UDSM kunani hapo?

UDSM kunani hapo?

ea0b41d84cb5db9b7a95797b096b950e.jpg

Hapo business School pako bomba sana.
Even design
 
Sijaona point yoyote uliyoongea zaidi ya personal biases zako.Hivi unajua vigezo vinavyotumika kupima ubora wa chuo.Kwa taarifa yako UDSM ndio chuo kinachoongoza kwa ubora East and Central Africa.Kwa Africa kinashika nafasi ya 13 kikizidiwa na vyuo vya South Africa pamoja na cha Misri.Just google it for your reference.
Anyway siku nyingine jipange unavyoanzisha thread manake inaonekana UDSM huijui kabisa kama sisi wahitimu tunavyoijua na tunavyokua proud kusoma kwenye chuo kinachotambulika international
 
Chemistry department,zoology department,botany department and physics department,Nkrumah hall Bila kusahau Mabibo hostel.
Those areas have free wifi
 
huyu jamaa anaonekana ni mpita njia, UDSM si kama ulivoielezea.

Nilitegemea baada ya kumponda huyo Jamaa kuwa amekosea kuielezea UDSM basi Wewe mwana UDSM kindakindaki sasa ungetuelezea sisi tusioijua hiyo UDSM yako ili tufahamu mengi juu yake. Otherwise hata Wewe nimekuona ni mpita njia vile vile wa hapo UDSM.
 
mtoa thread unachekesha kweli eti kwenye ranks za Africa kinajikita mkiani kweli nimeamini wewe hujui.Chuo kinashika nafasi ya 13 katika Africa alafu unasema kipo mkiani hahaaaaa.Ndio maana nimekwambia jipange unapotoa thread humu kama vigezo tu vinavyotumika kupima ubora wa chuo huvijui eti unataka majengo kupakwa rangi,bustani na mazingira kama vigezo vya kupima ubora wa chuo duuh shame on you
 
Mkuu, hata ile Library mpya inayojengwa pale itakuwa kama mapambo tu. Wanafunzi wa UD huwa hawapendi kabisa kusomea library... Wana aleji nayo!
 
Kuna ukweli mkubwa katika mambo uliyoyasema. Chuo hakina duka la vitabu. Lile duka la zamani limejaa vumbi na linauza vitabu vya kindergarten.

Maktaba iliyopo haikidhi mahitaji ya chuo kikuu kinachotoa mpaka PhD nyingi tu. Wachina wanajenga maktaba mpya nadhani wataweka mpaka vitabu vya kuanzia.

Majengo, hasa nyumba za wafanyakazi na barabara za zinatia aibu sana.

Kuna mambo yapo ndani ya uwezo wa UDSM lakini vingi tunavyoona vinakera sana vipo nje ya UDSM. Mfumo wa elimu umeoza kuanzia shule za msingi mpaka vyuo vikuu. Tembelea shule za msingi au sekondari uone jinsi zilivyochoka.

Kwa kiasi kikubwa sana mapato ya UDSM yanatokana na bajeti y serikali. Mnaowalaumu UDSM mmewahi kujiuliza licha ya kulipa mishahara pale chuoni serikali inapeleka nini zaidi?
 
Back
Top Bottom