Uchunguzi huu umenishangaza Sana!

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,050
50,998
Kwema Wakuu!

Nimefanya uchunguzi mdogo nao ni huu;

"Wale wanaoonekana ni wajinga ndio wanawatawala werevu.
Wale wanaoonekana waovu ndio waliobarikiwa kimaisha.
Wale wanaoonekana wahuni na Malaya ndio wanaoimudu ndoa.

Wale wanaoonekana wengi ndio wanaotawaliwa na waliowachache.

Wale wenye Ujuzi na maarifa ndio wanaotafuta kazi.

Wale waliovipofu tena wasioona maana wapo vipofu wanaoona, sasa hawa ni vipofu wasioona kabisa ndio wanawaongoza wenye macho wanaoona

Wale wanaoonekana ni Wazalendo ndio wezi na wahujumu uchumi.

Wale wanaoogopa sheria ndio wanaokutwa na hatia, Ila wasioiogopa sheria na kuzivunja huwa wenye haki wasio na hatia.
Wale wanaoogopa kuoa na kuzaa kisa maisha ndio hao hao wenye maisha magumu kuliko Wale waliooa na wanaozaa.

Wale wanaoonekana kujibana kiuchumi ili wafanye maendeleo ndio haohao wanaoshindwa maendeleo na Wale wanaotumia pesa Rafu.

Wale wanaoonekana wazuri wa Sura na maumbile ndio haohao wanaokosa wenza wa kuwaona/kuolewa nao ndio wanaolalamika, wakati wasio na mvuto wakiolewa na kuoa kila uchwao.

Wale wanaopenda Kwa watu na vitu vya watu, kwao na vyao ni vibaya.

Wale wanaoonekana ni watumishi wa Mungu ndio haohao wachawi na mashetani Wabaya.

Wale wanaoonekana ni watumishi wa Shetani ndio haohao watumishi wa Mungu aliyehai.

Wale waliofeli Hesabu shuleni ndio wanaofaulu Hesabu za maisha. Huku Wale waliofaulu Hesabu za shuleni wakishindwa Hesabu za mtaani.

Wale WANAOPENDA kulala hawana vitanda na magodoro mazuri lakini ndio wanaolala usingizi mnono.

Wale WANAOPENDA kusoma, husoma habari za watu waliokataa na wasiopenda kusoma, walioshindwa shule.

Wale wanaolima chakula ndio huwa wakwanza kupata njaa, wakati wasiolima wala hawana habari wao chakula kipo Tele siku zote.

Wale wanaoonekana Wana silaha na ulinzi mkali ndio haohao usalama wao mi mdogo na hawana Amani wakati wasio na ulinzi wowote wanausalama Mkubwa na Amani ya roho

Wale wanaozingatia Sana mambo ya Afya ndio haohao hukumbwa zaidi na magonjwa tofauti na Wale wasiozingatia"

Hayo nayo niliyaona kwenye Siasa za Dunia.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Dar es salaam
 
Hao ndio na pengine wakaingia peponi kuliko hao uliowaona ni wanufaika ,inasemwa ni mitihani ya kuingia Peponi .au pia inasemwa ni mitihani ya Mwenyezi Mungu ,hivyo ni kupambana nayo usije ukakengeuka kwenda kwenye ushirikina ili uwe na hao wanufaika,bro itakuwa umefeleli na utanafasika kwenye vyumba vya motoni.

Jaribu sana kuridhika na maendeleo uliyonayo au ulichonacho ili kazi zingine ziendelee.

Utavuka mtihani unaoitwa strec.
 
hao ndio na pengine wakaingia peponi kuliko hao uliowaona ni wanufaika ,inasemwa ni mitihani ya kuingia Peponi .au pia inasemwa ni mitihani ya Mwenyezi Mungu ,hivyo ni kupambana nayo usije ukakengeuka kwenda kwenye ushirikina ili uwe na hao wanufaika,bro itakuwa umefeleli na utanafasika kwenye vyumba vya motoni.
jaribu sana kuridhika na maendeleo uliyonayo au ulichonacho ili kazi zingine ziendelee. Utavuka mtihani unaoitwa strec.


Inakuwaje werevu watawaliwe na wajinga?

Ama inakuwaje kipofu awaongoze wenye macho?
 
Maisha ni kama mahesabu ya mantiki na vikokotoo vyake.

Negation of false is truth

and

Negation of truth is false
 
Nilichogundua kwako mleta mada ni kuwa muda mwingi unafuatilia sana maisha ya watu ndio maana umeandika mengi kuhusu watu mbalimbali uliowafuatilia maisha yao

Watu wa aina yako wengi huwa maskini na bila kuficha na wewe uko hilo kundi

Maskini muda mwingi hufuatilia maisha ya watu wakati tajiri hujua mengi kuhusu utajiri wake au biashara zake MTU kama Mo Dewji au Bakhresa wa Azam hawezi kuwa na muda wa kuchunguza watu na kuandika hayo uliyoandika mleta mada.Ni maskini pekee ndie aweza
 
Nilichogundua kwako mleta mada in kuwa muda mwingi unafuatilia sana maisha ya watu ndio maana umeandika mengi kuhusu watu mbalimbali uliowafuatilia maisha yao

Watu wa aina yako wengi huwa maskini na Vila kuficha na wewe uko hilol kundi

Maskini muda mwingi hufuatilia maisha ya watu wakati tajiri hujua mengi kuhusu utajiri wake au biashara zake MTU kama Mo Dewji au Bakhresa wa Azam hawezi kuwa na muda wa kuchunguza watu na kuandika hayo uliyoandika mleta mada.Ni maskini pekee ndie aweza

Afadhali Umesema watu wengi na sio wote.

Kuna ishu ya Exceptional siku ukijua Jambo hili utafika mbali.

Wakati nasoma wapo watu waliodhani Kwa akili zao ndogo kuwa Kwa vile Mimi ni mjanja mjanja, sisomi na wala hawajawahi kuniona na Daftari wakadhani nitafeli

Lakini kumbe ni ujinga kufikiri kuwa watu wote ni Sawa.
NILIFAULU Kwa kiwango cha daraja la Kwanza tena nikiwa kinara katika Darasa letu Kwa mwaka huo.

Kidato cha sita halikadhalika hivyo hivyo, nilikuwa miongoni mwa waliofaulu Kwa daraja la Kwanza ambao tuliokuwa wachache.

Chuo kikuu nacho halikadhalika.

Ninachotaka kusema ni nini!

Wapumbavu hulijaji jalada la kitabu pasipo kujua ndani yake kuna nini.
Ndio watu kama wewe.

Wengine ni Exceptional.

Unaweza kumuona yupo hivi kumbe yupo vile
Unaweza muona anamaisha simple kumbe anautajiri.
Unaweza muona ni Tajiri kumbe ni masikini.

So mtazamo wako mara nyingi hupatikana Kwa watu wapumbavu.
 
Upo sahihi. Refer Newton's third law. Ipo applicable emotionally, physically, na virtually.
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom