Infantry Soldier
JF-Expert Member
- Feb 18, 2012
- 15,893
- 16,317
Habari za wakati huu ndugu watanzania wenzangu. Kwa muda mrefu sasa nimekuwa na lundo la maswali ninayoishia kujiuliza mwenyewe na kukosa majibu sahihi. Hivi kwa nini hawa watanzania wenzetu (japo kuwa wanajibagua) wenye asili ya asia al maaruf kama WAHINDI waishio kwa wingi maeneo ya kati kati ya jiji la dar es salaam, hawashiriki katika ulinzi madhubuti wa taifa letu kwa kujitolea uwezo na nguvu zao katika vyombo vyetu vya ulinzi na usalama. Sijawahi kuona muhindi wanajeshi, polisi wala askari magereza ilhali wao pia ni watanzania na wanawajibu wa kulitumikia taifa letu kikamilifu na kwa uzalendo wote kwa kuwa nao pia wananufaika na amani inayopatikana kwa nguvu za wazalendo kutoka katika jamii nyingine za kitanzania kama wamatumbi, wamakonde na wengine wengi. Vipi likija suala la kupeleka wanafunzi wahitimu wa elimu ya secondary kwa mafunzo ya JKT, Je, na wao wataruhusu vijana wao wa KIHINDI kuhudhuria mafunzo hayo ya kikakamavu? Naombeni msaada wenu wa kimawazo. Napenda kuwasilisha. Asanteni sana.