwa maneno ya msemaji wa mfalme akitoa taarifa kwa umma wa Nugutu, sherehe ziliendelea huku kila mmoja akifikilia lake juu ya mrithi wa ufalme wa Nugutu ukizingatia mfalme Gaiya alikuwa na wake 6 na watoto 32 ivyo ilikuwa kazi ngumu kutabiri nani hasa atashika milki ya baba yake.
Siku zikasogea hatimaye siku ya 9 ikabisha hodi, wazee wakakusanyika barazani tayari kuongea na mfalme Gaiya juu ya mrithi wake. Wazee na wakuu wa kila idara wakawa tayari kusikiliza ni nani aliyeteuliwa na miungu ya Nugutu kushika nafasi ya Mfalme Gaiya,
"Uishi miaka mingi mfalme"
"Uishi..!!"
Mzee mmoja alisema na wenzake wakaitikia na kuinamisha vichwa vyao chini kutoa heshima kwa mfalme, ambaye alijikongoja na kufika hapo barazani kusikiliza nani aliyeteuliwa kuwa mtawala wa Nugutu.
"Mheshimiwa mfalme! Utukuke sana! Kama ilivyo ada kwa wazee na wananchi kufanya maombi na matambiko kwa miungu ya Nugutu, kila linapokuja swala linalohitaji maamuzi magumu. Mfalme mtukufu tunasikitika kukwambia kuwa kati ya vijana wako 20 wa kiume hamna hata mmoja aliyeidhinishwa na miungu yetu kushika nafasi yako, na kwa vyovyote itakavyokuwa ufalme hauwezi kwenda nje ya kizazi chako kitukufu," alisema Mzee Bongwa ambaye ndiye msemaji mkuu wa wazee.
Mfalme akashtushwa sana na taarifa hiyo, minong'ono ya chinichini ikaanza tapakaa ndani ya baraza lile, mfalme akavunja mkutano na kuahidi kulitolea ufumbuzi swala hilo ndani ya saa 72.
**************
Mfalme akaamua kweenda kwenye hazina za siri na muhimu sana ambazo mfalme pekee ndio ustahili kuingia humo, mbali na ugonjwa wake mfalme akajikongongoja huku akisindikizwa na jeshi lake na alipokaribia hazina hiyo ya kifalme, akaamuru jeshi limsubiri kisha yeye pekee akaendelea na safari na kuingia ndani ya pango ambapo hazina ya kifalme imeifadhiwa humo. Alipoingia upepo mkali ukavuma, ardhi ikatetemeka radi ikapiga, mfalme akachoma ubani na kupiga magoti hali ile iliendelea kwa muda wa saa 3 mfululizo kisha mfalme akaanguka na kupoteza fahamu.
Siku mbili zikapita bila kuwa na taarifa yeyote juu ya mfalme, wanajeshi walioambatana na mfalme wakaanza kuingiwa na hofu uenda kitu kibaya kimemkuta mfalme wao, hata hivyo wakashauriana waendelee kusubiri. Siku ya tatu asubuhi na mapema wakaona mfalme Gaiya akitokeza huku akiwa amebeba kifurushi kilichofungwa fungwa vizuri kwa kitambaa cheupe, wakainamana chini na kutoa heshima zao kwa mfalme.
"Kuna kazi moja ya kufanya kabla hatujarudi Nugutu, ni lazima twende Kigomile huko ndiko iliko nuru na hatima ya ufalme wa Nugutu" alisema mfalme.
"Na iwe kama ulivyosema mfalme," wanajeshi wakaitikia na kuinamisha vichwa vyao na kuanza safari ya kuelekea Kigomile.
*****************
Katika jumba la kifalme sintofahamu ikaendelea kutawala vichwani mwa wazee wa baraza, malkia na hata watoto wa mfalme kwani ni takribani siku 5 zimepita toka mfalme aondoke katika milki yake. Hawakupata taarifa yeyote kuhusu yeye wala jeshi aliloondoka nalo, ikabidi malkia aitishe kikao cha dharua kwa wazee wa baraza na wakuu wa kila idara.
