UDSM-Law First Classes

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,196
25,516
Leo nimekumbuka historia hii kama kumbukumbu:
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam almaarufu kama UDSM kilianzishwa mwaka 1961 kikiwa na kitivo kimoja tu cha Sheria. Kilianzia Lumumba na sasa Mwalimu Julius Nyerere Mlimani Campus kikiwa na Koleji na Shule Kuu mbalimbali.

Tangu kuanzishwa kwake,Kitivo cha Sheria kimetoa wahitimu wanne tu waliokuwa na ufaulu wa Daraja la Kwanza(yaani First Class-GPA ya 4.4 hadi 5.0).

Hao ni Dr.Ringo William Tenga,Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi, Dr.Asha-Rose Mtengeti Migiro na Prof. Hamudi Ismail Majamba. Hawa wanastahili sifa.Wanastahili kuitwa 'the Big Four'.Tangu mwaka 1992,hakukuwa na Daraja la kwanza lingine.

Wengine tulijaribu lakini tukashindwa.Tukaishia na Daraja la Pili la Juu (Upper Second Class). Ikumbukwe kuwa,Kitivo cha Sheria ndicho kinachochukua wanafunzi wanaofaulu zaidi,'the Cream of the Nation' kwa masomo ya sanaa(lakini kwasasa TCU wanaleta hata daraja la pili).

Juhudi ziongezwe kwa wengine kupata Daraja la Kwanza kitivoni hapo.Wapo watakaoweza. Wajiunge na wastahili hao. Mazingira ya kujisomea UDSM yanaboreshwa kila kukicha. Inawezekana hata kwa wengine.
 
Poleni sana.Sasa wenzenu tulikuwa tunasoma Law of Contract ya units 6...mwaka mzima

duh kumbe pale tulionjeshwa tu...
Ila Perfect alifanya course iwe poa, class ni full chai...

Lakini unadhani sababu za kutopata first class ni nini? Kozi ngumu au ukiritimba?
 
duh kumbe pale tulionjeshwa tu...
Ila Perfect alifanya course iwe poa, class ni full chai...

Lakini unadhani sababu za kutopata first class ni nini? Kozi ngumu au ukiritimba?
Sijui kwakweli.LAKINI NADHANI MFUMO WA KUFUNDISHA KOZI KWA MWAKA MZIMA UNACHANGIA
 
Leo nimekumbuka historia hii kama kumbukumbu:
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam almaarufu kama UDSM kilianzishwa mwaka 1961 kikiwa na kitivo kimoja tu cha Sheria. Kilianzia Lumumba na sasa Mwalimu Julius Nyerere Mlimani Campus kikiwa na Koleji na Shule Kuu mbalimbali.

Tangu kuanzishwa kwake,Kitivo cha Sheria kimetoa wahitimu wanne tu waliokuwa na ufaulu wa Daraja la Kwanza(yaani First Class-GPA ya 4.4 hadi 5.0).

Hao ni Dr.Ringo William Tenga,Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi, Dr.Asha-Rose Mtengeti Migiro na Prof. Hamudi Ismail Majamba. Hawa wanastahili sifa.Wanastahili kuitwa 'the Big Four'.Tangu mwaka 1992,hakukuwa na Daraja la kwanza lingine.

Wengine tulijaribu lakini tukashindwa.Tukaishia na Daraja la Pili la Juu (Upper Second Class). Ikumbukwe kuwa,Kitivo cha Sheria ndicho kinachochukua wanafunzi wanaofaulu zaidi,'the Cream of the Nation' kwa masomo ya sanaa(lakini kwasasa TCU wanaleta hata daraja la pili).

Juhudi ziongezwe kwa wengine kupata Daraja la Kwanza kitivoni hapo.Wapo watakaoweza. Wajiunge na wastahili hao. Mazingira ya kujisomea UDSM yanaboreshwa kila kukicha. Inawezekana hata kwa wengine.

Sasa hata division three ni za kumwaga tu! unachezea utandawazi? vyuo vikuu sasa ni kila mahali zamani ilikuwa hivyo kwa sababu watu walikuwa hawana pa kwenda.
 
