UDSM kuanza kutoa mitihani ya kimataifa ya Kiswahili ili kuikuza lugha hiyo duniani

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,501
9,280

Na Ezekiel Mtonyole, Dodoma.

Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM) kinataraji kuanza kutoa Mitihani ya Kimataifa ya Ujuzi wa Lugha ya Kiswahili kwa lengo la kuhakikisha lugha ya kiswahili inakuwa zaidi

Hayo yamebainishwa jijini Dodoma na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk.Leonard Akwilapo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mitihani hiyo ambayo inatarajia kuanza kufanyika kuanzia mwaka 2020.

Amesema hiyo inalenga juhudi zinazofanywa katika kuikuza na kuieneza Lugha ya Kiswahili ulimwenguni kote kwa kuhakikisha kuwa ni miongoni mwa lugha 10 zenye wazungumzaji wengi duniani.

“Mtakumbuka kwamba Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alishafanya jitihada kubwa sana na za kuiendeleza na kuieneza Lugha ya Kiswahili pamoja na kusimamia ubora wake ndani na nje ya nchi halikadhalika na waliofuata" amesema Dkt Akwilapo.

Amesema mitihani hiyo itakuwa ikifanyika mara sita kwa mwaka ikiendana na kipindi cha masomo ya Kiswahili kwa kila ngazi na itafanyika kwa njia za kielektroniki katika vyuo na vituo mbalimbali vya Kiswahili duniani ambavyo tayari kuna makubaliano maalumu.

“CKD(UDSM), kinakuwa ni Chuo Kikuu cha kwanza duniani kutunga mitihani hii na kusimamia utahini na usahihishaji wake na kutoa Cheti cha Kimataifa kinachoonesha kiwango cha ujuzi wa mtahiniwa,”amesema.

Amebainisha kuwa Chuo hicho kimechukua na jukumu la kuanzisha mitihani ya Kimataifa ya Ujuzi wa Lugha ya Kiswahili sanifu na ili lugha ya kimataifa ipate nguvu zaidi hutungiwa mitihani ili wanaojifunza lugha hizo waweze kutathminiwa na kupata vyeti.

Amesema tayari kuna makubaliano baina ya walimu wa Kiswahili wa Chuo kikuu Dar es saalam na walimu wanaofundisha Kiswahili katika vyuo vya nje kuhusiana na mitihani hiyo ambayo itaanza kutolewa mwakani.

“Chuo kikuu Cha Dar es saalam kimejiandaa kuhakikisha kuwa mifumo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano iko madhubuti kuwezesha mitihani hii kufanyika kwa ufanisi na kwa viwango vya kimataifa kwani kuna wahitaji ambao watafanyia mitihani hii wakiwa katika nchi zao, sio lzima wasafiri na kuja kufanyia mitihani yao hao Tanzania,”alisema.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Taasisi ya Taaluma za Kiswahili, Prof.Aldin Kai Mutembei, amesema mitihani hiyo itakuwa ikiitwa kwa jina la MKUKi.

“Kuna wanafunzi wengi wanasoma Kiswahili huko nje na walitamani kuja kwenye nchi zinazozungumza Kiswahili lakini wangependa wawe na utambulisho kuwa wanajua Kiswahili hawa ndio tunaowalenga,”amesema.

Amebainisha kuwa Chuo kikuu Cha Dar es saalam, kitahakikisha kinakuwa wawakilishi wazuri wa serikali katika kukuza na kuendeleza lugha ya kiswahili.
 

Na Ezekiel Mtonyole, Dodoma.

Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM) kinataraji kuanza kutoa Mitihani ya Kimataifa ya Ujuzi wa Lugha ya Kiswahili kwa lengo la kuhakikisha lugha ya kiswahili inakuwa zaidi

Hayo yamebainishwa jijini Dodoma na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk.Leonard Akwilapo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mitihani hiyo ambayo inatarajia kuanza kufanyika kuanzia mwaka 2020.

Amesema hiyo inalenga juhudi zinazofanywa katika kuikuza na kuieneza Lugha ya Kiswahili ulimwenguni kote kwa kuhakikisha kuwa ni miongoni mwa lugha 10 zenye wazungumzaji wengi duniani.

“Mtakumbuka kwamba Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alishafanya jitihada kubwa sana na za kuiendeleza na kuieneza Lugha ya Kiswahili pamoja na kusimamia ubora wake ndani na nje ya nchi halikadhalika na waliofuata" amesema Dkt Akwilapo.

