Udhaifu wa Tulia Ackson katika suala la kuchana hotuba ya upinzani - Two Wrongs Don't Make it Right!

Ni challenge kubwa sana, na sidhani kama kubadili katiba kutaleta suluhisho. Mara kadhaa tumeona katiba ikivunjwa kwa makusudi na bila aibu. Kitu gani kitazuia hilo kutokea hata ikibadilishwa? Sijui ni jinsi gani ya kumfanya Spika asiwe kibaraka wa chama au raisi

Uko sahihi kabisa ingawa unaonekana kukata tamaa. Haya mambo siyo magumu kiasi hicho. Huko nyuma Waziri Mkuu na mawaziri waliweza kuwajibishwa na Bunge kutokana tu na utashi wa kisiasa na kikatiba. Utashi huo umepotelea wapi? Kimfumo utashi huo upo pale pale; tatizo ni taasisi za kusimamia utashi huo wa kisiasa na kikatiba. Demokrasia ya kweli ni harakati za muda mrefu. Matatizo haya hayawezi kumalizwa siku moja lakini yanaweza kupunguzwa taratibu. Hata vyama vyetu vya siasa vinapaswa kujifunza na kuboresha mifumo yao. Haikubaliki kiongozi wa chama cha siasa kuwa ndiyo chama. Rasimu ya Warioba ilikuwa iwe mwanzo wa safari hii ya demokrasia ingawa maboresho yanayohitajika ni mengi. Rasimu hiyo kwa mfano ilitenganisha serikali na bunge. Hatua hii ingepunguza uwezekano wa kuwa na kiongozi wa bunge anayepokea maelekezo kutoka nje ya Bunge. Kwa kiasi ilipunguza pia madaraka ya mkuu wa serikali. Lakini bado kuna mambo ya kutazama. Ni pamoja na raia kuwekekewa utaratibu wa kikatiba wa kuchukua hatua pale wanapoonekana katiba inavunjwa. Kadhalika kuwa na mgombea huru kutawaondoleaa wabunge adha ya kuwa watumwa wa vyama vya siasa na kushindwa kutekeleza wajibu wao wa kusimamia serikali.
 
Hasemi mbona Mwiguru nae alichana tena akiwa naibu waziri wa fedha!!
Nimeushangaa sana uamuzi wa Dr, Tulia Ackson kuhusu Mbunge wa CCM kuchana hotuba ya upinzani. Tulia, ambaye ni mwanasheria wa kiwango cha PhD, bila aibu ametetea uamuzi wake kwa kutoa kauli kwamba "Vuma hawezi kupelekwa kwenye Kamati ya Nidhamu ya Bunge kwa kuwa kipindi cha nyuma mbunge wa Bunda (Chadema) Ester Bulaya aliwahi kurusha vitabu bungeni na kuvichana lakini hakupelekwa katika kamati hiyo"

Hivi kweli, Dr wa sheria, anawezaje kutoa kauli kama hii? Kama uongozi wa Bunge la Tanzania umewahi kutuhumiwa kuwa dhaifu, basi kwa kauli hii ya Tulia nasema Bunge linaongozwa na maspika ambao si tu ni dhaifu, bali pia ni wameamua kwa makusudi kujifanya vipofu na mbumbumbu wa uongozi, ili kulinda maslahi ya chama chao CCM.

Kwa kiingereza ninasema kwamba "Tanzania parliament leaders are excessively biased against the opposition, to the extent that most of the time they forget to be clever or intentionally choose to be stupid". Hii ya Tulia ni typical case. Za Ndugai zipo nyingi sihitaji hata kuzitaja. Za wenyeviti wengine wa vikao vya Bunge kama kina Chenge, Zungu nk zinatia hata aibu kuzitaja.

Tulia anachodai hapa ni kwamba, Bunge linaendeshwa kwa mantiki ya jino kwa jino. Ni sawa na refa wa mpira wa miguu ambaye anainyima penati ya wazi timu moja, na ili kusawazisha kosa lake, anainyima timu pinzani penati ya wazi pia.

Well Dr. Tulia, kauli ya kwamba "two wrongs don't make it right" sio ya kitoto. Wahenga waliiweka ili kuwaelimisha watu kama wewe ambao mnasahau kutumia akili na usomi wenu kwa manufaa yenu binafsi au ya chama chenu. Kama Ester Bulaya wa Chadema alifanya kosa na hakuchukuliwa hatua, hilo lilikuwa ni kosa na udhaifu wa uongozi wa Bunge. Lakini sasa udhaifu huo unazidi kuzidishwa pale ambapo Vuma wa CCM anafanya kosa kama la Ester na unaamua kwamba basi na yeye asichukuliwe hatua kama ilivyokuwa kwa Ester Bulaya.

Huo ni udhaifu mkubwa wa uongozi wa Bunge.
 
Huyo mdada ni mpumbafu sana.Daima majalalani kuna taka nyingi japo majalala yanatofautiana.
 
Hata angeenda kwenye kamati ya maadili hakuna lolote lingetokea. Naimani hata kapokea cm toka juu ya kumpongeza.
 
Kuna kitu kumbe watu hawakumuelewa CAG Professor Assad, nikuwa alichomaanisha ni kuwa Spika Ndugai na Naibu Spika Tulia ndio DHAIFU na udhaifu wao unadhalisha udhaifu wa Bunge.
 