"Hatuwezi kuendelea kukaa bila kuwa na kiongozi, siku 5 zimepita na hatuna taarifa yeyote juu ya mfalme, mimi nashauri tumteue mtoto wa kwanza wa mfalme ashike nafasi yake hadi atakaporejea mfalme Gaiya," alisema malkia ambaye ni mke wa kwanza wa mfalme.
Baraza la wazee likabaki kuitafakari ile kauli ambayo malkia aliitamka, mgawanyiko ukatokea baadhi ya wazee wakaungana na kauli ya malkia na wengine wakapinga na kutaka waendelee kusubiri, majibishano yakawa makali zaidi huku kila upande ukitetea hoja zake.
"Kuna vitu vya kupuuzia lakini si miiko na maagizo ya miungu ya Nugutu, haina haja kuingiza maswala binafsi katika hatima ya ufalme huu wa nchi hii, tunaweza kujiweka hatarini kwa kutokufikiri kwetu, lazima tusubiri hadi mfalme atakapo rejea ndivyo mambo mengine yataendelea," Alisema mzee Bongwa.
Maneno ya mzee huyo yakawanyamazisha wazee ambao walishaanza kutoka nje ya miiko ya Nugutu, lakini uchu wa madaraka ukamfanya Malkia atake kupindisha baadhi ya sheria na kwa gharama yeyote ile mtoto wake aapishwe kuwa mfalme wa Nugutu.
"Sawa tutasubili kwa siku 2 zaidi hadi siku ya 7 kama hakutokuwa na taarifa yeyote basi mtoto wangu lazima aapishwe na kuwa mtawala wa Nugutu" alisema malkia.
Tofauti iliyopo kati ya nchi ya kifalme ya Nugutu na falme nyingine ni mke wa mfalme kuwa na nguvu ya kuamua mambo pale mumewe anapokuwa nje ya ufalme.
***************
Mfalme na jeshi lake wakafika katika nchi ya kigomile, ikawalazimu kupia njia ya msituni ili kutokea sehemu ambayo mfalme aliikusudia. Kadri walivyozidi kuyakaribia makazi ya watu ndivyo kelele za vilio zenye kuomba msaada zilivyozidi kusikika masikioni mwao. Wakaongeza mwendo hili kujua kilichojili, wakafika na kukuta watu wengi wakiwa wameuawa na mali zao kuchukuliwa na nyingine kuteketezwa. Mfalme na jeshi lake lenye vijana wapatao 100 wakasogea kijijini hapo kwa tahadhari kubwa, akaamuru jeshi litawanyike na kutoa msaada kwa majeruhi waliosalia. Mbali na kuwa mtawala wa nchi ya Nugutu, mfalme Gaiya alisifika kwa roho ya huruma, karibu kila falme ilitambua hilo. Wakati wanajeshi wake wakiendelea kutoa msaada ghafla wakajikuta wakiweka katikati ya jeshi kubwa la nchi ya Kigomile ambalo kwa kukadilia wanaweza fika wanajeshi 300.
"hatukutegema kama ninyi mnaweza kuleta maafa katika nchi yetu ya kigomile, kwa kuwa hamkutaka kuongea nasi na mkafika kuteketeza watu wangu wa kigomile na mali zao hivyo pasi kusita nasi lazima tuwaangamize" ilikuwa kauli ya kikakamavu iliyotolewa na mfalme wa kigomile dhidi ya mfalme wa Nugutu na wanajeshi wake.
Mhmh! Unahisi nini kitafata!
Mtunzi – Nea Makala
Sehemu ya 1
+255 713 373731
"Wanakuja hao..! Hakikisha hamna anayetoroka akiwa hai!",
"Sawa mkuu, shambuliaa......"
zilikuwa kauli za Viongozi wa jeshi la ufalme wa nchi ya Nugutu, ambao waliamuru maadui zao wote kuangamizwa na asibaki hata mmoja, ivyo agizo lao lilitimizwa na mashujaa wao na kuleta ushindi kwa nchi yao.
"Uishi miaka mingi Nugutu, Kimbilio la wanyonge Nugutu, Nchi yenye Baraka na neema Nugutu"
Mashujaa wa Nugutu waliendelea kuimba huku wakirejea nyumbani kwa furaha sana. Wakiwa karibu kabisa na lango la kuingilia kwenye ufalme wao, tayari wake zao na watu wengine walishajipanga kwa ngoma, makofi na nderemo kushangilia ushindi ulioletwa na makamanda wao.
