Udahili wa pamoja sekondari ni ujuha?

tpaul

JF-Expert Member
Feb 3, 2008
21,933
18,403
Udahili wa pamoja kwa wanafunzi wanaochaguliwa kujiunga sekondari za umma na za binafsi, nauona kama ni mpango uliofeli hata kabla ya kuanza. Mpango huu, ambao haujawahi kujaribiwa na nchi yoyote hapa duniani, utekelezaji wake utakuwa mgumu sana kwa sababu kadhaa:

Kwanza, shule za binafsi zina utaratibu wake murua wa kuchagua wanafunzi wanaojiunga na shule zao. Pamoja na kufaulu mtihani wa taifa (NECTA) wanafunzi wanaoomba kujiunga na shule hizo hufanyishwa mtihani wa mchujo unaotungwa ma shule husika. Sio rahisi serikali iwachagulie wanafunzi vilaza wasiojua kusoma wala kuandika. Hawa wanafaa waende shule za kata.

Pili, haiwezekani kumpangia mwanafunzi asome shule ya kata wakati mzaziwe hana uwezo wa kumsomesha huko--kwa kuwa serikali haichangii chochote. Kuna kigogo mmoja kutoka wizara ya elimu amehojiwa akasema serikali haitachangia hata senti.

Tatu, elimu inayotolewa ktk shule za serikali (kata) ni duni mno. Huwezi kumlazimisha mzazi mwenye uwezo kumsomesha mwanae kwenye shule zisizokuwa na tija (huu ni udikteta wa kielimu).

Mimi naona kama huu mpango umefeli hata kabla ya kuanza. Wadau wengine mnasemaje kuhusu mpango huu?
Nawasilisha.
 
Udahili wa pamoja kwa wanafunzi wanaochaguliwa kujiunga sekondari za umma na za binafsi, nauona kama ni mpango uliofeli hata kabla ya kuanza. Mpango huu, ambao haujawahi kujaribiwa na nchi yoyote hapa duniani, utekelezaji wake utakuwa mgumu sana kwa sababu kadhaa:

Kwanza, shule za binafsi zina utaratibu wake murua wa kuchagua wanafunzi wanaojiunga na shule zao. Pamoja na kufaulu mtihani wa taifa (NECTA) wanafunzi wanaoomba kujiunga na shule hizo hufanyishwa mtihani wa mchujo unaotungwa ma shule husika. Sio rahisi serikali iwachagulie wanafunzi vilaza wasiojua kusoma wala kuandika. Hawa wanafaa waende shule za kata.

Pili, haiwezekani kumpangia mwanafunzi asome shule ya kata wakati mzaziwe hana uwezo wa kumsomesha huko--kwa kuwa serikali haichangii chochote. Kuna kigogo mmoja kutoka wizara ya elimu amehojiwa akasema serikali haitachangia hata senti.

Tatu, elimu inayotolewa ktk shule za serikali (kata) ni duni mno. Huwezi kumlazimisha mzazi mwenye uwezo kumsomesha mwanae kwenye shule zisizokuwa na tija (huu ni udikteta wa kielimu).

Mimi naona kama huu mpango umefeli hata kabla ya kuanza. Wadau wengine mnasemaje kuhusu mpango huu?
Nawasilisha.

So una ona halali, watoto wanavyodhalilishwa pale, Marian, Feza, msimbazi centre, kisa kutafuta nafasi ya mwanao akasome shule iliyopachikwa jina kuwa ni shule nzuri?

wachaguliwe watoto WAWAFUNDISHE wafaulu ndio tujuwe kweli shule ipi ni nzuri? the best school ni ili inayochukuwa wanafunzi ikawafunza na wakafaulu, sio inayojichaguliwa cream then inajitapa inafaulisha
 
Ni Wazo Zuri Lakini Bado Linamapungufu Mengi, Kabla Ya Kufanya Utekelezaji Lazima Uhakikishe Huduma Na Kiwango Cha Elimu Zinatolewa Kwa Usawa Tanzania Nzima,
 