Uko sahihi kabisa ingawa unaonekana kukata tamaa. Haya mambo siyo magumu kiasi hicho. Huko nyuma Waziri Mkuu na mawaziri waliweza kuwajibishwa na Bunge kutokana tu na utashi wa kisiasa na kikatiba. Utashi huo umepotelea wapi? Kimfumo utashi huo upo pale pale; tatizo ni taasisi za kusimamia utashi huo wa kisiasa na kikatiba. Demokrasia ya kweli ni harakati za muda mrefu. Matatizo haya hayawezi kumalizwa siku moja lakini yanaweza kupunguzwa taratibu. Hata vyama vyetu vya siasa vinapaswa kujifunza na kuboresha mifumo yao. Haikubaliki kiongozi wa chama cha siasa kuwa ndiyo chama. Rasimu ya Warioba ilikuwa iwe mwanzo wa safari hii ya demokrasia ingawa maboresho yanayohitajika ni mengi. Rasimu hiyo kwa mfano ilitenganisha serikali na bunge. Hatua hii ingepunguza uwezekano wa kuwa na kiongozi wa bunge anayepokea maelekezo kutoka nje ya Bunge. Kwa kiasi ilipunguza pia madaraka ya mkuu wa serikali. Lakini bado kuna mambo ya kutazama. Ni pamoja na raia kuwekekewa utaratibu wa kikatiba wa kuchukua hatua pale wanapoonekana katiba inavunjwa. Kadhalika kuwa na mgombea huru kutawaondoleaa wabunge adha ya kuwa watumwa wa vyama vya siasa na kushindwa kutekeleza wajibu wao wa kusimamia serikali.
Mkuu siku hayo yote yakitokea, basi nitakutafuta tunywe champagne pamoja. Kwangu mimi ninafikiri labda siku moja tunaweza kumpata raisi mzalendo wa kweli akayafanyia kazi mambo yote hayo unayoyasema. Lakini najua wazi kwamba raisi huyo mzalendo wa kweli sio Magufuli, wala sio Kabudi ambao nawaona kama wazalendo uchwara tu. Huenda Bashiru, au Tundu Lissu, sijui lakini. Tunahitaji raisi ambaye atakuwa juu ya chama chake cha siasa na kuwa Mtanzania kwanza, kujua kwamba nchi hii inahitaji mabadiliko ya kikatiba kwa faida ya kudumu ya sasa na baadaye kwa ajili ya vizazi vijavyo. Watu kama kina Lincoln, Washington wa USA, walifanya mambo si kwa ajili ya faida ya vyama vyao enzi zao, bali kwa ajili ya faida ya Wamarekani wote kwa wakati huo na miaka mingi baadaye. Huyo ndio aina ya raisi tunayehitaji.
 
Tatizo ni kwamba wapinzani wa nchi hii hawana mbinu za kisiasa.
Walichobaki nacho ni kumponda Magufuli tu kila siku bila kujua kuwa kuna watu wanaponda mema ya nchi hii kwa sababu ya kutaeuliwa kwao na Mh.Rais Magufuli.
Hivi mtu kama Mkuu wa mkoa anayejipatia mahela mpaka anakosa hata wa kumpa na kubaki sasa kugawa magari ,utamwambia nini kuhusu aliyemteua kama sio kutafuta pyuu pyuuu!!

Tulia anasoma upepo na kupima kina cha maji lakini ameona ni kina kifupi na kina mchanga wa kutosha na miamba sio matope hivyo hawezi kuzama .

Wapinzani wana ubinafsi wa kisiasa sana.
Kuna wakati unabaki ukiwashangaa kuwa wanawaza nini kujikwamua na hali ngumu ya kisiasa iliyopo unakosa jibu mana wanabaki kulalamika tu kwenye mitandao.

Wapinzani wafahamu wazi kuwa kwa sasa watu wa kuokoa taiga hili ili liwe na umoja ,upendo,haki na mshikamano ni Viongozi wa dini hasa , Dini zenye mizizi ya imani kama RC ,KKKT ,Anglikana kidogo na Waislam wale wasio chini ya tawi la CCM linaloitwa Bakwata.
Kundi la pili ni la wanasheria wakiwemo Majaji wenye hofu ya Mungu na wanaojua madhara makubwa ya Jaji kupindisha sheria kiimani,kijamii na hata kisiasa.

Mfano mambo kama hayo ni vyema ushshidi ukakusanywa wakaonyeshwa Viongozi wa makundi hayo ili waone wazi kuwa nchi inawasimamia kanuni na sheria wasio waadilifu hata kidogo.

Mtu hawezi kuwa muadilifu kama haogopi sheria. Yani Kwa sasa sheria ni pale mtu anapoamua kumfurahisha bosi wake tu hata kama anamfurahisha kwa kuvunja sheria.

Nimeona mtu mmoja akimtisha mtu kuwa nitakupiga gumi pamoja na kuwa Mimi na mwanamke.
Sasa tujiulize hivi atampiga ngumi kwa sheria gani na ni vipi mtu apigwe ngumi au akwidwe shati adharani na yeye akae kimya tu mana anayempiga ameteuliwa na mkuu kabisa. Hiyo ni hatari sana mana watu wengine ukimdhalilisha anaweza akatoa kisu akakuchoma pale pale na ukawa marehemu bila kujali nini kitamkuta alimradi tu adumishe heshima yake kama mtu mzima kwenye nchi ya kistarabu na kujenga ustarabu wa kesho.

