Uchina itaiomba Tanzania (kama bado haijafanya hivyo) iwapatie kituo cha kijeshi (military base)

Sijali

JF-Expert Member
Sep 30, 2010
2,589
1,679
Habari zinazotembea hivi sasa ni kuwa punde hivi Uchina itaiomba Tanzania (kama bado haijafanya hivyo) iwapatie kituo cha kijeshi (military base). Kama ilivyoomba nchi kadhaa ikiwemo UAE, Pakistan, Tajikistan (UAE imekwishawapa).

Najua ombi hilo likifika Tanzania kuna wale watakaosema 'lakini siasa ya Tanzania ni kutofungamana na kokote!' Au, 'wajua sisi Tanzania ni nchi ya amani' au 'mbona hiyo itatuletea matatizo'na mambo mengi yanayoonesha ugandaji wa fikra za karne ya 20.

Zama zimeendelea mbele na hivi sasa kuna uhalisia mpya. Ukitazama jinsi mataifa yanavyofukuzana kushindana katika kutengeneza na kulimbikiza silaha, utajua kuwa it is a matter of time, kabla ya vita kuu ya dunia 3 kutinga. Katika vita kama hiyo hakuna atakayejali kuwa Tanzania ni 'nchi isiyofungamana na dola lolote'.

Linalotakikana sasa ni kuwa 'pragmatic' na kukubali ombi la nchi hii ambayo tayari ni namba 1 katika mambo mengi isipokuwa machache tu ambayo Marekani bado inaongoza (utengezaji wa ndege za abiria/kivita, nano technology, AI...).

Ni vizuri kuwa juu ya mgongo wa ndovu wakati chui anashambulia kuliko kuwa unatembea kwa miguu.

Kuna saikolojia inayomfanya mwingine aone anaweza kukuamini pindi unapokuwa tayari kumsaidia wakati wa dhiki, kuliko wakati tayari amepata ofa nyingine.

Faida za kuwepo military base Tanzania zitakuwa nyingi ikiwemo kupata ujuzi wa vyombo vya kisasa na pengine kuanzisha viwanda vya kutengeneza silaha za kisasa. Ili mradi tu mkataba utakaoingiwa uwe unatazama maslahi mapana ya Tanzania.
 
Kila mtu atakuja na maoni yake tofauti, tena hawa mayahudi/marekani weusi nawasubiri hapa watakuja na neno gani la "kupinga"kuhusu hii mada inayosema

WACHINA WAPEWE MILITARY BASE TANZANIA​


Mayahudi weusi karibuni sana
 
Wakikubaliwa na Tanzania ( Serikali ) pamoja na JWTZ Wenyewe naiona ile Safari ya Tanzania kuanza 'Kuchukiwa' na Marekani itaanza kwani inasemekana kuwa nchini Kenya Marekani ama wameshaweka hiyo 'base' yao au ndiyo wanajiandaa kuiweka sasa, hivyo uwepo wa China karibu yao kutakuwa ni tatizo na hata tishio Kwao.

Katika hili Umakini unahitajika sana tu.
 
Ukishawapa naval base ,utaweza kuwadhibiti wewe!? Zaidi ya wao kuudhibiti ukanda wote wa bahari kwa maslahi yao. Tamaa mbele mauti nyuma. Tafuteni vya kwenu. Ukorofi wa mchina kawaulize majirani zake huko baharini.
 
Wakikubaliwa na Tanzania ( Serikali ) pamoja na JWTZ Wenyewe naiona ile Safari ya Tanzania kuanza 'Kuchukiwa' na Marekani itaanza kwani inasemekana kuwa nchini Kenya Marekani ama wameshaweka hiyo 'base' yao au ndiyo wanajiandaa kuiweka sasa, hivyo uwepo wa China karibu yao kutakuwa ni tatizo na hata tishio Kwao.

Katika hili Umakini unahitajika sana tu.
Usiamue mambo ya nchi yako kwa kuhofia au kuogopa wengine. Amua kwa maslahi yako. Marekani inasaidia nini Tanzania?
 
UAE gani imekubali kuwa na military base ya Mchina? UAE ni US ally na kuna airbase ya kurusha drones kuzurula Middle East.