So una ona halali, watoto wanavyodhalilishwa pale, Marian, Feza, msimbazi centre, kisa kutafuta nafasi ya mwanao akasome shule iliyopachikwa jina kuwa ni shule nzuri?

wachaguliwe watoto WAWAFUNDISHE wafaulu ndio tujuwe kweli shule ipi ni nzuri? the best school ni ili inayochukuwa wanafunzi ikawafunza na wakafaulu, sio inayojichaguliwa cream then inajitapa inafaulisha

wanadhalilishwaje? kuweka mchujo ni udhalilishaji? basi hata necta wafute tuwe tunaenda tu
pia mie mwanangu akichaguliwa feza ada milioni tano wakati sina uwezo nafanyaje? serikali itanilipia?
 
So una ona halali, watoto wanavyodhalilishwa pale, Marian, Feza, msimbazi centre, kisa kutafuta nafasi ya mwanao akasome shule iliyopachikwa jina kuwa ni shule nzuri?

wachaguliwe watoto WAWAFUNDISHE wafaulu ndio tujuwe kweli shule ipi ni nzuri? the best school ni ili inayochukuwa wanafunzi ikawafunza na wakafaulu, sio inayojichaguliwa cream then inajitapa inafaulisha

utawalipia karo wewe? na unaposema wanafunzi wanadhalilishwa una maana gani? kwani kufanyishwa mtihani ni kudhalilisha? unataka seminari na academies wapelekewa wanafunzi wasiojua kusoma wala kuandika? think BIG man.
 
Ni Wazo Zuri Lakini Bado Linamapungufu Mengi, Kabla Ya Kufanya Utekelezaji Lazima Uhakikishe Huduma Na Kiwango Cha Elimu Zinatolewa Kwa Usawa Tanzania Nzima,

POINT! Na hili la kutoa elimu sawa (na KARO na vipato sawa miongni mwa raia) miongoni mwa public & private schools, halitekelezeki hata kidogo. Kwa hiyo na mpango wenyewe hautekelezeki sawia.
 
Tatizo kubwa ni kuwa viongozi wakuu Wizara ya Elimu sana Shule zao binafsi kwa hiyo wamekuta na huo Mpango kwa maslahi Yao binafsi lakini ukweli ni kuwa hakuna mazingira ya kufanikisha Mpango huo maana ubora wa Shule umetofautiana sana. Kama Wizara Ina hela za kupeleka Provate schools mbona imeacha Shule zake katika Hali mbaya sana?nenda Tabora Boys, Milambo, Weruweru, Masasi, Pugu, Kazima n.k
Kwa nini wasiziboreshe Shule zao kwanza? Shule za Kata ndiyo usiseme zina Hali mbaya sana. Ubinafsi wa viongozi wa Elimu kutanguliza maslahi yao kumshauri elimu yetu
 
kama wanategemea kufanya ufisadi kwa mbinu hii, watashindwa mchana kweupe--huku ni sawa na kuchoma mahindi kwa kutumia mwanga wa tochi. mtu ukitaka kufanya uharibifu ktk elimu bila kuhitaji kutumia pesa, hilo linawezekana, lakini kama unahitaji fedha kutoka wizara ya elimu, lazima uchemshe. tatizo ni kwamba pale wizarani pana mchwa wengi sana na hawashibi kamwe.
 
wanadhalilishwaje? kuweka mchujo ni udhalilishaji? basi hata necta wafute tuwe tunaenda tu
pia mie mwanangu akichaguliwa feza ada milioni tano wakati sina uwezo nafanyaje? serikali itanilipia?

you probably missed the point, hata ada ziko kwenye mchakato wa kuwa regulated
 
you probably missed the point, hata ada ziko kwenye mchakato wa kuwa regulated

Wewe lazima utakuwa na matatizo. Karo zitafidiwa na nani wakati serikali imesema haihusiki na kuchangia chochote mbali na kudahili wanafunzi tu? Ukimpeleka mtoto wa masikini St Marian, nani atamlipia karo ya Tsh 2,000,000? Au baba yako atalipa? Acha ujuha ndugu yangu.
 
Back
Top Bottom