Tulitawaliwa na wazungu kwa sababu walikuja na dharau zao wakitegemea bunduki lakini watu walipozizoea bunduki walizitumia hizo hizo kutafuta Uhuru wao.

Nilifikia mahali nikamkubali sana Ndugai pale alipoamua kupambana na wabunge wakorofi bungeni na akafanikiwa kurejesha heshima ya bunge na akisema mbunge Fulani toka nje mtu anasimama na kutoka mwenyewe . Hili lilikua jambo zuri sana lakini naadae nikagundua kuwa wanaosimamiwa ili watii kanuni ni wapinzani tu lakini CCM wao wanafanya wanavyotaka na hata wakitukana kama Kibajaji wanaongezewa na muda.
Hii inaudhi sana na ikiachwa hivyo iko siku italeta balaa zaidi bungeni. Mana Nadhani kuchana Karatasi iliyoandikwa kwa gharama za walipa Kodi ni kuhujumu uchumi wa nchi. Sio kudharau wapinzani Bali ni kudharau pesa zetu zilizowaweka wote pale.

Hakuna mbunge anayelipwa kwa fedha za chama chake sasa kama tukiamua kuwaacha watumia Chama chao cha CCM ambacho ama kwa uhakika ni chama kisicho na huruma na mtanzania yeyeyote zaidi ya madaraka yao. Ndio maana CCM na serikali kama zilivyokua serikali za kina Sadam Hussein wanakua tayari kutumia majeshi kuwavunja vunja na hata kuwaangamiza wananchi wale wasiowachagua na kuwapa madaraka. Wanajua wapo kwa ajili ya maslahi yao.

Viongozi wa dini wa halali waendelee kusimamia umoja na upendo wa nchi yetu na wasimame kidete kuwaelimisha waumini wao wa kweli ili wakatae vitendo vya kujenga dhulma katika taifa letu ambavyo kwa asili ya mwanadamu ndivyo vinavyovunja amani.
Mkuu, umechanganya mengi sana! Nisikiapo mtu anakimbilia kwa viongozi wa dini, simuungi mkono. Viongozi hao ni sehemu ya jamii yetu na hawana jipya zaidi ya mambo yetu ya mtaani tu. Ndo maana unaona na wao wanajikuta wanaendesha mambo yao kiukabila. Dini na madhehebu hayo unayoyataja pia yamejaa migogoro ya kikabila na uongozi wa kiurafiki. Hatatusaidii kabisa!

Kwa upande wa vyama, nakuunga mkono lakini mimi sipendi kabisa wanasiasa wtufanye sisi kama ndo kinga yao. Wanasiasa wetu wanatengebneza maisha yao, siyo ya kwetu. Mikutano yao haitusaidii lolote zaidi ya wao kujiimarisha. Ndo maama unawasikia wanajimilikisha majimbo ya uchaguzi na wanasema majimbo ni yao. Tangu mwaka 1995 vyama hivi vilistahili kuwa vimekomaa badala ya kuendelea kuomba majukwaa ya kujiimalisha.
 
MUSI SHANGAE MAMBA KULA MZOGA WA SWALA.
HILI BUNGE NI MABAVU NA UJUHA MBELE KWA MBELE.HATA UKIWAMBI LEO IJUMAA WAO WATAPINGA.
HERI KUNYAMAZA NA KUNGOJA HATIMA YA O 2020.
TAZAMENI KULE ZENJI WAMO PEKE YAO MA SISIEM NAHIVYO BADO WANAUMANA WENYEWE KWA WENYEWE WAKIILAUMU SERIKALI YA MUUNGNO KUTOITENDEA HAKI ZNZ.WAKIJISAHAU KUWA SERIKALI ZOTE MBILI NI ZA SISISEM.
CHANGU KIMYAAAA "TIME WILL TELL"
 
Bavicha bwana wanajadili kuchanwa hotuba as if kuna mtu kachinjwa , yale ni makaratasi tu jamani, na pia mkuki kwa nguruwe...mara moja wamesahau namna yule dada wa USA alivyokuwa akiendesha kampeni ya kuchoma kadi za cccm na wao walikuwa wanashangilia. Haya sasa kazi kwenu.
 
Bavicha bwana wanajadili kuchanwa hotuba as if kuna mtu kachinjwa , yale ni makaratasi tu jamani, na pia mkuki kwa nguruwe...mara moja wamesahau namna yule dada wa USA alivyokuwa akiendesha kampeni ya kuchoma kadi za cccm na wao walikuwa wanashangilia. Haya sasa kazi kwenu.
Kadi za CCM zilikuwa zinachomwa Bungeni? Na kwani kinachollamikiwa ni upotevu wa karatasi? Hivi nyie watu mna akili lakini, hamuwezi hata kujibu hoja kwa lojiki? You either forget to be clever or intentionally choose to be stupid.
 
Mkuu siku hayo yote yakitokea, basi nitakutafuta tunywe champagne pamoja. Kwangu mimi ninafikiri labda siku moja tunaweza kumpata raisi mzalendo wa kweli akayafanyia kazi mambo yote hayo unayoyasema. Lakini najua wazi kwamba raisi huyo mzalendo wa kweli sio Magufuli, wala sio Kabudi ambao nawaona kama wazalendo uchwara tu. Huenda Bashiru, au Tundu Lissu, sijui lakini. Tunahitaji raisi ambaye atakuwa juu ya chama chake cha siasa na kuwa Mtanzania kwanza, kujua kwamba nchi hii inahitaji mabadiliko ya kikatiba kwa faida ya kudumu ya sasa na baadaye kwa ajili ya vizazi vijavyo. Watu kama kina Lincoln, Washington wa USA, walifanya mambo si kwa ajili ya faida ya vyama vyao enzi zao, bali kwa ajili ya faida ya Wamarekani wote kwa wakati huo na miaka mingi baadaye. Huyo ndio aina ya raisi tunayehitaji.

