Lakini sheria hiyo ilitambua shida ya dini inaweza kuingia kwenye vyana na ikawekwa clause ya kuzuia chama cha kidini kisiwe cha kisiasa.unajua unaposema sema chama fulani nichakidini wakati kimeanzishwa kwa mujibu wa sheria za nchi na wala si za dini fulani huu ni upotofu wa hoja. Hata mimi nilmishangaa wakati ule wakisema CUF ni cha kidini wakati kimeanzishwa kisheria . kama chama kuwa cha kidini tunaangalia dini za viongozi wake basi ccm inaongoza kuegemea dini fulani. lakini turudi palepale vyama vya siasa vimeanzishwa kwa mujibu wa sheria
Duu Hii Kali, Nilikua sijagundua hili!!
Hivi kumbe ndio maana hata rangi za hiki chama ni zilezile kama za Hezbolah?
Na ajenda zake ni za ajabuajabu kama kujiunga na OIC, Kuvunja Uhusiano na Israeli au kutaka kuanzisha Mahakama ya Kadhi.... Siku moja utasikia wakipendekeza kuanzishwa Sharia ili kupambana na ufisadi.
Pole sana kwa fikra potofu ulizo nazo.
Ukweli, mara zote huwa unauma.
Ni lini mtaleta Uhuru wa Kweli Zenji, angalau Mkristo awe Rais?
Mada kama hii iliwahi kuletwa jamvini lakini inaelekea wengine wameileta tena pengine kwa kuwa hawakuisoma ile iliyopita.
Kwa maoni yangu hakuna kitu kibaya kama uvivu wa kufikiri na ndiyo maana kuna baadhi ya mada ziletwazo hazina kichwa wala miguu na nyingine wala hazitufanyi wengine tukakuna bongo wala kufanya tafakuri zenye mantiki.
Kwanza ieleweke mimi siyo mwana ccm bali ni mchambuzi tu wa mambo na ninapenda mantiki itawale kwenye nyanja nyingi iwezekanavyo.
Kama observer uchaguzi wa viongozi ndani ya ccm ni wazi kuliko vyama vyote vya siasa na mara nyingi tunaonyeshwa kwenye luninga au radio [hiyo ndiyo tradition yao] kuhusu uwiano wa dini [i stand corrected] sijawahi kusikia kuwa kuna makubaliano yoyote yale ya namna hiyo.
Suala hili aliwahi kuulizwa hayati baba wa taifa kutokana na wingi wa wajumbe/cabinet/mabalozi kutozingatia dini naye jibu lake lilikuwa kwamba yeye binafsi "hajawahi kufikiria hivyo na kuna nyadhfa nyingine huteua bila kujua ni dini gani wala madhehebu gani na kwamba chama cha ccm siyo cha dini ila viongozi ndiyo wana dini". Hivi leo kipi kimebadilika???? kuna wakati nchi hii viongozi ambao ni wakristo walikuwa zaidi ya asilimia 70 lakini hakuna mtu aliyewaza kuwa chaguzi zao zimetokana na dini hivi leo tunaona ajabu gani????? Chama hiki kingekuwa cha kidini au kikabila sidhani kama kingekuwa na wanachama mamilioni na hata kwenye maeneo ambayo yamejaa watu wa dini moja wasingewachagua viongozi tuliyokuwa nao leo. Wajumbe wote wa NEC wamefika hapo kutokana na vikao vya chini.
Kama suala la udini chama kama Chadema na CUF mtasemaje kuhusu safu zao za viongozi???? Binafsi sidhani kama dini inatumika kuchagua ila kwa miaka ya hivi karibuni ukabila umejiingiza kwenye chaguzi zetu kiasi kuwa hivi sasa ni vigumu mmakonde kuchaguliwa uchagani au upareni.
Nadhani ni ni uwezo wa kufahamu mambo hapa
Je ni nani anaemchagua rais wa zanzibar?
Je kwa akili yako unaangalia dini au uwezo wa mtu?
Je lini amejitokeza mkristo kugombea urais zanzibar akakataliwa kwa dini yake? Kama yupo hebu tupe jina lake.
FYI. Kwa mtu mwenye upeo na akili timamu anaangalia uwezo wa mtu na siyo dini au kabila la mgombeaji.
Mwafrika
Kwa vile serikali ni ya ccm/tanu nimejumuisha viongozi wote kati ya miaka ya 1965-1980
Alikuwa hajazaliwa how can you ask if he/she remember?![]()
Do you remember this?
Picha hizi za Stempu, kutoka kushoto kwenda kulia,
Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph, Kanisa Kuu la Kristo,
Msikiti wa Malindi, Msikiti wa Hujjatul Islam,
Hekalu la Kihindi.
Uwiano unakujaje kama wakristo hawagombei?