Amesema mitihani hiyo itakuwa ikifanyika mara sita kwa mwaka ikiendana na kipindi cha masomo ya Kiswahili kwa kila ngazi na itafanyika kwa njia za kielektroniki katika vyuo na vituo mbalimbali vya Kiswahili duniani ambavyo tayari kuna makubaliano maalumu.

“CKD(UDSM), kinakuwa ni Chuo Kikuu cha kwanza duniani kutunga mitihani hii na kusimamia utahini na usahihishaji wake na kutoa Cheti cha Kimataifa kinachoonesha kiwango cha ujuzi wa mtahiniwa,”amesema.

Amebainisha kuwa Chuo hicho kimechukua na jukumu la kuanzisha mitihani ya Kimataifa ya Ujuzi wa Lugha ya Kiswahili sanifu na ili lugha ya kimataifa ipate nguvu zaidi hutungiwa mitihani ili wanaojifunza lugha hizo waweze kutathminiwa na kupata vyeti.

Amesema tayari kuna makubaliano baina ya walimu wa Kiswahili wa Chuo kikuu Dar es saalam na walimu wanaofundisha Kiswahili katika vyuo vya nje kuhusiana na mitihani hiyo ambayo itaanza kutolewa mwakani.

“Chuo kikuu Cha Dar es saalam kimejiandaa kuhakikisha kuwa mifumo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano iko madhubuti kuwezesha mitihani hii kufanyika kwa ufanisi na kwa viwango vya kimataifa kwani kuna wahitaji ambao watafanyia mitihani hii wakiwa katika nchi zao, sio lzima wasafiri na kuja kufanyia mitihani yao hao Tanzania,”alisema.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Taasisi ya Taaluma za Kiswahili, Prof.Aldin Kai Mutembei, amesema mitihani hiyo itakuwa ikiitwa kwa jina la MKUKi.

“Kuna wanafunzi wengi wanasoma Kiswahili huko nje na walitamani kuja kwenye nchi zinazozungumza Kiswahili lakini wangependa wawe na utambulisho kuwa wanajua Kiswahili hawa ndio tunaowalenga,”amesema.

Amebainisha kuwa Chuo kikuu Cha Dar es saalam, kitahakikisha kinakuwa wawakilishi wazuri wa serikali katika kukuza na kuendeleza lugha ya kiswahili.
Hivi jamani naomba mnusaidie labda mimi sikuwepo enzi za Nyerere. Mambo yote wakati ule aliyafanikisha Nyerere Kwa maana kila jumbo jema naona anatajwa yeye peke yake. Sijui kuleta uhuru Nyerere., kukuza kiswahili Nyerere., kuleta amani Nyerere, kupambana na umasikini Nyerere sasa nashindwa kuelewa najua alifanya juhudi ila ni yeye tuu...
 
Kweli ni jambo njema sana. Tumeachia kuendeleza Kiswahili kiasi kwamba majirani zetu wameingia kwa kasi kubwa lakini kwa njia ambayo inaharibu Kiswahili. Utasikia wakisema fulani amenona badala ya kunenepa! Pia Nyerere alianzisha baraza la Kiswahili kwa nia hiyo ya kukuza Kiswahili. Pia tulisikia kwenye vipindi vya radio mjadala iliyojadili matumizi bora ya Kiswahili. Hayo yote yanahitaji kurejewa kwa kasi na weledi zaidi. Microsoft wamesajili Kiswahili kama lugha ya Kenya. Tuache kuiala kwa sababu kama ambavyo tumealikwa kufundisha Kiswahili Afrika Kusini, ni fursa. Wizara ya utamaduni mpoo??

Niongeze tu kwamba ni kweli Nyerere amefanya mengi sana na ni lazima na sahihi kuzienzi juhudi zake katika mambo mengi mema. Ni kweli siyo yeye tu katika mambo yote , ila waTZ tuna tabia mbaya ya kuvipenda kuwaenzi waliolifanyia Taifa mambo mazuri. Nani alitunga jina Tanzania? Wimbo Tanzania Tanzania....? Bendera yetu?? Viongozi wepi wa jeshi letu walishiriki mstari wa mbele kumngoa idd amin? Kuna mTZ aliyekuwa Rais wa muda huko Seychelles? History is important. It inspires.
 
Back
Top Bottom