Nakubaliana nawe 100%. Imani yangu mimi ni kuwa awamu hii imetuongezea kasi ya kufikia huko. Moto uliowashwa na mchakato wa Katiba Mpya kamwe hautaweza kuzimwa kirahisi. Badala yake awamu ya tano imewafanya wale wote waliokwamisha Rasimu ya Warioba wajutie maamuzi yao. Nguvu nyingi inayotumika sasa kupambana na mawazo hayo ya katiba mpya ni fedheha kubwa siyo kwa hao walipoipinga tu bali kwa taifa hili. Watanzania wengi sasa bila kujali vyama wametambua thamani ya uhuru, demokrasia na utawala bora tofauti na huko nyuma ambapo waliamini tu kuwa viongozi wao wanajua mahitaji yao. Wengi wao waliamini kuwa watu wote wanaopata uongozi wa nchi ni aina ya Nyerere; watu wanaothamini uhai, utu, haki na usawa! Kwa maoni yangu sababu mojawapo ya Nyerere kubadilika na kuunga mkono maoni ya wachache waliotaka mfumo wa vyama vingi ni baada ya kutafakari uzoefu wa chama chake mwenyewe na ule wa Ulaya ya Mashariki na Urusi. Alikuwa na imani kubwa sana na watu/wananchì lakini alikuja kubaini kuwa mfumo wa chama kimoja hauamini watu bali watawala! Kuna watu wengi waliomuelewa hata ndani ya ccm kama ulivyowataja baadhi. Mimi naamini kufika kwetu hapa tulipo ni ajali tu. Muda siyo mrefu tutajisahihisha na kujisahihisha kwetu kutakuwa kwepesi zaidi kwa sababu ya uzoefu tulipopata. Kama ni pepo, tumeonja; hatuhitji tena kusimuliwa!
 
Mkuu, umechanganya mengi sana! Nisikiapo mtu anakimbilia kwa viongozi wa dini, simuungi mkono. Viongozi hao ni sehemu ya jamii yetu na hawana jipya zaidi ya mambo yetu ya mtaani tu. Ndo maana unaona na wao wanajikuta wanaendesha mambo yao kiukabila. Dini na madhehebu hayo unayoyataja pia yamejaa migogoro ya kikabila na uongozi wa kiurafiki. Hatatusaidii kabisa!

Kwa upande wa vyama, nakuunga mkono lakini mimi sipendi kabisa wanasiasa wtufanye sisi kama ndo kinga yao. Wanasiasa wetu wanatengebneza maisha yao, siyo ya kwetu. Mikutano yao haitusaidii lolote zaidi ya wao kujiimarisha. Ndo maama unawasikia wanajimilikisha majimbo ya uchaguzi na wanasema majimbo ni yao. Tangu mwaka 1995 vyama hivi vilistahili kuwa vimekomaa badala ya kuendelea kuomba majukwaa ya kujiimalisha.
Viongozi wa dini wana Mchango mkubwa sana wa kuleta Mageuzi na kuibadili jamii.
Tatizo la Afrika ni kuwa na watu wasio na hofu ya Mungu.
Wenzetu wote duniani wanafikia maendeleo makubwa kwa kuhusianisha uongozi na haki na kuwa kuna thawabu katika kutenda Haki .
Waarabu wanaamini kuwa Mungu,wazungu waliamini na kuihisha na utawala na Elimu rejea Dini kubwa kabisa ya Kirumi linavyoshika dola kupitia koti la siasa na kuishi maisha ya kimbingu hapa duniani. Rumi na dini yake ndiyo inayoongoza siasa za dunia nzima kupitia viongozi wa dini.
Huwezi kufanikiwa kisiasa bila kuwa karibu na viongozi wa dini . Kibaya ni kutumia dini kufanya vurugu lakini kukemea na kuwaelimisha waumini wao namna ya kuwatambua viongozi bora wasiovunja sheria na Katiba walizoapa kuzilinda.

Rejea kwa Askofu Daemon Tutu kula S.Afrika , Mch. Dr. Martini Luther wa Kisabato Kule Amerika alivyopigania haki na Uhuru wa watu wote hasa weusi. Aliitikisa Marekani kwa kujiolea kuutafuta ufalme wa Mungu na haki yake hata kufa. Mpaka Leo Dunia nzima inamuenzi na wazungu hawakumwita msaliti mana wanajua kuwa alichokua anapigania ndicho kilichosahihi. Hawakupotosha pamoja na kuwa walimuua walikua ni wazungu. Tofauti na Afrika watawala na mawakala njaa wao waikuchukia wanakuita msaliti na kukuchaifua na na kuzuia hata picha zako kuwekwe kwenye Tsheti za kuvaa na kufuta historia yako ya kweli na yale ya haki uliyoyaamini .

