Ufafanuzi kuhusu RAZABA

Ufafanuzi kuhusu RAZABA

Hatukuwai kuambiwa hapo nyums kuna RAZABA sijui kazabwa iweje leo?
Anyway kuna mchakato wa kujengwa bandari pale isijekuwa siyo yetu.
Tunywe mtori nyama ziko chini km tutazikuta🥲
ni ujinga wenu wa kutojua historia ya nchi yenu
 
Hamkufatilia tatizo RAzABA ilikuwepo miaka nenda rudi babu kijana

Ova
Naenda kusoma hii.
Ninachoongelea kuna wachina hawa wanapewa hiyo sehemu miaka 99wajenge bandari mahoteli.
Tutaambiwa ni ya Zanzibar
uchumi wa buluu.
Ndo mana ikaja brief report.
Wadanganyika tutanufaika nini.
 
ni ujinga wenu wa kutojua historia ya nchi yenu
Ninachoongelea kuna wachina hawa wanapewa hiyo sehemu miaka 99wajenge bandari mahoteli.
Tutaambiwa ni ya Zanzibar
uchumi wa buluu.
Ndo mana ikaja brief report.
Wadanganyika tutanufaika nini.
 
Watanganyika tunatakiwa tuamke kutoka usingizini. Hawa Wazanzibari tunawabeba, lakini hawabebeki. Ifikie wakati wajitegemee tu kama nchi kwa 100%.

Mimi sioni kama huu Muungano una tija kwa Tanganyika, zaidi tu ya kuwanufaisha Wazanzibari kwenye kila eneo.
 
Hili sakata la ardhi ya Bagamoyo ya hekari elfu sita kuwa ni mali ya Zanzibar lina ukakasi na halifai kupita bila ya kupata mawazo mbalimbali yenye lengo la kuboresha uelewa mpana wa raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Ni kweli Mwalimu Nyerere aliwapa Zanzibar ardhi ya Bagamoyo ili waweze kulima miaka hiyo ya sabini, hilo halina ubishi. Na pia ni kweli hayati Rais Magufuli akaja kuwapa wawekezaji wa Azam ardhi hiyo hiyo ili wafanye shughuli zao halali.

Kumuona Charles Hillary akipiga mkwara kwamba ardhi hiyo ni mali halali ya Zanzibar ndio kinapokuja kichekesho chenyewe.

Cession ni mchakato ambao sehemu ya ardhi ya nchi moja inatolewa rasmi na kuwa ni mali ya nchi nyingine, zipo sababu nyingi zenye kuyafikia maamuzi hayo.

Kwa kiswahili tunaita KUKOMA, yaani ardhi hiyo inakoma kuendelea kutumiwa na wakazi wa nchi husika inakuwa ni sehemu halali ya nchi nyingine na kiutaratibu inawekwa bandera ya nchi iliyoichukua kuanzia siku hiyo inapokoma kuwa ni mali ya nchi inapopatikana ardhi hiyo.

Je tangu miaka hiyo ya sabini kuna bendera yoyote inayopepea hapo Makurunge Bagamoyo kuonyesha kukoma kutumika kwa kipande hicho cha ardhi?, haijawahi kuwekwa bendera ya Zanzibar kuonyesha kuwa sehemu hiyo imekoma kuwa ni mali ya Tanzania, kiutaratibu bado ukubwa wa nchi ni ule ule unaotambulika kisheria tangu Tanzania ianze kuwa nchi kamili mwaka sitini na nne.

Hayati Rais Magufuli alikuwa na haki kabisa kumpatia muwekezaji Bakhresa sehemu ya ardhi iliyo chini yake kwa mujibu wa katiba. Kitendo cha Rais Mwinyi kuja na agizo la kufukuza waliopo katika ardhi hiyo wakati mchakato wa Cession haukuwahi kufanyika ni kosa la kiufundi la serikali anayoiongoza.

Naona kama wenye mamlaka ya kumshauri Rais Samia wameamua kutulia kwanza kutazama upepo wa huko juu utapita vipi. Wameliona hili kosa la kiufundi na nahisi ni suala litakalomalizwa kimya kimya tofauti na ule mkwara wa Charles Hillary alioutoa mbele ya media kule visiwani Unguja.

Mchakato wa Cession haukufanyika na hakuna bendera mahali pale yenye kuonyesha kuwa eneo limeshamilikishwa moja kwa moja kwa serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Hayati Magufuli alikuwa na haki zote kuligawa eneo hilo na pengine sababu za Mwalimu Nyerere kuwapa serikali ya Mapinduzi miaka hiyo ya sabini hazikuwa na mashiko ya muda mrefu, zilikuwa ni temporary measures.

Rais wa awamu ya nane Zanzibar na washauri wake wamechemka katika suala hili, warudi nyuma na wajipange upya kabla ya kutoka hewani na matamko yenye kuzua maswali mengi yenye utata ndani yake.

THE LAND WAS NOT CEDED TO ZANZIBAR BUT GIVEN FOR USE BUT STILL UNDER TANGANYIKA.

Credit: Phillipo Bukililo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ninachoongelea kuna wachina hawa wanapewa hiyo sehemu miaka 99wajenge bandari mahoteli.
Tutaambiwa ni ya Zanzibar
uchumi wa buluu.
Ndo mana ikaja brief report.
Wadanganyika tutanufaika nini.
munaanza na extrapolations za ajabu kabisa. Nani amesema kuwa bandari ya Bagamoyo itakuwa ya Zanzibar? hayo mumeongeza wenyewe na kila siku zikiendelea uzushi utazidi kunoga.
 
