Uchunguzi wa mapacha njiti waliochunwa ngozi ya uso wakamilika. Wanne kufikishwa Mahakamani kwa Uvunaji wa Viungo vya Binadamu

Nyendo

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
1,194
4,112
1684749972628.png

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Burian @batilda.burian amesema jalada la uchunguzi wa tukio tata la Watoto pacha waliozaliwa kabla ya muda katika Kituo cha Afya Kaliua na mmoja wao kunyofolewa jicho la kulia na ngozi ya paji la uso, limekamilika na Watumishi wanne wa Kituo hicho watafikishwa Mahakamani wakati wowote kuanzia sasa.

Akiongea na CG FM Dkt. Batilda amesema uchunguzi umebaini miili ya Watoto hao ilitunzwa katika chumba cha Wauguzi na sio katika wodi ya Wazazi kama ilivyosemwa awali na Wauguzi hao.

RC Batilda amewataja Wauguzi hao kuwa ni Theresia Kakiziba, Asha Magidi, Paulo James na Benson Maikase na kwamba amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua kuwasimamisha kazi Wauguzi wengine wawili walioongezwa katika kesi hiyo.

Itakumbukwa tukio hilo lilitokea May 9, 2023 katika Kituo cha Afya Kaliua ambapo inadaiwa Mtoto mmoja kati ya wawili pacha waliozaliwa kabla ya muda na kufariki alinyofolewa jicho na kuondolewa ngozi ya paji la uso hali iliyozua taharuki iliyopelekea Familia ya Isaka Rafael kugoma kuzika miili ya Watoto hao hadi leo.

Pia soma:
 
Inasemekana Polisi na D.C walipewa taarifa wakapuuza kwanini serikali imekuwa kimya? Kama taarifa hizo ni uongo wakanushe lakini tumeona hatua zikichukuliwa baada ya wakubwa kuingilia kati. Hili halipaswi kupita bila kuwekwa sawa.

Wazazi wametoa taarifa zikapuuzwa na kuelekezwa akazike hivyo hivyo. Hao wauguzi ni watu wadogo sana pamoja na wao kuhusika direct lakini bila uwajibikaji hili bado ni tatizo.
 
Inasemekana Polisi na D.C walipewa taarifa wakapuuza kwanini serikali imekuwa kimya? Kama taarifa hizo ni uongo wakanushe lakini tumeona hatua zikichukuliwa baada ya wakubwa kuingilia kati. Hili halipaswi kupita bila kuwekwa sawa.

Wazazi wametoa taarifa zikapuuzwa na kuelekezwa akazike hivyo hivyo. Hao wauguzi ni watu wadogo sana pamoja na wao kuhusika direct lakini bila uwajibikaji hili bado ni tatizo.
Kama watumishi wadogo hivyo tena kwa level ya kata huko kaliua bado kuna ugumu wa kuwachukulia hatua, vipi mawaziri, makatibu wakuu wanaotajwa kwenye report ya CAG. Ndio maana nasema nchi hii hatupo serious kwenye lolote
 
"Miili ilitunzwa chumba cha wauguzi na sio wodi wazazi kama ilivyoelezwa"

Maswali,

Kiutaratibu miili ilipaswa kutunzwa wapi?

Nani alinyofoa viungo vya watoto?

Walinyofoaje?Lengo ni nini?

Haya maswali ndio ilipaswa uchunguzi ujibu,sio kuja na sentensi moja kwamba miili ilitunzwa sehemu tofauti na wa maelezo ya awali? Kwahio ndio uchunguzi huo?
 
Miili ilitunzwa chumba cha wauguzi na sio wodi wazazi kama ilivyoelezwa,

Maswali,

Kiutaratibu miili ilipaswa kutunzwa wapi?

Nani alinyofoa viungo vya watoto?

Walinyofoaje?Lengo ni nini?