Utawala wa Kisikteta siku zote kazi zake ni kuanza kudharau Viongozi wa dini na dini kwa kuziita ni ukoloni na hazina umuimu wowote . Malengo yao ni kuwafanya watawala na waliiko kwenye dola kuwa watu katii wasiohofia chochote na wasiojali imani juu ya Mungu asiyeonekana kwa macho .Kwao Mungu ni mishahara mikubwa, majumba ya kifahari ,mali , na wale wanaowapa vyeo.
Dini ndiyo pekee inayosema mpende jirani yako kama nafsi yako.
Ukimpenda jirani yako huwezi kumwona amepigwa risasi na majambazi ukaacha kwenda hata kumsalimia na kumpa mkono wa Pole.
Mafano Lisu alipigwa Risasi na Majangili yasiyofahamika lakini Spika na uongozi mzima wa Bunge hawajawahi kwenda kumsaimia mtumishi wa umma na mwaklishi wa wananchi wa jimbo zima.

Bora hata Rais ambaye ni kiongozi wa muhimili Mwingine lakini aliwakilishwa na Makamu wa Rais kumsalimia Lisu kule Nairobi.

Lakini Spika wa Leo baada ya Kukemewa na Askofu wake Pale Moshi wakati wa Msiba wa Mengi amebadilika sana hata bungeni amekua ni mkali lakini anasikiliza hoja kwa umakini na hata kuikumbusha serikali majukumu yake.
Hakuna Mtu angekua na uwezo wa kumwita Kijana Jeuri kabisa mbele ya ummati wa watu na kumkemea na kumpatanisha na kiongozi wa chama cha upinzani mbele ya Umati mkubwa kama sio kiongozi wa dini.

Hata watawala wanajipima ubora na nguvu yao pale wanapoona waakubaliwa na viongozi wa dini.

Matamko ya Mwanaharakati wa Kiislam moja anaposimama na kukemea serikali bila kuhamasisha uvunjifu wa amani anasikilizwa sana.

Matamko ya kisomi ya Askofu Dr.Bagonza yanawaumiza sana kichwa watawala na wanabadilika sana kutokana na matamko yake uanayosimama katika misingi na kanuni za haki.

Kusema kuwa eti hao viongozi wa dini wana migogoro na ufisadi kwenye dini zao sio sababu ya kuwafanya wasikemee uovu wa wazi .
Ni kama mtu aliyepata Ukimwi kwa umalaya kuambiwa kuwa hana haki ya kukemea vitendo vya umalaya vinavyosambaza virus vya ukimwi.

Katiba na sheria zipo zinapaswa zifuatwe kwa haki ndio maana hata wakati wa awamu zilizopita na zilizopo kuna upigaji sana unaofanywa watawala lakini haachi kukemea vitendo hivyo.
Sawa na mtu wa kusimamia sheria anapomkamata mvunja Sheri halafu naye anavunja sheria kwa kula rushwa.
Ndivyo dunia ilivyo hasa nchi maskini ni lazima watokee watu wa kukemea na kukumbusha wajibu wa kufuata sheria kwa wote.

Tuliona kula Sudani Kusini Viongozi wao wajuu na wapinzani wao wakiwa wananyenyekea mbele ya Papa ,kiongozi mkuu wa Kanisa kubwa ulimwenguni na kupewa wosia wa kupatana ,kuwatumikia wananchi kwa wanyenyekevu kwa ajili ya manufaa ya watu wengi na kuacha ubinafsi.

CCM inafanya makosa mengi sana wanapokua madarakani lakini wanajua kujisusha mbele ya viongozi wa dini wa kujiliza mbele yao na kupiga magoti kuombewa.
Hii inawafanya waonekane kuwa wanatii Mamlaka kuu ya Mungu ambayo na kuwa marafiki na wa viongozi hao . Hii inawasaidia kukumbuka angalau kuteda mema wakati mwingine na kuiona nao ni wanadamu.

Unakuta Mtu wa Chama cha Upinzani anapinga mpaka masuala ya dini kwenye dini yake halafua anategemea kupata kura kwenye eneo hilo.
Nakumbuka Waitataraara alipoona ataangukia pua kule Ukonga alijipeleka kanisa la manabii waliotabiriwa nyakati za Mwisho na kuombewa ili ashinde pamoja na ulevi wake wa kutisha.
Lakini ilikua ni janja ya kuwapata wapiga kura kwa kusaidiwa na kiongozi wa kanisa lile aliyeonekaa kutabiri kuwa atashinda kwa upako wa kanisa lake.Akaonenaka naye ni muumini.

Hali kadhalika Kule Zenji uwe CCM au CUF au ACT kama utapuuza viongozi wa dini na utamaduni wa kiislaam na ibada inabidi ushinde kwa kishindo cha Mabomu.
 
Tatizo ni kwamba neno ustaarabu halimo katika vocabulary ya viongozi wa CCM, kuanzia ngazi ya juu kabisa hadi ya chini kabisa!
Ikisemwa kuwa wanapandikiza chuki za kisiasa na za kiudugu, linatokezea neno "uchochezi". Taifa linapelekwa pasiko:
- kwanini tusifikiri kuwa hatua kama hizo ni calculated towards utawala usio wa sheria? Amani inajengwa na kulelewa.
- macho ya serikali yameelekezwa kwa wapinzani wa kisiasa tu?
Kama si kesho lakini ipo siku mambo haya yatatugharimu sisi sote; si wapinzani wala watawala na vizazi vyao.
 