UAE haiwezi kubali kinjaanjaa kama Djibouti ilivyofanya. UAE anaomba kila siku US imuuzie F-35 alafu iruhusu base ya China si itakuwa kama kesi ya Turkey na S400 za Urusi. Alafu UAE haamini tena silaha za Mchina, US ilipokataa kumuuzia drones akaenda kwa China akauziwa drones zinadondoka ovyo. Kwa vile hana njaa akazigawa zile drones.

Ukiruhusu China iwe na base kwako usitarajie US akuuzie silaha. Hakuna anayetaka uwe unaoperate silaha zake wakati huo mifumo ya adui wake inakusoma vizuri kwa uwazi. US inaringa kuuza silaha na UAE inazitaka sana hizo made in US.

Sisi Tanzania njaa kali hata tukipewa silaha za Mchina zinazidi mahitaji yetu. Tuko situated sehemu nzuri hapa Afrika, ukitokea Tanzania unafika Kusini, Kaskazini, katikati kirahisi. Alafu tuko stable kiusalama na hatuna dalili za fujo. Ila tulikubali base ya yeyote lazima kuna vitu tutakosa au kupata. Sioni faida kubwa sana naona ni bora tuwe neutral
 
UAE wamekataa baada ya marekani kushinikiza.

Wachina wanaweza kuwa na base, syria lebanon, Lamu,, south africa, venezuela, pakistan, etc
 
Ukishawapa naval base ,utaweza kuwadhibiti wewe!? Zaidi ya wao kuudhibiti ukanda wote wa bahari kwa maslahi yao. Tamaa mbele mauti nyuma. Tafuteni vya kwenu. Ukorofi wa mchina kawaulize majirani zake huko baharini.
Inabidi uwe kanchi kalikojichokea na hakana maisha. Au uwe hatarini sana kushambuliwa ndio utoe eneo lako kuwa military base. Bora ukaribishe majeshi kwa muda kwenye airbase yako au kambi ya ardhi popote ila kwenye naval base ni vigumu nchi ihame baada ya kuijenga. Wakisemaga naval base hawa wajinga wote wanajenga military complex hapo hapo ndege zinatua na wanajeshi maelfu wapo.

Kuwa na base ya beberu ni ujinga mara nyingi. Guantanamo iko Cuba ila maamuzi yote yanatokea Marekani wamiliki wake na wana miaka zaidi ya 100 pale
 
UAE gani imekubali kuwa na military base ya Mchina? UAE ni US ally na kuna airbase ya kurusha drones kuzurula Middle East...
Vizuri umeuliza unataka kujua. Maana wengi hapa wanaposhindwa kujua wanatukana! Huu ndiyo upumbavu wa watu wetu.

Kwa ufupi, UAE ni nchi very pragmatic kama utafuata siasa zake. Hivi nisemavyo wanazungumza na Iran! Nataka Tanzania iwe hivyo na kujali maslahi yake tu. Hakuna mjomba kwenye siasa!

Juu ya habari hiyo ya base ya Wachina hebu google: 'UAE secret Chinese base' ujisomee mwenyewe.
 
Inabidi uwe kanchi kalikojichokea na hakana maisha. Au uwe hatarini sana kushambuliwa ndio utoe eneo lako kuwa military base. Bora ukaribishe majeshi kwa muda kwenye...
Inategemea mikataba. Guantanamo ilitolewa na Dikteta wa Cuba Batista kwa muda usiojulikana. Mimi ninachoongea ni mikataba mizuri. Pili usisikie tu.

Cuba yenyewe haitaki Wamarekani waondoke Guantanamo maana wanapata kodi, watu wao wanapata kazi.

Huu si mfano mzuri wa kutoa.
 
Serikali ya Afghanistan ilikua na military base ya marekani,

na Bado haikuambulia chochote zaidi ya kupinduliwa na taleban
Soma vizuri uzi wangu, usifananishe na uvamizi. Makubaliano ya kujenga base yanahusisha kukodisha ardhi kwa malipo, muda wa kukaa, nini kiingizwe n.k.
 
Wakikubaliwa na Tanzania ( Serikali ) pamoja na JWTZ Wenyewe naiona ile Safari ya Tanzania kuanza 'Kuchukiwa' na Marekani itaanza kwani inasemekana
Germany, France, Italy, United Kingdom, USA, China na Saudi Arabia wote hao wana military bases Djibouti yaani kanchi kadogo ila kamezungukwa na Wanajeshi wa kila aina

Na wote wamekaa karibu karibu sana
 
Back
Top Bottom