Nugutu ni nchi inayoongozwa kwa kuzingatia mashauri ya wazee wenye hekima na hata wale wenye ukaribu zaidi na miungu, Hivyo katika maamuzi yeyote yanayohusu wananchi au nchi kwa ujumla, lazima wazee wakae waombe miungu yao ili iwaoneshe njia sahihi ya kuamua. Ushindi wao ulichagizwa na maamuzi yenye busara pamoja na maombi kwa miungu ya Nugutu.
"Ndugu zangu wananchi, afya ya mfalme wetu si nzuri ivyo kuanzia kesho tutaanza maombi kwa miungu yetu ndani ya siku 9, hili kujua ni mtoto yupi sahihi kushika nafasi ya mfalme Gaiya"
Yalikuwa maneno ya msemaji wa mfalme akitoa taarifa kwa umma wa Nugutu, sherehe ziliendelea huku kila mmoja akifikilia lake juu ya mrithi wa ufalme wa Nugutu ukizingatia mfalme Gaiya alikuwa na wake 6 na watoto 32 ivyo ilikuwa kazi ngumu kutabiri nani hasa atashika milki ya baba yake.
Siku zikasogea hatimaye siku ya 9 ikabisha hodi, wazee wakakusanyika barazani tayari kuongea na mfalme Gaiya juu ya mrithi wake. Wazee na wakuu wa kila idara wakawa tayari kusikiliza ni nani aliyeteuliwa na miungu ya Nugutu kushika nafasi ya Mfalme Gaiya,
"Uishi miaka mingi mfalme"
"Uishi..!!"
Mzee mmoja alisema na wenzake wakaitikia na kuinamisha vichwa vyao chini kutoa heshima kwa mfalme, ambaye alijikongoja na kufika hapo barazani kusikiliza nani aliyeteuliwa kuwa mtawala wa Nugutu.
"Mheshimiwa mfalme! Utukuke sana! Kama ilivyo ada kwa wazee na wananchi kufanya maombi na matambiko kwa miungu ya Nugutu, kila linapokuja swala linalohitaji maamuzi magumu. Mfalme mtukufu tunasikitika kukwambia kuwa kati ya vijana wako 20 wa kiume hamna hata mmoja aliyeidhinishwa na miungu yetu kushika nafasi yako, na kwa vyovyote itakavyokuwa ufalme hauwezi kwenda nje ya kizazi chako kitukufu," alisema Mzee Bongwa ambaye ndiye msemaji mkuu wa wazee.
Mfalme akashtushwa sana na taarifa hiyo, minong'ono ya chinichini ikaanza tapakaa ndani ya baraza lile, mfalme akavunja mkutano na kuahidi kulitolea ufumbuzi swala hilo ndani ya saa 72.
**************
Mfalme akaamua kweenda kwenye hazina za siri na muhimu sana ambazo mfalme pekee ndio ustahili kuingia humo, mbali na ugonjwa wake mfalme akajikongongoja huku akisindikizwa na jeshi lake na alipokaribia hazina hiyo ya kifalme, akaamuru jeshi limsubiri kisha yeye pekee akaendelea na safari na kuingia ndani ya pango ambapo hazina ya kifalme imeifadhiwa humo. Alipoingia upepo mkali ukavuma, ardhi ikatetemeka radi ikapiga, mfalme akachoma ubani na kupiga magoti hali ile iliendelea kwa muda wa saa 3 mfululizo kisha mfalme akaanguka na kupoteza fahamu.
Siku mbili zikapita bila kuwa na taarifa yeyote juu ya mfalme, wanajeshi walioambatana na mfalme wakaanza kuingiwa na hofu uenda kitu kibaya kimemkuta mfalme wao, hata hivyo wakashauriana waendelee kusubiri. Siku ya tatu asubuhi na mapema wakaona mfalme Gaiya akitokeza huku akiwa amebeba kifurushi kilichofungwa fungwa vizuri kwa kitambaa cheupe, wakainamana chini na kutoa heshima zao kwa mfalme.
