Uchi wa moto....!!!

Salaam wakuu,
Nipo huku kawe ukwamani kuna mama mmoja anaitwa mama upinde hua jioni anauza uji mmoja wa ngano aisee ni matata sana ukiunywa huachi. Sasa nipo kwenye benchi na wazee fulani hapa sasa kuna jamaa amekuja ametuchekesha wote. Jamaa ana accent kama ya watu wa kule nyanda za juu amekaa kwenye benchi akasema,"mama upinde naomba uchi wa moto. Mama upinde acha aanze kummind jamaa anamdhalilisha kumbe jamaa matamshi ya J, G kwake yanampa shida kabisa hadi mzee mmoja ndio akamuamulia. Anyways, mi ndio namalizia kikombe changu cha tatu hapa nianze mdogo mdogo kwenda home. Jioni njema jamani!
kudadadeki kesho nakuja Kawe kuupiga huo uchi wa moto!!
 
Back
Top Bottom