Elimu inayotolewa vyuoni inaweza kuwa ni ile ile tu kwa vyuo vingi maana hata waalimu wa vyuo vingine wengi wanatokea udsm.
Ishu kubwa katika hivi vyuo ni uzito wa jina la chuo, baaasi??
Mtu anaweza kuwa na gpa ya 4.3 kutoka vyuo vingine lakini mtu wa Udsm mwenye gpa ya 2.9 akapewa uzito kwasababu tu kasoma udsm.
Ukiangalia vizuri unakuja kugundua vyeo vingi sana vya serikalini vya juu juu wengi ni wahitimu wa udsm, ni kama vile wanabebana kifamilia.
Kupata nafasi tu ya kusoma udsm ni heshima kubwa sana, mtu anaweza kawa kapata divisioni 3 form 4, division 3 form 6 lakini akiinga tu udsm ana uwanja mpana sana kuliko kipanga aliepiga division 1 kali form 4 na 6 ila akaishia kusomea vyuo vingine.
Kwa lugha nyepesi, UDSM NI BABA LAO!!