Mimi nimeshangaa sana yani, hii dharau ya Vuma aisee daaah. Upinzani una hali ngumu sana awamu hii kupita wamu zote... This is not right at all.
Jimbo la dr Tulia ni rais Magufuli hivyo lazima alinde jimbo lake ili 2020 asilipoteze
 
It is by the goodness of God that in our country we have those three unspeakably precious things: freedom of speech, freedom of conscience, and the prudence never to practice either of them
 
It is by the goodness of God that in our country we have those three unspeakably precious things: freedom of speech, freedom of conscience, and the prudence never to practice either of them
Hahahah! That is a good one. For a moment I thought you were living in utopia, then you hit me with the last part of your text! Only that it cant be such a precious thing compared to the other two. Thanks for that philosophical piece.
 
Nakubaliana nawe 100%. Imani yangu mimi ni kuwa awamu hii imetuongezea kasi ya kufikia huko. Moto uliowashwa na mchakato wa Katiba Mpya kamwe hautaweza kuzimwa kirahisi. Badala yake awamu ya tano imewafanya wale wote waliokwamisha Rasimu ya Warioba wajutie maamuzi yao. Nguvu nyingi inayotumika sasa kupambana na mawazo hayo ya katiba mpya ni fedheha kubwa siyo kwa hao walipoipinga tu bali kwa taifa hili. Watanzania wengi sasa bila kujali vyama wametambua thamani ya uhuru, demokrasia na utawala bora tofauti na huko nyuma ambapo waliamini tu kuwa viongozi wao wanajua mahitaji yao. Wengi wao waliamini kuwa watu wote wanaopata uongozi wa nchi ni aina ya Nyerere; watu wanaothamini uhai, utu, haki na usawa! Kwa maoni yangu sababu mojawapo ya Nyerere kubadilika na kuunga mkono maoni ya wachache waliotaka mfumo wa vyama vingi ni baada ya kutafakari uzoefu wa chama chake mwenyewe na ule wa Ulaya ya Mashariki na Urusi. Alikuwa na imani kubwa sana na watu/wananchì lakini alikuja kubaini kuwa mfumo wa chama kimoja hauamini watu bali watawala! Kuna watu wengi waliomuelewa hata ndani ya ccm kama ulivyowataja baadhi. Mimi naamini kufika kwetu hapa tulipo ni ajali tu. Muda siyo mrefu tutajisahihisha na kujisahihisha kwetu kutakuwa kwepesi zaidi kwa sababu ya uzoefu tulipopata. Kama ni pepo, tumeonja; hatuhitji tena kusimuliwa!
Well said Mkuu. Kwangu mimi, kosa kubwa alilofanya Nyerere ni kuto-vipromote vyama vya siasa kwa nguvu zake zote. Nyerere alielewa sana umuhimu wa siasa za upinzani imara nchini, lakini bado mwanzoni alichelea CCM kudumazwa na upinzani na hivyo kwa namna fulani alichangia kutoimarisha upinzani. Naelewa kwamba alikuwa akiona upinzani wakati huo ulikuwa haujakomaa vya kutosha kuchukua nchi, na akasahau kwamba hata TANU ilipochukua nchi ilikuwa haijakomaa. Alipaswa kuacha maji yafuate mkondo wake.

Kwa mfano, Nyerere alijua wazi kwamba bila yeye kuingilia kati Mrema angekuwa raisi dhidi ya Mkapa. Lakini akawa anauliza maswali, hivi Mrema akiwa Raisi kwa mfano, atawachagua nani katika chama chake kuunda baraza la mawaziri? Sasa hili lilimtia hofu kwamba Tanzania inaweza kujikuta katika hali ambayo viongozi hawako serious wanachukulia uwaziri kama jambo la mzaha. Hilo lilikuwa kosa kwa Nyerere. Angeacha NCCR wajifunze the hard way. Na pia Nyerere alisahau kwamba kama NCCR na Raisi Mrema wangevurunda, CCM ingeshinda tena uchaguzi uliofuata.

Enzi hizo Nyerere aliona Chadema peke yake ndio kilikuwa angalau na viongozi na sera serious, lakini hakikuwa na nguvu ya wanachama wengi.

Zanzibar hivyo hivyo. Kuna wakati ilibidi aingilie kati kwa namna ambayo ilimuuma sana, lakini akasema hakukuwa na jinsi nyingine ili kuepusho mkanganyiko wa kisiasa kati ya bara na visiwani. Lakini kuingilia kwakwe kuliidhoofisha CUF na upinzani kwa ujumla

So Nyerere, mzalendo wa kweli wa Tanzania, alifanya kosa sana kuibeba CCM dhidi ya NCCR Mageuzi. Angeacha Mkapa apigwe chini na Mrema. Ona hata kwamba huyo Mkapa aliyembeba alikuja kumsaliti vibaya sana, kiasi hata kusemwa alisababisha kifo cha Nyerere!
 
Viongozi wa dini wana Mchango mkubwa sana wa kuleta Mageuzi na kuibadili jamii.
Tatizo la Afrika ni kuwa na watu wasio na hofu ya Mungu.
Wenzetu wote duniani wanafikia maendeleo makubwa kwa kuhusianisha uongozi na haki na kuwa kuna thawabu katika kutenda Haki .
Waarabu wanaamini kuwa Mungu,wazungu waliamini na kuihisha na utawala na Elimu rejea Dini kubwa kabisa ya Kirumi linavyoshika dola kupitia koti la siasa na kuishi maisha ya kimbingu hapa duniani. Rumi na dini yake ndiyo inayoongoza siasa za dunia nzima kupitia viongozi wa dini.
Huwezi kufanikiwa kisiasa bila kuwa karibu na viongozi wa dini . Kibaya ni kutumia dini kufanya vurugu lakini kukemea na kuwaelimisha waumini wao namna ya kuwatambua viongozi bora wasiovunja sheria na Katiba walizoapa kuzilinda.

