Ufafanuzi kuhusu RAZABA

Ufafanuzi kuhusu RAZABA

Maaana halisi ya neno RAZABA ni Ranchi ya Zanzibar, Bagamoyo (Ranch of Zanzibar in Bagamoyo) Kwa simulizi kutoka kwa watangulizi wetu eneo la RAZABA ilikuwa ni zawadi ya Mwalimu Nyerere kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na lina ukubwa wa zaidi ya hekta elfu ishirini na nane.

Mto Wami, reli ya Tanga, Barabara ya Bagamoyo Msata, mto ruvu na bahari ya hindi ndio mipaka halisi ya RAZABA. Mmiliki wa RAZABA ni Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Kwa maana halisi, RAZABA ni eneo la Zanzibar ndani ya Tanganyika.

Hayati Mwalimu Nyerere alitoa eneo hilo ili kuwapa fursa Wazanzibari kumiliki mifugo yao wenyewe, na mifugo yote inayotoka maeneo ya Shinyanga, Tabora, Singida, Dodoma na kwingineko kwenda Zanzibar, ifikie RAZABA kabla ya kusafirishwa kwenda kutumiwa na wananchi wa Zanzibar.

View attachment 2643043View attachment 2643044

Sent using Jamii Forums mobile app
Ukimsikiliza vzr yule bwana alikua anaitwa Ustaadhi Ilinga Hassan Kapungu kuna kitu kama nakua naelewa sana, na mbaya zaidi wao walichelewa, walitakiwaga toka enzi hizo waifanye Zanzibar kua kama mkoa ili kuondoa tofauti, lakini ilipofanywa kua Serikali, kuna namna ambavyo wao wanaona wazi kua walipolwa nchi yao, na hata leo hua wanatamani kujitenga muda wowote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hili mbona liko wazi Kuna shida kubwa sana ya Watanganyika kutokujua historia Na Kwani Smz KUWA na ardhi NDANINYA TANGANYIKA nikosa !!! mbona sisi Tz tuna majengo ya ubakozi tunamiliki mataifa mengi tu
Tofautisha majengo ya ubalozi na umiliki wa ardhi....kwani majengo ya ubalozi ndio umemiliki ardhi mazima.
 
Kwamba zawadi kutoka kwa Nyerere....who is Nyerere kwa maamuzi kama haya? Tatizo wanasheria wetu wamelala yooo...ingekua nchi nyingne vifungu vingetafsiriwa. Zanzibar ipo siku atasema dar ni sehemu yake walipewa zawadi na sultani....hahaaa
 
Kwa kipindi chote hicho eneo halijaendelezwa, karibia miaka 50.. kwa sasa mzani umeinama huwezi kuwatoa wananchi pale.

Sheria yetu ya ardhi pia iangaliwe upya, inakuaje mtu hajaendeleza eneo miaka yote hiyo na bado ana umiliki?

Sheria iwe miaka mitano, kama huna chakufanya eneo linarudi serikalini hatuwezi kufuga mapori miaka 50 halafu unawaita wanacnhi wavamizi. Wakajenge wapi mtu kahodhi ekari 6000 tangu Uhuru?
 
Maaana halisi ya neno RAZABA ni Ranchi ya Zanzibar, Bagamoyo (Ranch of Zanzibar in Bagamoyo) Kwa simulizi kutoka kwa watangulizi wetu eneo la RAZABA ilikuwa ni zawadi ya Mwalimu Nyerere kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na lina ukubwa wa zaidi ya hekta elfu ishirini na nane.

Mto Wami, reli ya Tanga, Barabara ya Bagamoyo Msata, mto ruvu na bahari ya hindi ndio mipaka halisi ya RAZABA. Mmiliki wa RAZABA ni Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Kwa maana halisi, RAZABA ni eneo la Zanzibar ndani ya Tanganyika.

Hayati Mwalimu Nyerere alitoa eneo hilo ili kuwapa fursa Wazanzibari kumiliki mifugo yao wenyewe, na mifugo yote inayotoka maeneo ya Shinyanga, Tabora, Singida, Dodoma na kwingineko kwenda Zanzibar, ifikie RAZABA kabla ya kusafirishwa kwenda kutumiwa na wananchi wa Zanzibar.

View attachment 2643043View attachment 2643044

Sent using Jamii Forums mobile app
Sheria ya ardhi kuwa chini ya Rais hapo imetumika vibaya.

Utaratibu wa kuwapatia Zanzibar ulifanyikaje?
 
tutawanyang'anya tu muungano ukifa.
FB_IMG_1685677007525.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sio Kila alichofanya Nyerere ni sahihi, hata yeye mwenyewe aliwahi kusema Kila awamu Ina mazuri na mabaya yake . Kitendo alichofanya Nyerere lilikuwa takwa lake binafsi na sio takwa la kikatiba Wala halikuwahi kupitisha bungeni hivyo kama kweli tunamuenzi tunatakiwa kuachana na mabaya yake na kuendeleza mazuri yake
 
Ardhi ya nchi haijawahi kuwa ya Nyerere, alikuwa msimamizi tu. Aliwatapeli. Hilo ni kama 280 Kmsqr, si eneo dogo.
 
Muungano wa sasa umeshikiliwa na uzi mwembamba sana wa kipengele cha siasa

Sent using Jamii Forums mobile app
Pamoja na kwamba sipaswi kulizungumza hili ila kila tukitawaliwa na Mzanzibari, huwa hajali mambo ya Bara as if inakuwa na donge! Ufisadi huzidi na huwa hawajali. Ukienda Zenji Ona wanavyojitanua. In fact nao wanasubiri tu uzi ukatike
 
Back
Top Bottom