Omusolopogasi
JF-Expert Member
- Aug 31, 2017
- 7,101
- 18,083
- Itategemea doctor umeajiriwa wapi, ukiajiriwa doctor halmashauri mshahara ni 1,400,000/- Wakati Legal Officer wa TRA Ni 3,200,000/-, Customs Officer Ni 2.3M, Customs assistant Ni 1.8 M
-Mtu mwenye diploma anayefanya Kazi TRA, Ewura,latra anamzidi daktari mbali Sana, mwenye Degree mbali zaidi
Logic ni kwamba vitengo vingi serikalini vile vyenye Hela havihitaji madaktari wanahitaji CPA, ADVOCATES,ENGINEERS, FINANCE MANAGERSUsisahau kuwa kuna madaktari pia wako WHO, UNICEF, UNFPA, nk. Linganisha machungwa kwa mchungwa (daktari na lawyer wa halmashauri). Siyo machungwa na mapera (daktari wa halmashauri na lawyer wa TRA).
Hapa ndo umedanganya laba kama unamanisha kwa scale za halmshauri madakatari ndo wana mishahara mikubwaNaambiwa Udaktari unalipa mara tatu zaidi ikiwa utataka kulinganisha na fani nyingine yoyote, kwa mfano.
1. Heshima kubwa kijamii.
2. Uhakika wa ajira (ikiwa utalinganisha na fani nyingine yoyote)
3. Mshahara mkubwa zaidi ya fani zote (katika ajira za serikali)
Logic ni kwamba vitengo vingi serikalini vile vyenye Hela havihitaji madaktari wanahitaji CPA, ADVOCATES,ENGINEERS, FINANCE MANAGERS
Kwa hiyo hao wa vitengo unavyosema serikalini wanazidi mshahara madaktari wa WHO ama UNICEF? Think again. Ama unasema hata huku WHO wanataka zaidi CPA.
Udaktari, kama akiwa daktari bingwa, ni kazi nzuri. ila ni kazi yenye mateso, stress. though generally, ukiwa daktari unaheshimika na kila mtu kwa hofu ya kuugua ukakutana nao wakahitaji msaada wako (heshima ya woga). nikiwaza ningekuwa doctor, huwa nawaza ningefanyeje kwenye mambo ya night. hilo huwa nalizingatia hata kuwashauri watoto wangu vitu vya kusomea.Habarini wanajukwaa,
Naomba kujua,udaktari unalipa?
Nimekuwa nikipashwa habari kuwa "mtoto mpeleke udaktari" ni taaluma isiyokuwa na longolongo na hakuna daktari mwenye bachelor mtaani anapambania ajira zaidi ya mwaka mmoja,hivyo imepelekea mwanangu kukulia maisha fulani yenye mtazamo wa kuwa daktari mahili hapo mbeleni,wahusika nipeni uzoefu juu ya hili mzazi ninapoteza muda juu ya hili au kuna ukweli ndani yake?
- usichoelewa WHO, UNICEF huko pia Kuna maCPA🤣🤣
- Taaluma ya Udaktari iko very confined Sio Kama Uhasibu ambapo wanaingia kila Kona/kila taasisi Hadi Mahakamani wahasibu wapo,
Hivi ni kweli ukisomea udaktari hukosi kazi hukai mtaani sana kama hawa graduates wengine ?Kama Unasoma udaktari ilii uje kuwa Tajiri bhasi Umekosea njiaa..
NdioHivi ni kweli ukisomea udaktari hukosi kazi hukai mtaani sana kama hawa graduates wengine ?
Ni ngumu kukosa kazi kabisaNdio
Basi hio ndio kazi ya kusomea kama huna mtotoNdio
Mtu mwenye CPA anayefanya Kazi EWURA nijikutajia salary yake unaweza kuliaKama unasomea udaktari ili upate mshahara mkubwa unakosea njia
Cheki hapa uangalie kama inalingana na struggle zake
Level ya degree MD
Daktari chini ya TAMISEMI mshahara 1.48M
Baada ya makato anapokea 870k
Wizara ya afya 1.8M
Baasa ya makato anapokea 1.05M
Daktari kwenye hospitali ya taifa na
taasisi mf MOI,JKCI -mshahara kuanzia 2M
Bila kusahau hela za bima,night shifts,procedure mbalimbali -hii ni kwa wote from tamisemi-hosp ya taifa na taasisi za afya
Daktari kwenye mashirika mf MDH,NIMR,ICAP mara nyingi anaanzia 2.5M
sku iz kuna mabadiliko kidogo kutegemea na cheo na experience
Bila kusahau hela za vikao,semina,per diem
🤦🤦🤦🤦Mtu mwenye CPA anayefanya Kazi EWURA nijikutajia salary yake unaweza kulia
- TRA 75% ni Watu wa Accounting, finance,Customs,Law, EconomicsKama ni issue ya kuwepo CPA 2-3, kwa hiyo unafikiri Benki Kuu, TRA, TPA... hakuna madaktari? Fikiri tena.
- TRA 75% ni Watu wa Accounting, finance,Customs,Law, Economics
BoT wengi ni Watu wa Economics, Accounting, finance,law,hr,law,banking, business administration
TPA ni hivyo hivyo
- Udaktari uko very confined compared to Accounting kila department CPA yupo Hadi Mahakamani, Daktari anaingia mahakamani?
Daktari anaingia LATRA? EWURA? TANROADS? eGA? TCRA?
-Ukifanya Research utagundua Madaktari wengi wanaishia kuajiriwa TAMISEMI
-Hao madaktari wanaosoma CPA ni kwamba wamegundua fursa zilizoko kwenye CPA (T), wamegundua taaluma ya Udaktari iko confined kwenye fursa za kujiajiri na kuajiriwaNani kakwambia madaktari hawawezi kuwa CPA, MBA? Mbona nawajua madaktari waliosoma ESAMI na kutoka with flying colors? Lakini sijawahi kusikia mhasibu ambaye amekuwa daktari bingwa wa kitu fulani.
Ukitaka kuchangia vizuri, soma mtiririko wa hoja. Kuna mchangiaji amesema kuwa CPA wako UNICEF na WHO pia. WHO na UNICEF siyo za madaktari tu, hapa CPA wapo. Mi nikamjibu kuwa ndio wapo lakini ni wachache kama madaktari walivyo wachache BOT, TPA... Sasa sijui hoja yako inapinga nini katika hili?
Unataka kudanganya watu kuwa maisha ni rahisi ukiwa na CPA huku vijana wetu wenye CPA, MBA wakisota miaka na miaka bila kazi. Kukiwa na kikazi sehemu fulani, waombaji ni 10,000 na mtihani wanafanyia kwenye stadium kama vile kuna mechi ya mpira!