Rejea kwa Askofu Daemon Tutu kula S.Afrika , Mch. Dr. Martini Luther wa Kisabato Kule Amerika alivyopigania haki na Uhuru wa watu wote hasa weusi. Aliitikisa Marekani kwa kujiolea kuutafuta ufalme wa Mungu na haki yake hata kufa. Mpaka Leo Dunia nzima inamuenzi na wazungu hawakumwita msaliti mana wanajua kuwa alichokua anapigania ndicho kilichosahihi. Hawakupotosha pamoja na kuwa walimuua walikua ni wazungu. Tofauti na Afrika watawala na mawakala njaa wao waikuchukia wanakuita msaliti na kukuchaifua na na kuzuia hata picha zako kuwekwe kwenye Tsheti za kuvaa na kufuta historia yako ya kweli na yale ya haki uliyoyaamini .

Utawala wa Kisikteta siku zote kazi zake ni kuanza kudharau Viongozi wa dini na dini kwa kuziita ni ukoloni na hazina umuimu wowote . Malengo yao ni kuwafanya watawala na waliiko kwenye dola kuwa watu katii wasiohofia chochote na wasiojali imani juu ya Mungu asiyeonekana kwa macho .Kwao Mungu ni mishahara mikubwa, majumba ya kifahari ,mali , na wale wanaowapa vyeo.
Dini ndiyo pekee inayosema mpende jirani yako kama nafsi yako.
Ukimpenda jirani yako huwezi kumwona amepigwa risasi na majambazi ukaacha kwenda hata kumsalimia na kumpa mkono wa Pole.
Mafano Lisu alipigwa Risasi na Majangili yasiyofahamika lakini Spika na uongozi mzima wa Bunge hawajawahi kwenda kumsaimia mtumishi wa umma na mwaklishi wa wananchi wa jimbo zima.

Bora hata Rais ambaye ni kiongozi wa muhimili Mwingine lakini aliwakilishwa na Makamu wa Rais kumsalimia Lisu kule Nairobi.

Lakini Spika wa Leo baada ya Kukemewa na Askofu wake Pale Moshi wakati wa Msiba wa Mengi amebadilika sana hata bungeni amekua ni mkali lakini anasikiliza hoja kwa umakini na hata kuikumbusha serikali majukumu yake.
Hakuna Mtu angekua na uwezo wa kumwita Kijana Jeuri kabisa mbele ya ummati wa watu na kumkemea na kumpatanisha na kiongozi wa chama cha upinzani mbele ya Umati mkubwa kama sio kiongozi wa dini.

Hata watawala wanajipima ubora na nguvu yao pale wanapoona waakubaliwa na viongozi wa dini.

Matamko ya Mwanaharakati wa Kiislam moja anaposimama na kukemea serikali bila kuhamasisha uvunjifu wa amani anasikilizwa sana.

Matamko ya kisomi ya Askofu Dr.Bagonza yanawaumiza sana kichwa watawala na wanabadilika sana kutokana na matamko yake uanayosimama katika misingi na kanuni za haki.

Kusema kuwa eti hao viongozi wa dini wana migogoro na ufisadi kwenye dini zao sio sababu ya kuwafanya wasikemee uovu wa wazi .
Ni kama mtu aliyepata Ukimwi kwa umalaya kuambiwa kuwa hana haki ya kukemea vitendo vya umalaya vinavyosambaza virus vya ukimwi.

Katiba na sheria zipo zinapaswa zifuatwe kwa haki ndio maana hata wakati wa awamu zilizopita na zilizopo kuna upigaji sana unaofanywa watawala lakini haachi kukemea vitendo hivyo.
Sawa na mtu wa kusimamia sheria anapomkamata mvunja Sheri halafu naye anavunja sheria kwa kula rushwa.
Ndivyo dunia ilivyo hasa nchi maskini ni lazima watokee watu wa kukemea na kukumbusha wajibu wa kufuata sheria kwa wote.

Tuliona kula Sudani Kusini Viongozi wao wajuu na wapinzani wao wakiwa wananyenyekea mbele ya Papa ,kiongozi mkuu wa Kanisa kubwa ulimwenguni na kupewa wosia wa kupatana ,kuwatumikia wananchi kwa wanyenyekevu kwa ajili ya manufaa ya watu wengi na kuacha ubinafsi.

CCM inafanya makosa mengi sana wanapokua madarakani lakini wanajua kujisusha mbele ya viongozi wa dini wa kujiliza mbele yao na kupiga magoti kuombewa.
Hii inawafanya waonekane kuwa wanatii Mamlaka kuu ya Mungu ambayo na kuwa marafiki na wa viongozi hao . Hii inawasaidia kukumbuka angalau kuteda mema wakati mwingine na kuiona nao ni wanadamu.

Unakuta Mtu wa Chama cha Upinzani anapinga mpaka masuala ya dini kwenye dini yake halafua anategemea kupata kura kwenye eneo hilo.
Nakumbuka Waitataraara alipoona ataangukia pua kule Ukonga alijipeleka kanisa la manabii waliotabiriwa nyakati za Mwisho na kuombewa ili ashinde pamoja na ulevi wake wa kutisha.
Lakini ilikua ni janja ya kuwapata wapiga kura kwa kusaidiwa na kiongozi wa kanisa lile aliyeonekaa kutabiri kuwa atashinda kwa upako wa kanisa lake.Akaonenaka naye ni muumini.