Haya maswali ndio ilipaswa uchunguzi ujibu,sio kuja na sentensi moja kwamba miili ilitunzwa sehemu tofauti na wa maelezo ya awali? Kwahio ndio uchunguzi huo?
Inawezekana kabisa kuwa wauguzi huwa wanashirikiana na hao wanaojiita wachawi au walozi

Wanapewa thamani ndogo huku wakiuza utu wao
Mimi naona wabanwe sana mpaka wajue ni mara ngapi wamefanya hivyo?

Ushirikina umefanya nchi isiendelee kabisa kwa upumbavu wao
 
Hawa watoto waliuwawa kwa msukumo wa imani za kushirikina.

Kuna jamii bado zinajihushisha na ibada za kafara za watoto especially mapacha na hata maalbino.

Hii kitu isipochukuliwa hatua na kutokomezwa utaanza mchezo wa kuua watoto kabla hawajapokelewa na wazazi wao.

Mimi wangewarudisha hao watoto, hii kesi isingekwenda polisi. Ningekwenda kutafuta silaha ya moto , pistol ningetafuta hao wauguzi m'moja baada ya mwingine ningewauwa kikatili sana. Tena kwa kuficha evidence. Hadi nihakikishe wote wamekwisha.
 
Inawezekana kabisa kuwa wauguzi huwa wanashirikiana na hao wanaojiita wachawi au walozi

Wanapewa thamani ndogo huku wakiuza utu wao
Mimi naona wabanwe sana mpaka wajue ni mara ngapi wamefanya hivyo?

Ushirikina umefanya nchi isiendelee kabisa kwa upumbavu wao
Ni kweli inawezekana
 
Inasemekana Polisi na D.C walipewa taarifa wakapuuza kwanini serikali imekuwa kimya? Kama taarifa hizo ni uongo wakanushe lakini tumeona hatua zikichukuliwa baada ya wakubwa kuingilia kati. Hili halipaswi kupita bila kuwekwa sawa.

Wazazi wametoa taarifa zikapuuzwa na kuelekezwa akazike hivyo hivyo. Hao wauguzi ni watu wadogo sana pamoja na wao kuhusika direct lakini bila uwajibikaji hili bado ni tatizo.
Asingekuwa mzazi mwenye msimamo ingepita kimyakimya,imagine mtu mpaka anaanza kuomba msaada mtandaoni?
Je ni watoto wangapi wameshafanyiwa ukatili huo na imeachwa tu?
 
Inawezekana kabisa kuwa wauguzi huwa wanashirikiana na hao wanaojiita wachawi au walozi

Wanapewa thamani ndogo huku wakiuza utu wao
Mimi naona wabanwe sana mpaka wajue ni mara ngapi wamefanya hivyo?

Ushirikina umefanya nchi isiendelee kabisa kwa upumbavu wao
Unaambiwa mpaka hospitali humo kuna maagent kabisa
 
Wauguzi wanne katika mkoa wa Tabora Magharibi nchini Tanzania watafikishwa Mahakamani kwa kosa la kuvuna viungo vya watoto mapacha, afisa wa mkoa amesema.

Kamati iliyoundwa kuchunguza tukio hilo iligundua kuwa miili ya mapacha hao waliozaliwa kabla ya wakati wao ilikuwa imeharibika baada ya kufariki.

Mama huyo alikuta macho ya watoto wake yametobolewa na sehemu ya ngozi yao ikiwa imetoka kwenye paji la uso.

Mkuu wa mkoa wa Tabora, Batilda Buriani alisema wauguzi hao ambao wako chini ya ulinzi wamesimamishwa kazi. Alisema uvunaji wa viungo hivyo unahusishwa na uchawi.

Wauguzi hao waliipotosha kamati ya uchunguzi kwa madai ya uwongo kwamba miili hiyo ilihifadhiwa katika wadi ya wazazi wakati, ilipatikana katika chumba cha wauguzi, Bi Buriani aliongeza.

Wauguzi hao bado hawajazungumzia madai hayo.

Taarifa hiyo pia inaeleza kuwa pacha hao walifariki dunia kutokana na kukosa huduma za watoto wachanga ambazo hazikupatikana katika kituo walichozaliwa.
 
Back
Top Bottom