Hizo grade ni number tu, ila kwenye tasnia ya sheria tanzania hakuna na itachukua muda mrefu kuwapata kama wafuatao, James Mwalusanya (RIP), Kawa Lugakingira (RIP), Buxton Chipeta, Dan Mapigano, wote 4 walikuwa majaji. Prof. Maina Chris Peter, Twaha Ulimwengu (General Ulimwengu) Tundu Lissu, na Halima Mdee, hao uliowataja na first class zao ni sawa na Sofia Simba na masters yake ya Law japo hawezi kuongea sentence 2 za kiingereza
 
Hizo grade ni number tu, ila kwenye tasnia ya sheria tanzania hakuna na itachukua muda mrefu kuwapata kama wafuatao, James Mwalusanya (RIP), Kawa Lugakingira (RIP), Buxton Chipeta, Dan Mapigano, wote 4 walikuwa majaji. Prof. Maina Chris Peter, Twaha Ulimwengu (General Ulimwengu) Tundu Lissu, na Halima Mdee, hao uliowataja na first class zao ni sawa na Sofia Simba na masters yake ya Law japo hawezi kuongea sentence 2 za kiingereza

Hapo umenena mkuu,suala ni application hivyo vyeti ni mbwembwe tu!umenikumbusha yule mama aliyekuwa akiomba kura bungeni"ee my daily bread is engineering"
 
Leo nimekumbuka historia hii kama kumbukumbu:
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam almaarufu kama UDSM kilianzishwa mwaka 1961 kikiwa na kitivo kimoja tu cha Sheria. Kilianzia Lumumba na sasa Mwalimu Julius Nyerere Mlimani Campus kikiwa na Koleji na Shule Kuu mbalimbali.

Tangu kuanzishwa kwake,Kitivo cha Sheria kimetoa wahitimu wanne tu waliokuwa na ufaulu wa Daraja la Kwanza(yaani First Class-GPA ya 4.4 hadi 5.0).

Hao ni Dr.Ringo William Tenga,Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi, Dr.Asha-Rose Mtengeti Migiro na Prof. Hamudi Ismail Majamba. Hawa wanastahili sifa.Wanastahili kuitwa 'the Big Four'.Tangu mwaka 1992,hakukuwa na Daraja la kwanza lingine.

Wengine tulijaribu lakini tukashindwa.Tukaishia na Daraja la Pili la Juu (Upper Second Class). Ikumbukwe kuwa,Kitivo cha Sheria ndicho kinachochukua wanafunzi wanaofaulu zaidi,'the Cream of the Nation' kwa masomo ya sanaa(lakini kwasasa TCU wanaleta hata daraja la pili).

Juhudi ziongezwe kwa wengine kupata Daraja la Kwanza kitivoni hapo.Wapo watakaoweza. Wajiunge na wastahili hao. Mazingira ya kujisomea UDSM yanaboreshwa kila kukicha. Inawezekana hata kwa wengine.

Mimi UDSM nimesoma BCom ambako kila mwaka lazima First Class zitoke. Sheria tatizo ni watu kutokukubali historia zao kufutwa! I don't believe that Kabudi is the best lawyer this country has ever had! Yes is good but is not the best.

Wanafunzi wa UDSM hawa wanaotoka na Pass, Lower Second wanaonekana ni wazuri kuliko First Class wa vyuo vingi tu. Kwa heshima naomba nisitaje vyuo hivyo!

Mbali na Kitivo changu (FCM) na sasa UDBS ( Uni.of DSM Business School) kutokuwa na ukilitimba, UDSM kwa ujumla bado kuna walimu wapuuzi na wenye chuki. Nilishangaa nikiwa mwaka wa kwanza mwalimu wa IT anatuambia eti semester hii nataka A zisizidi 4. How can you say that before setting and marking an exam?

Nashukuru Mungu nilipata hivyo 1st Class kwa shughuli kweli kweli, na baadae nikachukua Masters UK tena kwenye chuo bora by far kuliko UDSM. Huko walimu lengo ni mwanafunzi afaulu. Wanafanya kila njia ufaulu na si kukukamata ili mradi uwezo unao! Kwanza chuo kinachukua wanafunzi bora, sasa ukifeli maana yake ni kwamba chuo hakijui kufundisha. Kuna wanafunzi rafiki yangu aliwahi kuniuliza, hivi si itakuwa vichekesho wanafunzi wote wa Cambridge kukosa First Class?

Sasa, mimi wakati nasoma UDSM, wanafunzi waliokuwa wanachaguliwa ni Div I & II. Hii ilikuwa ni kigezo cha wewe kupata msaada wa kusomeshwa na serikali. Sasa ndani ya hii cream eti mtu anafeli kabisa (discontinued)!

Kuweka ugumu wa shule haina maana ya ubora wa elimu. UDSM sasa ndio kwanza inazidi kupolomoka katika medani za taaluma duniani. Matokeo mapya ya mwaka 2012 yanaonyesha UDSM imepitwa hata na chuo cha juzi juzi ilichokizaa yenyewe, MUHAS (link URAP - University Ranking by Academic Performance )
 
Back
Top Bottom