Hali kadhalika Kule Zenji uwe CCM au CUF au ACT kama utapuuza viongozi wa dini na utamaduni wa kiislaam na ibada inabidi ushinde kwa kishindo cha Mabomu.
Unaowataja kama viongozi wa dini, ni sawa lakini kuhusika kwao ktk mageuzi na siasa, siyo kwa sababu ya dini. Ni wao kama wao kwa tabia zao na ni wachache. Ni sawa na waalimu kama Nyerere au wanasheria kama Mandela. huwezi ukaomba waalimu watusaidie kwa sababu yupo Nyerere mwalimu aliyetusaidia au wanasheria kama Mandela.

Wapo viongozi wengi wa dini ambao ni tatizo kubwa ktk jamii yetu na ukiwapa nafasi kwa ujumla eti wana mchango, wanaishia kulawiti vijana wetu tu! Wengi wanalewa sifa kwa kujidai wana u-Mungu na wanaweza kutufanya kama walituumba. NO! Baadhi wana udhaifu wa kutuumiza tusiwape madaraka ya jumla.
Sikiliza hiyo:

 
This is Tanzania, they don't stop doing something because it is wrong. They keep doing it until its right.
I'm surprised non of them have thought about conducting a psych evaluation before taking an oath to serve us. Insanity is no longer a mental problem to our leaders, rather a personality trait
Hahahah! That is a good one. For a moment I thought you were living in utopia, then you hit me with the last part of your text! Only that it cant be such a precious thing compared to the other two. Thanks for that philosophical piece.
 
Unaowataja kama viongozi wa dini, ni sawa lakini kuhusika kwao ktk mageuzi na siasa, siyo kwa sababu ya dini. Ni wao kama wao kwa tabia zao na ni wachache. Ni sawa na waalimu kama Nyerere au wanasheria kama Mandela. huwezi ukaomba waalimu watusaidie kwa sababu yupo Nyerere mwalimu aliyetusaidia au wanasheria kama Mandela.

Wapo viongozi wengi wa dini ambao ni tatizo kubwa ktk jamii yetu na ukiwapa nafasi kwa ujumla eti wana mchango, wanaishia kulawiti vijana wetu tu! Wengi wanalewa sifa kwa kujidai wana u-Mungu na wanaweza kutufanya kama walituumba. NO! Wana udhaifu wa kutuumiza na hatutaki.
Sikiliza hiyo:

Kuna mzee alinisimulia jinsi Tanganyika ilivyopata Uhuru na kuanisha kuwa Uingereza waliamua kutoa Uhuru mezani baada ya kuona Mtiti uliotokea Kenya.Wazungu waliuawa sana na Mau mau.
Wakaona bora watoe tu bure mana wakiacha Tanganyika nayo ikaanza vita watakosa pa kukimbiia .

Kwatika mazungumzo yake yule Mzee aliweka bayana kuwa kwenye Tawala za kuwatawala watu kuna makundi Matano :-

1.Watawala wanakua ndio kundi lililojiweka Juu kabisa Wakifuatiwa na
2. Wakuu wa majeshi
3.Viongozi wa dini wapo katikakati.
4. Wafanyakazi wanafuata .
5. Wakulima ndilo kundi la mwisho kabisa.

Viongozi wa dini wanawekwa katikati ili kusaidia haya makundi mawawili ya chini yaani ya 4 na 5 yapate faraja kwa kupewa maneno mazuri na ya kuwafanya wawe watiifu na kujipa moyo wa imani .
Majeshi kazi yake ni kuyazuia makundi kuanzia la tatu ,la NNE na la Tano wasilifikie kundi la Kwanza.

Kwa ushawishi wa makundi ya viongozi wa dini ni muhimu sana.
Na pia kuhusu kufanya maovu kwao sio sababu ya kuwatenga na harakati za kuleta haki kwenye jamii.
Ikumbukwe kuwa wengi wa watawala na viongozi wa dini ni wamoja na ndio maana hata Chama tawala kinajitahidi kwa namna yoyote kuwa karibu nao.
Migogoro kwenye makundi ya dini Mara nyingi kuna wanasiasa nyuma mana kama nchi iko stable kwenye Katiba na sheria haliwezekani migogoro ikaibuka kwenye miangoni mwa wananchi.

Mfano Migogoro mingi ya KKKT na Bakwata ni kwa sababu ya Ujanja walioutumia mwanzoni wanasiasa na Watawala wa kuwezesha dini hizo kujitoa kwenye Jumuiya pana za kimataifa na kuanzisha taasisi za ndani ambazo zinakua na migogoro ya madaraka madarakani.
Yote ni kuyafanya makundi ya dini yagawanyike ili wasije wakamulika wanasiasa na kuziona dhambi zao.

Dini ni pamoja na dini za asili ndio maana mpaka leo CCM na serikali yake wanaabudu Mwenge kwa maelekezo ya wazee wa mila na mizimu yao.
Na mwenye umekua na mvuto mkubwa sana kwenye jamii kuliko kitu chochote.
Hebu fikiri kama Mwalimu angedharau Maelekezo ya viongozi wa dini za jadi kule Bagamoyo leo hii wengi wangekua wanakosa dili za kukimbiza mwengi na kupiga hela.
 
Back
Top Bottom