Uchumba kuvunjika ...kisa HARUSI

Uchumba kuvunjika ...kisa HARUSI

Wasalaam

Iko hivi ...Ni rafiki wa karibu wa familia yetu,ameajiriwa na taasisi ya fedha mwaka wa tatu huu Yuko kwenye mahusiano na mdada waliekutana chuo...Ni muda kiasi tunamuita shemeji yetu

Jamaa anataka kutoa mahari,lakini mwanamke amegoma anasema mpaka jamaa akubali sharti la kufanyika harusi

Familia ya jamaa yetu,Ni watu wenye uwezo wao kiasi,ila mzee wao Ni mtu wa kuchukia Sana Sherehe na harusi,anasema atachangia misiba na majanga mengine sio mambo ambayo mtu anayapanga mwenyewe halafu anasumbua watu kwa michango,ndivyo anavyishi

Dada za mshikaji wameozwa Tena kwa mahari ndogo,harusi hakuhudhuria,ila baada ya hapo aliwapa kiasi Fulani (kikubwa) Kama Cha kuanzia maisha,imekua utaratibu wake

Na mwaka Jana Kaka yake mshikaji kaoa kwa mtindo huo huo...alienda half day jmos...akatoka kuwaambia staff wenzie naenda funga ndoa ,hawakuamini,lakini jamaa alifunya ndoa,na home walikuja watu wachache tuu kwa ajili ya evening dinner

Jamaa anasema sio kuwa Hana uwezo,ila Ni namna Anaona atamhuzunisha mzee wake ..mzee wake kamwambia mikosi na mambo ya shetani huanzia kwenye tafrija/Sherehe...anasema Ni kujikweza...jamaa atanye Nini tukivaa viatu vyake?

Sent using Jamii Forums mobile app
Me naomba kama anampiga chini huyo mchumba wake basi aniachie tu namba yake. Labda na mimi nitakula tunda kimasihara ili nije nilete kisa changu kwenye ule uzi wetu pendwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wasalaam

Iko hivi ...Ni rafiki wa karibu wa familia yetu,ameajiriwa na taasisi ya fedha mwaka wa tatu huu Yuko kwenye mahusiano na mdada waliekutana chuo...Ni muda kiasi tunamuita shemeji yetu

Jamaa anataka kutoa mahari,lakini mwanamke amegoma anasema mpaka jamaa akubali sharti la kufanyika harusi

Familia ya jamaa yetu,Ni watu wenye uwezo wao kiasi,ila mzee wao Ni mtu wa kuchukia Sana Sherehe na harusi,anasema atachangia misiba na majanga mengine sio mambo ambayo mtu anayapanga mwenyewe halafu anasumbua watu kwa michango,ndivyo anavyishi

Dada za mshikaji wameozwa Tena kwa mahari ndogo,harusi hakuhudhuria,ila baada ya hapo aliwapa kiasi Fulani (kikubwa) Kama Cha kuanzia maisha,imekua utaratibu wake

Na mwaka Jana Kaka yake mshikaji kaoa kwa mtindo huo huo...alienda half day jmos...akatoka kuwaambia staff wenzie naenda funga ndoa ,hawakuamini,lakini jamaa alifunya ndoa,na home walikuja watu wachache tuu kwa ajili ya evening dinner

Jamaa anasema sio kuwa Hana uwezo,ila Ni namna Anaona atamhuzunisha mzee wake ..mzee wake kamwambia mikosi na mambo ya shetani huanzia kwenye tafrija/Sherehe...anasema Ni kujikweza...jamaa atanye Nini tukivaa viatu vyake?

Sent using Jamii Forums mobile app
Jamaa ni shaidi wa yehova huyo atakuwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
100%kwa uyo mzee, ni kama mm kabisa sijawah kuwa mfuasi wa sherehe zisizo na tija ndoa ni agano kati ya muaji,muolewaji na Mungu wao safi.piga chini uyo binti
 
Huyo mzee kama mzee wangu aisee... Tushakubaliana future husband akikubali tunafunga ndoa kanisani tena ikiwezekana ofisini kwa mchungaji jioni dinner ya familia. Sipendi misherehe na kuingia gharama za kijinga
 
Housegirl kaingiaje? 🤣🤣🤣
Huyo mzee wake namkubali kwa 100%

Kuhangaika na sherehe za harusi Hakuna Maana Wala mantiki yoyote, Ni uupuzi tu kwangu!!

Hata Mimi nikifika hatua ya kuoa Basi sitahangaika na upuuzi wa sherehe

House girl(dada wa kazi) Ni binadamu aheshimiwe, apumzike, apewe Uhuru wa kuabudu pia
 
Kuna binti alikua ni jirani yangu na tunaabudu sehemu moja .Basi bwana mi sina hili wala lile nikapewa taarifa/mualiko natakiwa kuwa mwanakamati kwa ajili ya hiyo send off ya huyo kigori .Changa mapesa kimbizana na michango bongeee la sherehe likafanyika.Nikaombwa tena kama kijana mwenye busara na heshima niongozane nao kwenye kufunga ndoa mji kasoro.Picha linaanza bwana harusi kasema yeye atahudumia watu wanne tu,mama wa biharusi kachukua ndugu ,majirani tumekaribia kujaza coaster 2 na nusu.Kufika kwenye eneo la tukio ,ndoa imefungwa kanisani tumerudi nyumbani tumekula ubwabwa pale zikapigwa picha mbili tatu Mc akatangaza jamani na huu ndio mwisho wa sherehe hakuna party hakuna nini.Wacha mama wa binti aanze kulia na kujigaragaza huku anamtaja jina bwana harusi kuwa kamdhalilisha,kamtia aibu kwa ndugu ,jamaa na marafiki.Nilichojifunza tunaongozwa sana na sifa kuliko uhalisia wa maisha.
 
Huyo mzee wake namkubali kwa 100%

Kuhangaika na sherehe za harusi Hakuna Maana Wala mantiki yoyote, Ni uupuzi tu kwangu!!

Hata Mimi nikifika hatua ya kuoa Basi sitahangaika na upuuzi wa sherehe

House girl(dada wa kazi) Ni binadamu aheshimiwe, apumzike, apewe Uhuru wa kuabudu pia
Duuh kweli Wanasuaso Akili zinafanana.. hata Mimi huo ujinga wa harusi siukubali hata kidogo.
Subri nikifikia hiyo hatua Wachache tu ndo watanielewa Ila wengi watakuja kunishangaa..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Narudia Tena kwa Akili zangu timamu Kufunga harusi na Mwanamke wa kizazi hiki Cha online Ni Ujinga wa kiwango Cha SGR.

Ninayo mifano mingi juu ya mbwembwe za harusi zilizofungika lkn leo ndo zinazidi kutuongezea Ma single mother na ma braza men mtaani kila kukichaa.

Pia Naunga jitihada na msimamo wa mzee wetu Mwenye Akili nyingi kwa asilimia zote.(He has motivated me to follow his action)

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom