Long'ututi
Member
- Dec 5, 2010
- 41
- 4
Ndugu zangu niwewaza sijapata jibu,kwa kifupi mimi ni mwanaume kijana niliyehitimu masomo chuo kikuu miaka miwili iliyopita,nina mchumba naye anasoma chuo kikuu binafsi hapa hapa tz,nilimfaham baada ya mimi kuhitimu chuo,tunapendana sana nishamtambulisha nyumbani na yeye kanitambulisha kwao,tatizo kumbe ana kigogo anamsomesha kwani form six hakufanya vizuri kuweza kulipiwa na bodi ya mikopo,ana uhusiano wa mapenzi na kigogo huyu na mimi sikujua mpaka nilipoona vyeti vyake vya shule na kugundua hasomeshwi na serikali,nilimbana akaniambia ukweli,msichana yupo mwaka wa pili,mimi uwezo wa kumlipia ada bado si kihivyo ndio maisha yanaanza kuchanganya,kumkatisha masomo si jambo la busara,sasa wandugu nifanyeje?