Hayati Mwalimu Nyerere alitoa eneo hilo ili kuwapa fursa Wazanzibari

View attachment 2643043

Sent using Jamii Forums mobile app
Shida iliyopo ni Katiba ya Sasa Kumpa Rais wa Jamhuri madaraka Makubwa ambayo wakati mwingine anafanya maamuzi ya Nchi nzima kwa kuongozwa na Utashi wake.

Katiba inasema Ardhi ni Mali ya Rais 😢

Kwahiyo hata kama itatokea Rais wa Sasa akaamua kuwa Ardhi ya Mkoa wa Dar Es Salaam aitoe kwa Wazanzibar kama Zawadi(Wakazi wa Dsm mumuombee Rais asichukue maoni yangu ya Utani akafanya kweli tu 😅) anakuwa hana makosa kwa kuwa amepewa mamlaka hayo na Katiba.

Ni muhimu tubadirishe hii Katiba kupata Mpya itakayo mpunguzia Rais Madaraka.
 
munaanza na extrapolations za ajabu kabisa. Nani amesema kuwa bandari ya Bagamoyo itakuwa ya Zanzibar? hayo mumeongeza wenyewe na kila siku zikiendelea uzushi utazidi kunoga.
Tupo hapa tunasubiri mtori uishe tuone nyama
 
Hatukuwai kuambiwa hapo nyums kuna RAZABA sijui kazabwa iweje leo?
Anyway kuna mchakato wa kujengwa bandari pale isijekuwa siyo yetu.
Tunywe mtori nyama ziko chini km tutazikuta🥲
Hili nalo neno la kupatiwa maelezo!
 
Hili mbona liko wazi Kuna shida kubwa sana ya Watanganyika kutokujua historia Na Kwani Smz KUWA na ardhi NDANINYA TANGANYIKA nikosa !!! mbona sisi Tz tuna majengo ya ubakozi tunamiliki mataifa mengi tu
ni ranchi tu, inaweza kuwa revoked kama ardhi yeyote ya tz inavyoweza kuwa revoked. ila sio zanzibar ndani ya Tanganyika.
 
we ndio mjinga, wazee walikuwa na akili, kila jambo linafanywa kwasababu zake
 
wana nyaraka? lipo kwenye muungano? kama hivyo vitu havipo, waliuziwa mbuzi kwenye gunia. hata leo hii mimi nikiwa rais, nafuta na nawafukuzia mbali kabisa. that day is coming.
 
Hili mbona liko wazi Kuna shida kubwa sana ya Watanganyika kutokujua historia Na Kwani Smz KUWA na ardhi NDANINYA TANGANYIKA nikosa !!! mbona sisi Tz tuna majengo ya ubakozi tunamiliki mataifa mengi tu
unaongea Kama huelewi mambo.tatizo Kuna ubaguzi ndo maana watanganyika wanaona Kama wanaibiwa Mali zao , haiwezekani mzanzibar anaruhusiwa kumiliki ardhi huku Tanzania lkn mtanzania haruhusiwi !!! ikumbukwe kwa Sasa wa zbar ni wengi sio laki 3 wa enzi za Uhuru. huu ndo uhuni na ubaguzi ambao haukubaliki kwa watanzania . huu muungano ni fake .. fake... fake.
 
Unaitwa Muungano, lakini kwa jicho la 3 hapa mfano wake, ni kama Tanzania bara kamuoa Zanzibar. Na wakati wa uchumba ndiyo kuhongwa Ranchi hiyo na bado mengi tutayasikia.

Sasa kipindi kamili cha ndoa ndiyo, hii kuhudumia mke sasa mara kafutiwa deni lote la umeme.
Unajua ile mke, anadekezwa na kupewa kila anachotaka. Ndiyo nikionacho hapo.
ubaya mke kawa na kiburi , mabwana wengi na anataka kujitawala bila kuingiliwa lolote!! Hii ndoa haikubaliki. Ni Kama. wanatukomoa hivi!!
 
Maaana halisi ya neno RAZABA ni Ranchi ya Zanzibar, Bagamoyo (Ranch of Zanzibar in Bagamoyo) Kwa simulizi kutoka kwa watangulizi wetu eneo la RAZABA ilikuwa ni zawadi ya Mwalimu Nyerere kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na lina ukubwa wa zaidi ya hekta elfu ishirini na nane.

Mto Wami, reli ya Tanga, Barabara ya Bagamoyo Msata, mto ruvu na bahari ya hindi ndio mipaka halisi ya RAZABA. Mmiliki wa RAZABA ni Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Kwa maana halisi, RAZABA ni eneo la Zanzibar ndani ya Tanganyika.

Hayati Mwalimu Nyerere alitoa eneo hilo ili kuwapa fursa Wazanzibari kumiliki mifugo yao wenyewe, na mifugo yote inayotoka maeneo ya Shinyanga, Tabora, Singida, Dodoma na kwingineko kwenda Zanzibar, ifikie RAZABA kabla ya kusafirishwa kwenda kutumiwa na wananchi wa Zanzibar.

View attachment 2643043View attachment 2643044

Sent using Jamii Forums mobile app
Shukrani kwa taarifa
 
Je Masharti au makubaliano ya Zanzibar kupewa eneo hilo yamekaa vipi?

Ikitokea Muungano unavunjika muda huu je, bado eneo hili litaendelea kumilikuwa na Zanzibar? Na itakuwaje yaani!
 
Back
Top Bottom