"Kuna kazi moja ya kufanya kabla hatujarudi Nugutu, ni lazima twende Kigomile huko ndiko iliko nuru na hatima ya ufalme wa Nugutu" alisema mfalme.
"Na iwe kama ulivyosema mfalme," wanajeshi wakaitikia na kuinamisha vichwa vyao na kuanza safari ya kuelekea Kigomile.
*****************
Katika jumba la kifalme sintofahamu ikaendelea kutawala vichwani mwa wazee wa baraza, malkia na hata watoto wa mfalme kwani ni takribani siku 5 zimepita toka mfalme aondoke katika milki yake. Hawakupata taarifa yeyote kuhusu yeye wala jeshi aliloondoka nalo, ikabidi malkia aitishe kikao cha dharua kwa wazee wa baraza na wakuu wa kila idara.
"Hatuwezi kuendelea kukaa bila kuwa na kiongozi, siku 5 zimepita na hatuna taarifa yeyote juu ya mfalme, mimi nashauri tumteue mtoto wa kwanza wa mfalme ashike nafasi yake hadi atakaporejea mfalme Gaiya," alisema malkia ambaye ni mke wa kwanza wa mfalme.
Baraza la wazee likabaki kuitafakari ile kauli ambayo malkia aliitamka, mgawanyiko ukatokea baadhi ya wazee wakaungana na kauli ya malkia na wengine wakapinga na kutaka waendelee kusubiri, majibishano yakawa makali zaidi huku kila upande ukitetea hoja zake.
"Kuna vitu vya kupuuzia lakini si miiko na maagizo ya miungu ya Nugutu, haina haja kuingiza maswala binafsi katika hatima ya ufalme huu wa nchi hii, tunaweza kujiweka hatarini kwa kutokufikiri kwetu, lazima tusubiri hadi mfalme atakapo rejea ndivyo mambo mengine yataendelea," Alisema mzee Bongwa.
Maneno ya mzee huyo yakawanyamazisha wazee ambao walishaanza kutoka nje ya miiko ya Nugutu, lakini uchu wa madaraka ukamfanya Malkia atake kupindisha baadhi ya sheria na kwa gharama yeyote ile mtoto wake aapishwe kuwa mfalme wa Nugutu.
"Sawa tutasubili kwa siku 2 zaidi hadi siku ya 7 kama hakutokuwa na taarifa yeyote basi mtoto wangu lazima aapishwe na kuwa mtawala wa Nugutu" alisema malkia.
Tofauti iliyopo kati ya nchi ya kifalme ya Nugutu na falme nyingine ni mke wa mfalme kuwa na nguvu ya kuamua mambo pale mumewe anapokuwa nje ya ufalme.
***************
Mfalme na jeshi lake wakafika katika nchi ya kigomile, ikawalazimu kupia njia ya msituni ili kutokea sehemu ambayo mfalme aliikusudia. Kadri walivyozidi kuyakaribia makazi ya watu ndivyo kelele za vilio zenye kuomba msaada zilivyozidi kusikika masikioni mwao. Wakaongeza mwendo hili kujua kilichojili, wakafika na kukuta watu wengi wakiwa wameuawa na mali zao kuchukuliwa na nyingine kuteketezwa. Mfalme na jeshi lake lenye vijana wapatao 100 wakasogea kijijini hapo kwa tahadhari kubwa, akaamuru jeshi litawanyike na kutoa msaada kwa majeruhi waliosalia. Mbali na kuwa mtawala wa nchi ya Nugutu, mfalme Gaiya alisifika kwa roho ya huruma, karibu kila falme ilitambua hilo. Wakati wanajeshi wake wakiendelea kutoa msaada ghafla wakajikuta wakiweka katikati ya jeshi kubwa la nchi ya Kigomile ambalo kwa kukadilia wanaweza fika wanajeshi 300.
"hatukutegema kama ninyi mnaweza kuleta maafa katika nchi yetu ya kigomile, kwa kuwa hamkutaka kuongea nasi na mkafika kuteketeza watu wangu wa kigomile na mali zao hivyo pasi kusita nasi lazima tuwaangamize" ilikuwa kauli ya kikakamavu iliyotolewa na mfalme wa kigomile dhidi ya mfalme wa Nugutu na wanajeshi wake.
Mhmh! Unahisi nini kitafata!