UCHAWI: Upo au haupo?

Mimi siamini katika miujiza yaani siamini Mungu wala Shetani, ila naamini katika sayansi na teknolojia
Tuko pamoja mkwepa Kodi, Uchawi wao haujawahi fanya kitu practicle na cha manufaa hata siku moja , hata kuzuia wizi wa makanikia, Pia swala la mungu ni mtambuka juhudi binafsi na maarifa ndo mafanikio yako ukitaka ujue hilo kashinde kanisani mwaka Mzima afu weka pambano na Mayweather aliyetoka kwenye strip club yake Jana ndo utajua
 
Hebu twende kwa mifano pengine utanielewa ....ninini kinafanya gari itembee
Four stroke engine cycle, kufupisha stori Mafuta mpaka yatakapoisha ni sawa na mkaa unawaka kwa chain reaction Kama ilivyo nuclear fusion
 
Kwann wachawi siyo matajiri?
Nn kinawafanya wawe masikini wakati wana uwezo?
Utajiri wao ni tunguli zao hawahitaji pesa kwakuwa wanapata kila wanachotaka at a click
Zile pesa kidogo wanazopokea ni sadaka na kifungo chako mwenyewe kama muhuri wa kukabiliana na kukubalina yale utakayoyafanya mwenyewe kwa maelekezo ya mganga
 
Utajiri wao ni tunguli zao hawahitaji pesa kwakuwa wanapata kila wanachotaka at a click
Zile pesa kidogo wanazopokea ni sadaka na kifungo chako mwenyewe kama muhuri wa kukabiliana na kukubalina yale utakayoyafanya mwenyewe kwa maelekezo ya mganga
kuna hali ya kupoteza hela na ukikopesha hairudi wanasema kuna hela yako imechukuliwa na wachawi je hii ni kweli? N aunajinasua vipi kwenye hali hii?!
 
Ndoto za kula ama kulishwa si tatizo sana ila inategemea unakula ama kulishwa nini. Maranyingi kibaya ni nyama ama kinywaji cha rangi nyekundu ama nyeusi
Fanya hivi wakati wa kulala lamba ndimu ,hata ukishtuka usiku lamba! Hii imewasaidia wengi na kama ni mambo ya kishirikina hiyo kitu itakata
 
Hodii wana jamvi mi ni mpya humu. Ila nilikua nikifatilia sana topic za mshana huwa napenda sana mada za kunifikirisha. Kama hii napata elimu na kujifunza zaidi maana ndo ulimwengu wenyewe huu na uchawi upo mpk kwenye biblia umeandikwa kwa sisi waamini wa bible. So usibishe sana kwa sababu kuna watu wana uishi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…