UDSM kunani hapo?

UDSM kunani hapo?

Who cares,? unataka nijue nini? kwenye ranks za Africa chuo kinajikita mkiani, website mbovu, elimu substandard, miundombinu hafifu,
By the way, hiki chuo sio chako, usihangaike kutetea, ni chetu Watanzania wote. Tusaidiane kukisaidia kwa kukosoa.
Hii itasaidia kuinua elimu yetu Mimi na wewe.
Umenena vyema.
 
kuna jamaa yangu aliwahi kwenda uholanzi baada ya kumaliza degree ya banking& finance pale IFM.Alipofika kule akaomba kazi na alipoenda kwenye interview akaonyesha cheti chake cha Ifm.Jamaa wakamjibu palepale kwamba hawakitambui hicho chuo wao kwa East Africa wanavitambua vyuo vitatu tu University of Makerere,UDSM na University of Nairobi kwahiyo jamaa akakosa kazi.

Tuache ushabiki wala nini UDSM kitaendelea kuwa amongst the best universities in Africa and international wise. Angalia kilivyokua na hazina kubwa ya wataalamu maprofesa,wahadhiri.

Kupata udahili UDSM inabidi uwe na first au second division.Licha ya TCU kuanzisha mfumo wa udahili wa pamoja kwa vyuo vyote yaani CAS Central Admission System bado vigezo vya kuchaguliwa kusoma UDSM ndio vigumu na vitaendelea kuwa hivyo kuliko vyuo vyote Tanzania kwa sababu hicho ndio chuo bora na kikongwe kuliko vyote.

Proudly to be UDSM alumni

Hakuna chuo duniani hujivunia vigezo vigumu kudahili. Ndio naona hapa. Maana kwangu hata div.3 ya pcm bado ni ufailu mzuri tu...(another topic though)
What is important ni product inayotoka ina nini cha kusaidia yeye na jamii yake.
 
Watz hatupendi kuumiza vichwa tupo kufanya yale yale kila siku ndio kinachotusumbua sio UDSM tu taasisi nyingi za kiserikali zipo kama zilivyo siku zote hakuna innovation
 
hahaaa pcm yako ya division three utapata udahili kwenye vyuo vya kata kama Udom na vinavyofanana na hivyo ila sio UDSM.

Kama unadhani ugumu wa kupata udahili vyuo kama hujafaulu vizuri jaribu kuomba udahili Harvard University, Oxford University au Cambridge University uone kama watakuchukua hahaaaa
 
Hahaha.
Hebu achana na picha, vipi kuhusu uhalisia wa haya majengo,
Ukipita kule kota za watumishi ni vile vile kama alivyoacha Mwalimu.

Hilo halina ubishi, nimeshawahi kukoswa na kipande cha zege pale hall 2 kilimeguka kutoka ghorofa za juu. Pia pale CoET cafeteria block A kama unapajua.. ukipiga upepo mkali kuna vipande vya bati madirishani huwa vinachomoka. Hivi tupoongea hapa bila uwepo wa Mungu wangu aliye hai huenda nisingekuwa na sikio moja. Majengo ni machakavu sio siri. Hapo hatujaingia ndani ya vyoo .. Bado hujakuta lift za hazijabuma upande ngazi ghorofa nane.. Ushuke uende darasani. Chemba za choo bado hajifanya yake hapo.
 
hahaaa pcm yako ya division three utapata udahili kwenye vyuo vya kata kama Udom na vinavyofanana na hivyo ila sio UDSM.

Kama unadhani ugumu wa kupata udahili vyuo kama hujafaulu vizuri jaribu kuomba udahili Harvard University, Oxford University au Cambridge University uone kama watakuchukua hahaaaa
Sasa hata nikipata div1 ya tatu HKL, halafu nikawa professor,
And I can not help to make the world better then what??? Hiyo div1 kazi yake nini?
Nadhani umeelewa namaanisha nini..!!
 
huyu jamaa anaonekana ni mpita njia, UDSM si kama ulivoielezea.
Nadhani,
Wasomi wa vyuo vikuku Nyakati hizi wabadilike/tubadilike, Wanakuwa wazito kukubali udhaifu wa baadhi ya vitu katika vyuo wanavyosoma na haswa wakiwa mtaani wakiulizwa wanashindwa kueleza udhaifu.

Hiki si kitu kizuri kabisa,lazima tuwemstari wa mbele kuondoa madhaifu kama yapo ili kizazi kinachokuja kipate Mambo yaliyo bora!
 
UDSM hovyo kabisa..nikiikumbuka library ilivyojaa mavitabu yaliyopitwa na wakati sina hamu, nakumbuka pale kulikuwa na baadhi ya vitabu vina copy 2 wakati kozi mnasoma zaidi ya watu 200...kinachotokea ni kuwahi foleni pale ili tu uwahi kitabu..ukichelewa ndo basi, bado upungufu wa vitabu ni mkubwa hasa shule ya biashara!!

Nafikiri majengo tu kuyajenga haina maana kama reources kama vitabu itakuwa shida kupata!!
 
Hata sisi hatutaki kujua undani wowote, tunataka kujua baadhi ya mambo tu ya kawaida kama vile Maabara, hapa najua wanafunzi wa MBB hukaririshwa theory pure, hawafanyi probing, wala sequencing, wala cloning. Sijui kama tunaongea lugha moja.
Na vipi kuhusu hii website ya Chuo?
Halafu usisahau kuwa products za UD ndio hizihizi huku mtaani, hata kujieleza tu ni mgogoro.
Labda unataka tujue nini, ?
Hapo kwenye kujieleza ni janga la taifa..UDSM unaionea bure! All in all kuna ujinga mwingi sana unaendelea pale, kile hakiwezi kuwa CHUO KIKUU ni CHOO KIKUU..

Wanafunzi wenyewe ustaarabu zero, wanatupa taka ovyo...chooni unakuta mpaka mawe humo ndani..vyoo hawaflash, viunga vikanyang'wa hovyo hovyo yani hapaeleweki!!
 
Maprofesa wana siasa, product ya pale wana siasa, pia faza house ex, na wasasa ni product ya ud, wanasiasa vilevile so hamna jambo linalo fanikiwa kwa siasa, uteuzi daily ni udsm, wachambuzi wa mambo ya kisiasa tz ni maprofu ud, Ata elimu Yao siasa siasa tu.
na mnao tetea mtupe fact za picha
mfano, uktaka kujinyonga kapande lift za Ud, hall no 5 na ukhtaji ngeo pia kaa nje kwa chini ya hilo block.
Mungu bariki Tanzania.
 
Tatizo la mwandishi viroba vinamsumbua, Tumia akili chuo kilijengwa lini na kipindi hicho miaka hiyo hayo majengo kwa Dar yalikuwa the best, huwezi bomoa kila kumbukumbu ili uendane na technology mpya, Ungeshauri wajenge Campus mpya zingine sio hayo mawazo ya viroba

baada ya kutoa ushauri, wewe unaanza kuleta kejeli na lugha zisizo na maana....

hata kama chuo ni cha kale ni vyema kukifanyia ukarabati, hata majengo ya kale ni vyema kuyapaka rangi itaongeza thamani walau kidogo....

old is gold endapo tu kutakuwa na modification, kinyume na hapo vya kale ni takataka....
 
...vyuo vingi vya kibongo ni majengo tu hamna kitu...kwa umri wa udsm kilitakiwa kiwe mfano kwa vyuo vingine lakini sivyo....hayo majengo yanayoonekana hayana wanafunzi mchana basi ujue usiku yanajaa wapiga ngono gizani...yani yanageuka gesti....na mda mwingi wanafunzi wanashnda hapo mlimani city mall wakila starehe....wanakua bize wakati wa mitihani tu...sasa hapo innovation zitoke wapi....wao innovation wanazifanyia kwenye ngono na mabinti wabichi wa chuo...kwama nani kamchapa demu gani mpya...ama nani kanunua nini na anatumiaje...hiyo ndiyo innovation inayotawala mind za wanafunzi mda wote...

...chuo pekee chenye kufanya vema sana sana tanzania nzima kwa innovation pamoja na uchanga wake ni chuo cha nelson mandela arusha...chuo hiki kimeanzishwa mwaka 2011 tu lakini kinatambulika tayari duniani.....ndio maana hata mwaka huu wamepewa hela ndefu na world bank na AfDB kwa ajili ya kuchukua wanafunzi africa nzima....
 
...vyuo vingi vya kibongo ni majengo tu hamna kitu...kwa umri wa udsm kilitakiwa kiwe mfano kwa vyuo vingine lakini sivyo....hayo majengo yanayoonekana hayana wanafunzi mchana basi ujue usiku yanajaa wapiga ngono gizani...yani yanageuka gesti....na mda mwingi wanafunzi wanashnda hapo mlimani city mall wakila starehe....wanakua bize wakati wa mitihani tu...sasa hapo innovation zitoke wapi....wao innovation wanazifanyia kwenye ngono na mabinti wabichi wa chuo...kwama nani kamchapa demu gani mpya...ama nani kanunua nini na anatumiaje...hiyo ndiyo innovation inayotawala mind za wanafunzi mda wote...

...chuo pekee chenye kufanya vema sana sana tanzania nzima kwa innovation pamoja na uchanga wake ni chuo cha nelson mandela arusha...chuo hiki kimeanzishwa mwaka 2011 tu lakini kinatambulika tayari duniani.....ndio maana hata mwaka huu wamepewa hela ndefu na world bank na AfDB kwa ajili ya kuchukua wanafunzi africa nzima....
Huwezi ku-generalize watu wote katika kundi la aina moja, wanafunzi wa UDSM utawalaumu kwa lipi? hayo majengo yanatakiwa kukatabatiwa na serikali yako, UDSM wana uongozi kamili kwani hawaoni haja ya kufanya marekebisho?

Wanafunzi kwenda mlimani city mall kunazuia majengo kukarabatiwa?

Unataka wafanye nini ikiwa wanakwenda huko kununua mahitaji? Ivi wewe enzi zako muda wote uliutumia kusoma? Ulikua hutembei au sehemu za kutembea hazikuwepo?

Rudi kwenye hoja ya msingi, majengo ya UDSM yamechakaa yarekebishwe.
 
kabla ya kuandika uwe unafanya utafiti mzee!
ntakujibu no1;kuna library kubwa inajengwa afrika mashariki na kati km sio afrika hapo katika kati ya yombo5 n udbs;na hayo majengo ya utawala hapo cass tower kutakuwa na daraja kubwa kutoka library mpk cass/coss tower!

na hayo mengine yote juhudi zinachukuliwa nenda flat research chin kaangalie majengo mapya,nenda coet chini kule kaangalie majengo mapya;hill park chin kachek;caftria ya yombo juu porini kule majengo mapya kachek!

#n.b kwa geografia ya mlimani majengo hayawez kurundikana sehemu moja,na km mgen unawez hiz ud inaishia utawala!
mkuu iyo coss tower huwoni ilivyo chok utasema kama lilejengo ni lakisasa

hayo majengo mpya ya coet yanatumika au ni yakufanyia UE tu mana sijwahi ona yakitumika

all in all chuo kinahitaji mabadiliko kama mtoa mda alivyosema
 
..wanasoma wakati wa mitihani...muda mwingi nawaona wakiranda city....hayo mahitaji unayosema labda bia...na penzi....issue ya mtoa hoja si majengo chakavu tu.....bali hata kutowaona wanafunzi wakijishughulisha na academics campus...haswa mchana...kwamba kama wanafunzi hawajibidishi je watavumbua lini??...kwamba hata lab za maana hazionekani chuoni pamoja na umri mkubwa wa chuo....hii ndio hoja....hayo ya mimi nilisomaje ni yako....


Huwezi ku-generalize watu wote katika kundi la aina moja, wanafunzi wa UDSM utawalaumu kwa lipi? hayo majengo yanatakiwa kukatabatiwa na serikali yako, UDSM wana uongozi kamili kwani hawaoni haja ya kufanya marekebisho?

Wanafunzi kwenda mlimani city mall kunazuia majengo kukarabatiwa?

Unataka wafanye nini ikiwa wanakwenda huko kununua mahitaji? Ivi wewe enzi zako muda wote uliutumia kusoma? Ulikua hutembei au sehemu za kutembea hazikuwepo?

Rudi kwenye hoja ya msingi, majengo ya UDSM yamechakaa yarekebishwe.
 
..wanasoma wakati wa mitihani...muda mwingi nawaona wakiranda city....hayo mahitaji unayosema labda bia...na penzi....issue ya mtoa hoja si majengo chakavu tu.....bali hata kutowaona wanafunzi wakijishughulisha na academics campus...haswa mchana...kwamba kama wanafunzi hawajibidishi je watavumbua lini??...kwamba hata lab za maana hazionekani chuoni pamoja na umri mkubwa wa chuo....hii ndio hoja....hayo ya mimi nilisomaje ni yako....
Hupajui pale wewe, ukiona watu wanakula bata UDSM inategemeana na kozi zao, kuna wale wa Fine and performing arts wanakula bata mpaka basi, sasa wewe unasoma Tele jichanganye wakate kichwa

Alafu pale wanafunzi ni wengi mno kipindi changu ilikua kama 18,000 sasa kinachofanyika ni kupishana venues sio wote mtakua class, pia ukumbuke usomaji wa chuo sio kama form six mkuu, chuo watu wanasoma na mambo mengine kama vibarua wanafanya cha msingi akili kumkichwa
 
Back
Top Bottom